Kutoka 15:1-27

  • Wimbo wa ushindi wa Musa na Israeli (1-19)

  • Miriamu anaimba kwa kuitikia wanaume (20, 21)

  • Maji machungu yanageuzwa kuwa matamu (22-27)

15  Wakati huo Musa na Waisraeli wakamuimbia Yehova wimbo huu:+ “Nimuimbie Yehova, kwa maana ametukuzwa sana.+ Farasi na mupandaji wake amewatupa katika bahari.+   Nguvu zangu na uwezo wangu ni Yah,* kwa maana amekuwa wokovu wangu.+ Huyu ndiye Mungu wangu, na nitamusifu;+ Mungu wa baba yangu,+ na nitamutukuza.+   Yehova ni mupiganaji-vita mwenye nguvu.+ Yehova ni jina lake.+   Ametupa magari ya Farao na jeshi lake katika bahari,+Na wapiganaji-vita wake wenye nguvu zaidi wamezama katika Bahari Nyekundu.+   Maji yenye mawimbi makubwa yaliwafunika; walishuka kama jiwe katika sehemu za chini kabisa.+   Mukono wako wa kuume, Ee Yehova, uko na nguvu nyingi;+Mukono wako wa kuume, Ee Yehova, unaweza kumuvunja-vunja adui.   Katika wingi wa ukubwa wako unaweza kuangusha chini wale wenye kusimama ili kukupinga;+Unatuma kasirani yako yenye kuwaka, inawateketeza kama majani yenye kukauka.   Kwa pumuzi ya matundu ya pua yako maji yalijikusanya pamoja;Yalisimama imara, yalizuia mafuriko yasiteremuke;Maji yenye mawimbi makubwa yaligandamana katika moyo wa bahari.   Adui alisema, ‘Nitafuatilia! Nitafikia! Nitagawanya vitu vyenye vinachukuliwa katika vita mupaka nitosheke!* Nitachomoa upanga wangu! Mukono wangu utawanyenyekeza!’+ 10  Ulipuliza kwa pumuzi yako, bahari ikawafunika;+Walizama kama risasi katika maji makubwa. 11  Ni nani kati ya miungu mwenye kuwa kama wewe, Ee Yehova?+ Ni nani mwenye kuwa kama wewe, mwenye kujionyesha kuwa mwenye nguvu katika utakatifu?+ Mwenye anapaswa kuogopwa kwa kumuimbia nyimbo za sifa, Mwenye anatenda mambo ya ajabu.+ 12  Ulinyoosha mukono wako wa kuume, na dunia ikawameza.+ 13  Kwa upendo wako mushikamanifu umeongoza watu wenye ulikomboa;+Kwa nguvu zako utawaongoza kwenye makao yako matakatifu. 14  Vikundi vya watu vitasikia+ na kutetemeka;Wakaaji wa Ufilisti watashikwa na uchungu.* 15  Wakati huo mashehe* wa Edomu wataogopa sana,Na kutetemeka kutashika watawala wenye nguvu* wa Moabu.+ Wakaaji wote wa Kanaani watavunjika moyo.+ 16  Woga na hofu vitaanguka juu yao.+ Kwa sababu ya mukono wako wenye nguvu watabakia bila kutikisika kama jiweMupaka watu wako wapite, Ee Yehova,Mupaka watu wenye ulitokeza+ wapite.+ 17  Utawaleta na kuwapanda katika mulima wa uriti wako,+Mahali kwenye kulifanywa imara kwenye ulijitayarishia ili ukae pale, Ee Yehova,Patakatifu, Ee Yehova, kwenye mikono yako imejenga. 18  Yehova atatawala akiwa mufalme milele na milele.+ 19  Wakati farasi za Farao pamoja na magari yake ya vita na maaskari wake wapanda-farasi waliingia katika bahari,+Basi Yehova alirudisha maji ya bahari juu yao,+Lakini watu wa Israeli walitembea juu ya inchi kavu katikati ya bahari.”+ 20  Kisha Miriamu nabii mwanamuke, dada ya Haruni, akakamata ngoma ya kidogo* katika mukono wake, na wanamuke wote wakamufuata wakiwa na ngoma za kidogo* na walikuwa wanacheza dansi. 21  Miriamu alikuwa anaimba hivi kwa kuitikia wanaume: “Mumuimbie Yehova, kwa maana ametukuzwa sana.+ Farasi na mupandaji wake amewatupa katika bahari.”+ 22  Kisha wakati fulani Musa akaongoza Israeli kutoka kwenye Bahari Nyekundu, na wakaenda kwenye jangwa la Shuri na kusafiri kwa siku tatu (3) katika jangwa, lakini hawakupata maji. 23  Wakafika Mara,*+ lakini hawakuweza kunywa maji ya Mara kwa sababu yalikuwa machungu. Ndiyo sababu aliita mahali pale Mara. 24  Kwa hiyo watu wakaanza kumunungunikia Musa,+ kwa kusema: “Tutakunywa nini?” 25  Musa akamulilia Yehova,+ na Yehova akamuongoza kwenye muti fulani. Wakati alitupa muti huo ndani ya maji hayo, maji hayo yakakuwa matamu. Pale Mungu akawawekea sharti na musingi wa hukumu, na pale akawatia katika jaribu.+ 26  Mungu akasema: “Kama utasikiliza kabisa sauti ya Yehova Mungu wako na kufanya mambo yenye kuwa sawa mbele ya macho yake na kusikiliza kwa uangalifu amri zake na kushika masharti yake yote,+ sitakuletea magonjwa yenye nilileta juu ya Wamisri,+ kwa sababu mimi, Yehova, niko nakuponyesha.”+ 27  Kisha wakafika Elimu, mahali kwenye kulikuwa chemchemi kumi na mbili (12) na miti ya mitende makumi saba (70). Kwa hiyo wakapiga kambi pale pembeni ya maji.

Maelezo ya Chini

“Yah” ni kifupi cha jina Yehova.
Ao “nafsi yangu itosheke.”
Tnn., “maumivu ya kuzaa.”
Shehe alikuwa mukubwa wa kabila.
Ao “viongozi wenye kutawala kwa nguvu.”
Ao “tari.”
Ao “matari.”
Maana yake “Uchungu.”