Waamuzi 2:1-23

  • Onyo la malaika wa Yehova (1-5)

  • Kifo cha Yoshua (6-10)

  • Mungu anainua waamuzi ili kuokoa Israeli (11-23)

2  Kisha malaika wa Yehova+ akapanda kutoka Gilgali+ na kuenda Bokimu na kusema: “Niliwatosha Misri na kuwaleta katika inchi yenye niliapia mababu zenu.+ Pia nilisema, ‘Sitavunja hata kidogo agano langu pamoja na ninyi.+ 2  Na ninyi kwa upande wenu, musifanye agano pamoja na wakaaji wa inchi hii,+ mubomoe mazabahu zao.’+ Lakini hamukutii sauti yangu.+ Sababu gani mumefanya hivi? 3  Ndiyo maana nilisema pia, ‘Sitawafukuza mbele yenu,+ na watakuwa mutego kwenu,+ na miungu yao itawapoteza.’”+ 4  Wakati malaika wa Yehova aliambia Waisraeli wote maneno hayo, watu wakaanza kulia kwa sauti kubwa. 5  Kwa hiyo wakapatia mahali pale jina Bokimu,* na wakamutolea Yehova zabihu pale. 6  Wakati Yoshua aliruhusu watu waende, kila Mwisraeli akaenda kwenye uriti wake ili kukaa katika inchi.+ 7  Watu wakaendelea kumutumikia Yehova siku zote za Yoshua na siku zote za wazee wenye waliendelea kuishi kisha Yoshua kufa na wenye walikuwa wameona mambo yote makubwa yenye Yehova alitendea Israeli.+ 8  Kisha Yoshua mwana wa Nuni, mutumishi wa Yehova, akakufa na miaka mia moja na kumi (110).+ 9  Basi wakamuzika katika eneo la uriti wake kule Timnat-heresi,+ katika eneo lenye milima la Efraimu, upande wa kaskazini wa Mulima Gaashi.+ 10  Na watu wote wa kizazi hicho wakakusanywa pamoja na mababu zao,* na kizazi kingine kikatokea kisha wao chenye hakikumujua Yehova wala mambo yenye alikuwa amefanyia Israeli. 11  Basi Waisraeli wakafanya mambo ya mubaya mbele ya macho ya Yehova na wakatumikia* Mabaali.+ 12  Basi wakamuacha Yehova, Mungu wa baba zao, mwenye aliwatosha katika inchi ya Misri.+ Na wakafuata miungu mingine, miungu ya vikundi vya watu vyenye viliwazunguka pande zote,+ na wakaiinamia na kumukasirisha Yehova.+ 13  Wakamuacha Yehova na wakatumikia Baali na sanamu za Ashtoreti.+ 14  Basi kasirani ya Yehova ikawaka juu ya Israeli, akawatia katika mukono wa wanyanganyi wenye walinyanganya vitu vyao.+ Akawauzisha katika mukono wa maadui wenye waliwazunguka,+ na hawakuweza tena kusimama mbele ya maadui wao.+ 15  Kila mahali walienda, mukono wa Yehova ulikuwa juu yao ili kuwaletea musiba,+ kama vile Yehova alikuwa amesema na kama vile Yehova alikuwa amewaapia,+ na wakateseka sana.+ 16  Basi Yehova alikuwa anainua waamuzi wenye walikuwa wanawaokoa katika mukono wa wanyanganyi wao.+ 17  Lakini walikataa kusikiliza hata waamuzi hao na walifanya uasherati na miungu mingine na kuiinamia. Waliacha haraka njia yenye mababu zao walikuwa wametembea ndani yake, wenye walikuwa wametii amri za Yehova.+ Hawakufanya vile. 18  Kila wakati wenye Yehova aliwainulia waamuzi,+ Yehova alikuwa pamoja na muamuzi huyo na alikuwa anawaokoa katika mukono wa maadui wao siku zote za muamuzi huyo; kwa maana Yehova aliwasikilia huruma*+ kwa sababu ya kilio chao cha maumivu chenye kilitokezwa na wale wenye waliwakandamiza+ na wale wenye walikuwa wanawatendea mubaya. 19  Lakini wakati muamuzi huyo alikufa, walikuwa wanageuka na kutenda kwa upotovu zaidi kuliko baba zao kwa kufuata miungu mingine, kwa kuitumikia na kuiinamia.+ Hawakuacha matendo yao na tabia yao ya kuwa kichwa-nguvu. 20  Mwishowe kasirani ya Yehova ikawaka juu ya Israeli,+ na akasema: “Kwa sababu taifa hili limevunja agano langu+ lenye nilifanya pamoja na mababu zao na wamekataa kunitii,+ 21  mimi pia sitafukuza hata taifa moja kati ya mataifa yenye Yoshua aliacha wakati alikufa.+ 22  Itakuwa vile ili kujaribu Israeli kama watashika njia ya Yehova+ na kutembea katika njia hiyo kama vile baba zao walifanya.” 23  Kwa hiyo Yehova akaruhusu mataifa hayo yabakie. Hakuyafukuza haraka, wala hakuyatia katika mukono wa Yoshua.

Maelezo ya Chini

Maana yake “Wenye Kulia.”
Haya ni maneno ya kishairi yenye kumaanisha kifo.
Ao “wakaabudu.”
Ao “aliwasikitikia.”