Muhubiri 6:1-12

  • Mali bila furaha (1-6)

  • Furahia vitu vyenye uko navyo sasa (7-12)

6  Kuko jambo lingine la mubaya sana lenye* nimeona chini ya jua, na linatokea mara nyingi kati ya wanadamu: 2  Mungu wa kweli anapatia mutu utajiri na vitu vya kimwili na utukufu, na hivyo mutu hakose kitu chochote chenye anatamani;* lakini Mungu wa kweli hamuwezeshe kuvifurahia, hata kama mugeni anaweza kuvifurahia. Jambo hili ni bure* na ni mateso makubwa. 3  Kama mwanaume anazaa watoto mia moja (100) na kuishi miaka mingi na kuzeeka, lakini hafurahie* vitu vyake vya muzuri mbele aingie katika kaburi,* ninapaswa kusema kwamba mutoto mwenye alizaliwa akiwa amekufa anashindia mwanaume huyo.+ 4  Kwa maana mutoto huyo alikuja bure na kuenda katika giza, na jina lake limefunikwa katika giza. 5  Hata kama hakuona jua wala kujua kitu, anashindia* tu mwanaume huyo.+ 6  Kuko faida gani kuishi miaka elfu moja (1 000) mara mbili bila kuwa na furaha? Je, wote hawaende mahali pamoja?+ 7  Kazi yote ya nguvu yenye mutu anafanya ni kwa ajili ya kujaza kinywa chake;+ lakini hamu yake ya kula* haitoshelezwe hata kidogo. 8  Kwa maana mwenye hekima anamupita mujinga kwa njia gani,+ ao mutu maskini anapata faida gani kwa sababu ya kujua kupambana na maisha?* 9  Ni muzuri zaidi kufurahia mambo yenye macho yanaona kuliko mutu kuhangaikia tamaa zake.* Jambo hili pia ni bure,* ni kufuatilia upepo. 10  Kila kitu chenye kiko kimekwisha kupewa jina, na inajulikana mwanadamu ni nini; na hawezi kubishana na* ule mwenye kuwa na nguvu kuliko yeye. 11  Wingi wa maneno,* ni wingi wa mambo ya bure;* na maneno mengi yanamuletea mwanadamu faida gani? 12  Ni nani anajua jambo la muzuri zaidi kwa mwanadamu kufanya katika siku kidogo za maisha yake ya bure,* yenye anapitisha kama kivuli?+ Kwa maana ni nani anaweza kumuambia mambo yenye yatatokea chini ya jua kisha yeye kufa?

Maelezo ya Chini

Ao “musiba mwingine mubaya sana wenye.”
Ao “hakose kitu chochote kwa ajili ya nafsi yake.”
Ao “ubatili.”
Ao “nafsi yake haifurahie.”
Ao “na hata kaburi halijakuwa lake.”
Tnn., “iko na pumuziko zaidi kuliko.”
Ao “nafsi yake.”
Tnn., “kutembea mbele ya wazima.”
Tnn., “kutanga-tanga kwa nafsi.”
Ao “ubatili.”
Ao “kutetea jambo lake mbele ya.”
Ao pengine, “vitu.”
Ao “ubatili.”
Ao “ubatili.”