MUSAADA KWA WALE WENYE WAMEFIWA NA MUPENDWA WAO
Mambo Yenye Unapaswa Kutazamia
Hata kama wachunguzi wanasema kuwa mutu mwenye amefiwa anapaswa kupita mu hatua fulani za kuonyesha huzuni, kila mutu iko na namna yake ya pekee ya kuonyesha huzuni. Je, tofauti hizo zinamaanisha kama watu fulani wanahuzunika kidogo ao “wanazuia” hisia zao? Haiko vile kabisa. Hata kama kukubali huzuni na kuionyesha kunaweza kufanya mutu ajisikie muzuri, hakuna “njia moja tu ya muzuri” ya kuonyesha huzuni. Jambo hilo linategemea sana desturi ya mutu mwenye amefiwa, utu wake, na mambo yenye yalimupata mu maisha, na pia namna alipenda mutu mwenye amekufa.
HALI ITAKUWA MUBAYA KWA KIASI GANI?
Pengine watu wenye wamefiwa hawawezi kujua mambo yenye wanapaswa kutazamia kisha kifo cha mupendwa wao. Lakini kwa kawaida, kuko hisia na magumu mbalimbali yenye inatokea, na mara nyingi mutu anaweza kutazamia itokee. Tufikirie mambo yenye kufuata:
Kuwa na hisia nyingi sana. Kulia, kutamani kuona mutu mwenye alikufa, na hisia kubadilika haraka, ni mambo yenye inaweza kufikia mutu mwenye amefiwa. Zaidi ya kuwa na hisia, mutu mwenye amefiwa anaweza kukumbuka sana mupendwa wake na anaweza kuota ndoto. Hata hivyo, jambo la kwanza lenye linaweza kutokea ni kushtuka na kushindwa kuamini. Tiina anakumbuka vile alitenda wakati bwana yake Timo, alipatwa na kifo cha kushtukia. Anasema hivi: “Ku mwanzo nilisikia kama vile mwili hautumike tena. Ku mwanzo nilishindwa hata kulia. Nilichoka sana hivi kwamba wakati fulani ilikuwa nguvu kupumua. Sikuamini jambo lenye lilikuwa limefanyika.”
Pia, ni kawaida kuwa na mahangaiko, kisirani na kujilaumu. Ivan anasema hivi: “Kwa muda fulani kisha kifo cha Eric mutoto wetu mwanaume wa miaka 24, mimi na bibi yangu Yolanda, tulikasirika sana! Jambo hilo lilitushangaza, juu tulikuwa hatujawazaka kama tunaweza kukasirika. Tulijilaumu pia, juu tuliwaza kama pengine hatukufanya mengi zaidi ili kusaidia mutoto wetu.” Alejandro, mwenye bibi yake alikufa na ugonjwa wenye kukawia, alijisikia pia kuwa mwenye kosa. Anasema hivi: “Ku mwanzo, niliwaza kuwa, ikiwa Mungu anaruhusu niteseke hivi, ninapaswa kuwa mutu mubaya. Kisha, nilijisikia kuwa mwenye kosa, juu ilionekana kama vile nilikuwa ninamulaumu Mungu juu ya jambo lenye lilikuwa limefanyika.” Kostas mwenye tulizungumuzia mu habari yenye ilitangulia, yeye pia anasema hivi: “Wakati fulani hata nilimukasirikia Sophia juu alikufa. Kisha, kujisikia vile kulifanya nijilaumu. Kwa kweli, haikuwa kosa lake.”
Kushindwa kufikiri muzuri. Kuko wakati wenye mutu mwenye amefiwa anaweza kuwa na mawazo yenye haifuatane muzuri. Kwa mufano, mutu mwenye amefiwa anaweza kufikiri kuwa inawezekana kusikia mutu mwenye amekufa, ao kumuona. Pia, mutu mwenye amefiwa anaweza kushindwa kukaza akili juu ya jambo fulani ao kukumbuka. Tiina anasema hivi: “Wakati fulani tungekuwa na mazungumuzo, lakini ningetambua kuwa mawazo yangu ilikuwa fasi ingine! Wakati huo, mambo yenye yalifanyika mbele na kisha kifo cha Timo, yalikuja haraka sana mu akili yangu. Kushindwa kukaza akili juu ya mambo, kulileta pia mahangaiko.”
Mutu kupenda kuwa peke yake. Mutu mwenye huzuni kwa sababu ya kufiwa anaweza kukosa kutulia wakati iko na watu wengine. Kostas anasema hivi: “Wakati nilikuwa pamoja na watu wenye kuoana, nilijiona kama vile mugeni. Lakini pia wakati nilikuwa pamoja na watu wenye hawajaoa ao kuolewa, nilijiona kama mugeni.” Yolanda bibi ya Ivan, anakumbuka: “Ilikuwa nguvu sana kuwa kati ya watu wenye walilalamika juu ya magumu yenye yalionekana kuwa ya kidogo sana kama yangelinganishwa na magumu yetu! Kisha, kulikuwa watu wenye walituambia namna watoto wao walikuwa wanafanya maendeleo ya muzuri. Nilifurahi wakati waliniambia vile, lakini haikuwa mwepesi kuendelea kuwasikiliza. Mimi na bwana yangu tulielewa kuwa maisha inaendelea, lakini ni sisi njo tulikosa nia na uvumilivu.”
Matatizo ya Afya. Ni kawaida kupata mabadiliko katika hamu ya kula, kilo ya mwili kuongezeka ao kupunguka, ao kuwa na matatizo ya usingizi. Aaron anakumbuka jambo lenye lilitokea mwaka moja kisha kifo cha baba yake. Anasema hivi: “Nilifikia kabisa kuwa
na matatizo ya usingizi. Kila usiku niliamuka wakati uleule nikifiri juu ya kifo cha baba yangu.”Alejandro anakumbuka kama alikuwa na matatizo ya afya yenye ilikuwa nguvu kuelewa. Anasema hivi: “Mara mingi nilichunguzwa na munganga na alinihakikishia kama nilikuwa na afya ya muzuri. Niliwaza kuwa ni huzuni njo yenye ilifanya nikuwe na alama za mutu mwenye kugonjwa.” Alama hizo zilifikia kuisha. Hata hivyo, uamuzi wa Alejandro wa kuona munganga ulikuwa wenye hekima. Huzuni inaweza kupunguza uwezo wa mwili wa kujikinga na magonjwa, kufanya tatizo fulani la afya liongezeke, ao kutokeza tatizo lingine la afya.
Kuwa na magumu ya kufanya kazi za maana. Ivan anakumbuka: “Kisha kifo cha Eric, tulipaswa kujulisha jambo hilo kwa watu wa jamaa na marafiki, lakini pia kwa watu wengine kama vile mukubwa wake wa kazi na mutu mwenye alikuwa anamupangisha. Kulikuwa pia vikaratasi vingi vyenye kuombwa na sheria vyenye tulipaswa kujaza. Kisha tulipaswa kuangalia vitu vyenye Eric alikuwa navyo. Mambo hayo yote yalituomba kutumikisha sana akili hata kama wakati huo tulikuwa wenye kuchoka kiakili, kimwili, na hata kama tulikuwa na huzuni nyingi.”
Lakini kwa watu fulani, hali inakuwa nguvu kabisa kisha muda fulani, wakati wanakuwa na lazima ya kufanya mambo yenye yalikuwa yanafanywa na mupendwa wao mwenye alikufa. Jambo hilo lilimufikia Tiina. Anasema hivi: “Sikuzote Timo alikuwa anaangalia mambo yetu ya benki na mambo mengine yenye kuhusu biashara. Sasa mimi njo nilipaswa kuangalia mambo hayo, na hilo liliniongezea mahangaiko. Je, ningeweza kabisa kutimiza mambo yote hayo bila kufanya makosa?”
Magumu yenye tumezungumuzia hapo juu, ni kusema, ya kiakili, ya kimwili, na yenye kuhusu hisia, yanaonyesha kama inaweza kuwa nguvu sana kupambana na huzuni ya kufiwa. Ukweli ni kwamba, maumivu ya kufiwa na mupendwa yanaweza kuwa makali sana, lakini kujua hilo mbele ya wakati kunaweza kusaidia mutu mwenye amefiwa hivi karibuni avumilie. Kumbuka pia kama haiko kila mutu anapatwa na matokeo hayo yote yenye yanaweza kuletwa na huzuni. Zaidi ya hilo, watu wenye wamefiwa wanaweza kupata kitulizo kwa kujua kama hisia kali zenye kuletwa na huzuni ya kufiwa ni za kawaida.
NITAKUWAKA TENA NA FURAHA?
Kile unapaswa kutazamia: Maumivu ya kufiwa haiendeleake milele; inafikia kupunguka. Hilo halimaanishe kuwa mutu mwenye amefiwa “anapona” kabisa ao anasahau mupendwa wake. Lakini, maumivu makali yenye kuletwa na huzuni yanapunguka polepole. Yanaweza kutokea tena wakati mutu anakumbuka mambo fulani bila kutazamia, ao wakati wa siku fulani katika mwaka, kama vile siku ya ndoa ao siku yenye mupendwa alikufa, na mambo mengine. Lakini, watu wengi wanafikia kuwa na usawaziko katika namna yao ya kuonyesha hisia na wanafikia tena kukaza akili juu ya kazi zao za kila siku. Mambo inakuwa kabisa vile, wakati watu wa familia ao marafiki wanategemeza mutu mwenye amefiwa na wakati anakamata hatua zenye kufaa ili kuvumilia.
Hali hiyo itaendelea mupaka wakati gani? Kwa watu fulani, hali hiyo yenye kuwa mubaya zaidi inaweza kufanya miezi. Kwa watu wengi, hali hiyo inaweza kuchukua mwaka moja ao mbili mbele wajisikie muzuri zaidi. Na kwa watu fulani inaomba wakati murefu zaidi. a Alejandro anakumbuka: “Kwangu mimi, huzuni kubwa ya kufiwa ilifanya karibu miaka tatu.”
Ujivumilie. Kaza akili juu ya mambo ya leo, ufanye mambo kama zamani, na ujue kuwa maumivu ya kufiwa haiwezi kuendelea milele. Hata hivyo, ni mambo gani yenye unaweza kufanya ili kupunguza huzuni yako sasa na hata kuizuia iendelee bila sababu yoyote?
Hisia kali zenye kuletwa na huzuni ya kufiwa ni za kawaida
a Watu kidogo wanaweza kupatwa na huzuni kali sana na yenye kuendelea hivi kwamba huzuni hiyo imefikia kuitwa huzuni yenye kuwa “nguvu kuelewa” ao huzuni yenye “kukawia.” Watu kama hao wanaweza kuwa na lazima ya kusaidiwa na wanganga wa akili.