Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

MAISHA YA MUKRISTO

Zabihu ya Ukombozi Inafanya Ufufuo Uwezekane

Zabihu ya Ukombozi Inafanya Ufufuo Uwezekane

Ukumbusho unatutolea nafasi nzuri ya kuwaza sana juu ya baraka za wakati unaokuja, kama vile ufufuo; baraka hizo zitawezekana kupitia zabihu ya ukombozi. Yehova hakuwaumba wanadamu ili wakufe. Hiyo ndiyo sababu kifo cha mupendwa wetu ni kati ya mambo yenye inatuletea huzuni sana. (1Kor 15:26) Yesu alihuzunika kuona wanafunzi wake wakimulia Lazaro. (Yoh 11:33-35) Kwa kuwa Yesu ni mufano kamilifu wa Baba yake, tuko hakika kwamba Yehova anahuzunika pia wakati tunateseka moyoni kwa sababu mupendwa wetu anakufa. (Yoh 14:7) Yehova anangojea kwa hamu siku atawafufua watumishi wake, tunapaswa pia kungojea siku hiyo kwa hamu.—Ayu 14:14, 15.

Kwa sababu Yehova ni Mungu wa utaratibu, tuko na sababu ya kuamini kwamba ufufuo utafanywa kwa utaratibu. (1Kor 14:33, 40) Maziko hayatakuwa tena; pengine watu watakutana ili kuwakaribisha wale watafufuliwa. Je, unafikiri sana juu ya ufufuo, zaidi sana wakati unapoteza mupendwa wako? (2Kor 4:17, 18) Je, unamushukuru Yehova kwa zabihu ya ukombozi na kwa kutuonyesha katika Maandiko kwamba watu wenye wamekufa wataishi tena?—Kol 3:15.

  • Kati ya rafiki zako na watu wa familia yako ni nani unangojea kwa hamu sana kuwaona tena?

  • Ni watu gani wenye kutajwa katika Biblia unangojea kwa hamu kukutana nao na kuzungumuza nao?