Waamuzi 2:1-23
2 Kisha malaika wa Yehova+ akapanda kutoka Gilgali+ na kuenda Bokimu na kusema: “Niliwatosha Misri na kuwaleta katika inchi yenye niliapia mababu zenu.+ Pia nilisema, ‘Sitavunja hata kidogo agano langu pamoja na ninyi.+
2 Na ninyi kwa upande wenu, musifanye agano pamoja na wakaaji wa inchi hii,+ mubomoe mazabahu zao.’+ Lakini hamukutii sauti yangu.+ Sababu gani mumefanya hivi?
3 Ndiyo maana nilisema pia, ‘Sitawafukuza mbele yenu,+ na watakuwa mutego kwenu,+ na miungu yao itawapoteza.’”+
4 Wakati malaika wa Yehova aliambia Waisraeli wote maneno hayo, watu wakaanza kulia kwa sauti kubwa.
5 Kwa hiyo wakapatia mahali pale jina Bokimu,* na wakamutolea Yehova zabihu pale.
6 Wakati Yoshua aliruhusu watu waende, kila Mwisraeli akaenda kwenye uriti wake ili kukaa katika inchi.+
7 Watu wakaendelea kumutumikia Yehova siku zote za Yoshua na siku zote za wazee wenye waliendelea kuishi kisha Yoshua kufa na wenye walikuwa wameona mambo yote makubwa yenye Yehova alitendea Israeli.+
8 Kisha Yoshua mwana wa Nuni, mutumishi wa Yehova, akakufa na miaka mia moja na kumi (110).+
9 Basi wakamuzika katika eneo la uriti wake kule Timnat-heresi,+ katika eneo lenye milima la Efraimu, upande wa kaskazini wa Mulima Gaashi.+
10 Na watu wote wa kizazi hicho wakakusanywa pamoja na mababu zao,* na kizazi kingine kikatokea kisha wao chenye hakikumujua Yehova wala mambo yenye alikuwa amefanyia Israeli.
11 Basi Waisraeli wakafanya mambo ya mubaya mbele ya macho ya Yehova na wakatumikia* Mabaali.+
12 Basi wakamuacha Yehova, Mungu wa baba zao, mwenye aliwatosha katika inchi ya Misri.+ Na wakafuata miungu mingine, miungu ya vikundi vya watu vyenye viliwazunguka pande zote,+ na wakaiinamia na kumukasirisha Yehova.+
13 Wakamuacha Yehova na wakatumikia Baali na sanamu za Ashtoreti.+
14 Basi kasirani ya Yehova ikawaka juu ya Israeli, akawatia katika mukono wa wanyanganyi wenye walinyanganya vitu vyao.+ Akawauzisha katika mukono wa maadui wenye waliwazunguka,+ na hawakuweza tena kusimama mbele ya maadui wao.+
15 Kila mahali walienda, mukono wa Yehova ulikuwa juu yao ili kuwaletea musiba,+ kama vile Yehova alikuwa amesema na kama vile Yehova alikuwa amewaapia,+ na wakateseka sana.+
16 Basi Yehova alikuwa anainua waamuzi wenye walikuwa wanawaokoa katika mukono wa wanyanganyi wao.+
17 Lakini walikataa kusikiliza hata waamuzi hao na walifanya uasherati na miungu mingine na kuiinamia. Waliacha haraka njia yenye mababu zao walikuwa wametembea ndani yake, wenye walikuwa wametii amri za Yehova.+ Hawakufanya vile.
18 Kila wakati wenye Yehova aliwainulia waamuzi,+ Yehova alikuwa pamoja na muamuzi huyo na alikuwa anawaokoa katika mukono wa maadui wao siku zote za muamuzi huyo; kwa maana Yehova aliwasikilia huruma*+ kwa sababu ya kilio chao cha maumivu chenye kilitokezwa na wale wenye waliwakandamiza+ na wale wenye walikuwa wanawatendea mubaya.
19 Lakini wakati muamuzi huyo alikufa, walikuwa wanageuka na kutenda kwa upotovu zaidi kuliko baba zao kwa kufuata miungu mingine, kwa kuitumikia na kuiinamia.+ Hawakuacha matendo yao na tabia yao ya kuwa kichwa-nguvu.
20 Mwishowe kasirani ya Yehova ikawaka juu ya Israeli,+ na akasema: “Kwa sababu taifa hili limevunja agano langu+ lenye nilifanya pamoja na mababu zao na wamekataa kunitii,+
21 mimi pia sitafukuza hata taifa moja kati ya mataifa yenye Yoshua aliacha wakati alikufa.+
22 Itakuwa vile ili kujaribu Israeli kama watashika njia ya Yehova+ na kutembea katika njia hiyo kama vile baba zao walifanya.”
23 Kwa hiyo Yehova akaruhusu mataifa hayo yabakie. Hakuyafukuza haraka, wala hakuyatia katika mukono wa Yoshua.
Maelezo ya Chini
^ Maana yake “Wenye Kulia.”
^ Haya ni maneno ya kishairi yenye kumaanisha kifo.
^ Ao “wakaabudu.”
^ Ao “aliwasikitikia.”