Muhubiri 6:1-12
6 Kuko jambo lingine la mubaya sana lenye* nimeona chini ya jua, na linatokea mara nyingi kati ya wanadamu:
2 Mungu wa kweli anapatia mutu utajiri na vitu vya kimwili na utukufu, na hivyo mutu hakose kitu chochote chenye anatamani;* lakini Mungu wa kweli hamuwezeshe kuvifurahia, hata kama mugeni anaweza kuvifurahia. Jambo hili ni bure* na ni mateso makubwa.
3 Kama mwanaume anazaa watoto mia moja (100) na kuishi miaka mingi na kuzeeka, lakini hafurahie* vitu vyake vya muzuri mbele aingie katika kaburi,* ninapaswa kusema kwamba mutoto mwenye alizaliwa akiwa amekufa anashindia mwanaume huyo.+
4 Kwa maana mutoto huyo alikuja bure na kuenda katika giza, na jina lake limefunikwa katika giza.
5 Hata kama hakuona jua wala kujua kitu, anashindia* tu mwanaume huyo.+
6 Kuko faida gani kuishi miaka elfu moja (1 000) mara mbili bila kuwa na furaha? Je, wote hawaende mahali pamoja?+
7 Kazi yote ya nguvu yenye mutu anafanya ni kwa ajili ya kujaza kinywa chake;+ lakini hamu yake ya kula* haitoshelezwe hata kidogo.
8 Kwa maana mwenye hekima anamupita mujinga kwa njia gani,+ ao mutu maskini anapata faida gani kwa sababu ya kujua kupambana na maisha?*
9 Ni muzuri zaidi kufurahia mambo yenye macho yanaona kuliko mutu kuhangaikia tamaa zake.* Jambo hili pia ni bure,* ni kufuatilia upepo.
10 Kila kitu chenye kiko kimekwisha kupewa jina, na inajulikana mwanadamu ni nini; na hawezi kubishana na* ule mwenye kuwa na nguvu kuliko yeye.
11 Wingi wa maneno,* ni wingi wa mambo ya bure;* na maneno mengi yanamuletea mwanadamu faida gani?
12 Ni nani anajua jambo la muzuri zaidi kwa mwanadamu kufanya katika siku kidogo za maisha yake ya bure,* yenye anapitisha kama kivuli?+ Kwa maana ni nani anaweza kumuambia mambo yenye yatatokea chini ya jua kisha yeye kufa?
Maelezo ya Chini
^ Ao “musiba mwingine mubaya sana wenye.”
^ Ao “hakose kitu chochote kwa ajili ya nafsi yake.”
^ Ao “ubatili.”
^ Ao “nafsi yake haifurahie.”
^ Ao “na hata kaburi halijakuwa lake.”
^ Tnn., “iko na pumuziko zaidi kuliko.”
^ Ao “nafsi yake.”
^ Tnn., “kutembea mbele ya wazima.”
^ Tnn., “kutanga-tanga kwa nafsi.”
^ Ao “ubatili.”
^ Ao “kutetea jambo lake mbele ya.”
^ Ao pengine, “vitu.”
^ Ao “ubatili.”
^ Ao “ubatili.”