Kumbukumbu la Torati 24:1-22

  • Ndoa na kuvunja ndoa (1-5)

  • Kuheshimia uzima (6-9)

  • Kuhangaikia maskini (10-18)

  • Sheria kuhusu kuokota masalio (19-22)

24  “Kama mwanaume anamuoa mwanamuke lakini hapendezwe naye kwa sababu alipata jambo fulani lenye halifae juu yake, anapaswa kuandika cheti cha kuvunja ndoa kwa ajili ya mwanamuke huyo,+ kumupatia cheti hicho, na kumufukuza atoke katika nyumba yake.+ 2  Kisha yeye kuondoka katika nyumba ya mwanaume huyo, anaweza kuenda na kuwa bibi ya mwanaume mwingine.+ 3  Kama mwanaume huyo wa pili anamuchukia* na anamuandikia cheti cha kuvunja ndoa, anamupatia cheti hicho, na anamufukuza katika nyumba yake ao kama mwanaume huyo wa pili mwenye alimuoa anakufa, 4  bwana yake wa kwanza mwenye alimufukuza hataruhusiwa kumuchukua tena ili akuwe bibi yake kisha mwanamuke huyo kuchafuliwa, kwa maana jambo hilo ni chukizo kwa Yehova. Haupaswe kuleta zambi katika inchi yenye Yehova Mungu wako anakupatia kuwa uriti. 5  “Wakati mwanaume ameoa karibuni, hatatumika katika jeshi ao kupewa kazi ingine yoyote. Atakuwa huru kwa mwaka mumoja na atabakia katika nyumba yake na kumufurahisha bibi yake.+ 6  “Mutu yeyote hapaswe kukamata jiwe la kusagia la mukono ao jiwe la juu la kusagia kuwa kitu chenye kinawekeshwa kwa ajili ya mukopo,+ kwa sababu kufanya vile ni sawa na kukamata riziki ya* mutu kuwa kitu chenye kinawekeshwa kwa ajili ya mukopo. 7  “Kama mutu anapatikana amemubeba kwa nguvu ndugu yake Mwisraeli na amemutesa na kumuuzisha,+ mutu huyo mwenye kubeba watu kwa nguvu anapaswa kufa.+ Unapaswa kuondoa mambo ya mubaya katikati yako.+ 8  “Wakati ukoma* unatokea, ukuwe muangalifu sana ili kufanya kulingana na mambo yote yenye makuhani Walawi watawaagiza.+ Mukuwe waangalifu ili kufanya sawasawa na vile niliamuru makuhani Walawi. 9  Kumbuka namna Yehova Mungu wako alimutendea Miriamu katika njia wakati mulikuwa munatoka Misri.+ 10  “Kama unamukopesha jirani yako kitu chochote,+ haupaswe kuingia katika nyumba yake ili kumunyanganya kitu chenye ameahidi kuwekesha kwa ajili ya mukopo. 11  Utasimama inje, na mutu huyo mwenye alipokea mukopo atakuletea inje kitu chenye anawekesha kwa ajili ya mukopo. 12  Na kama mutu huyo iko* katika uhitaji, haupaswe kulala na ungali na kitu chenye aliwekesha kwa ajili ya mukopo.+ 13  Unapaswa kabisa kumurudishia kitu chenye amewekesha kwa ajili ya mukopo wakati tu jua linashuka, na ataenda kulala akiwa na nguo yake,+ na atakubariki; na hilo litamaanisha haki kwa ajili yako mbele ya Yehova Mungu wako. 14  “Haupaswe kupunja mufanyakazi wa kulipwa mwenye kuwa katika uhitaji na mwenye iko* maskini, akuwe mumoja wa ndugu zako ao mukaaji mugeni katika inchi yako, ndani ya miji yako.*+ 15  Utamupatia mushahara wake siku ileile,+ mbele ya jua kushuka, kwa sababu iko* katika uhitaji na uzima wake unategemea* mushahara wake. Kama haufanye vile, atamulilia Yehova kwa sababu yako, na utakuwa na hatia ya zambi.+ 16  “Baba hawapaswe kuuawa kwa sababu ya mambo yenye watoto wao wanafanya, na watoto hawapaswe kuuawa kwa sababu ya mambo yenye baba zao wanafanya.+ Kila mutu anapaswa kuuawa kwa sababu tu ya zambi yake mwenyewe.+ 17  “Haupaswe kupotosha hukumu ya mukaaji mugeni ao ya mutoto mwenye hana baba,*+ na haupaswe kukamata nguo ya mujane kuwa kitu chenye kinawekeshwa kwa ajili ya mukopo.+ 18  Kumbuka kwamba ulikuwa mutumwa katika Misri, na Yehova Mungu wako akakukomboa kutoka kule.+ Ndiyo sababu ninakuamuru ufanye vile. 19  “Wakati unavuna mavuno yako katika shamba lako na unasahau fungu la mbegu katika shamba, usirudie ili kulikamata. Litaachwa kwa ajili ya mukaaji mugeni, mutoto mwenye hana baba, na mujane,+ ili Yehova Mungu wako akubariki katika mambo yote yenye unafanya.+ 20  “Wakati unapiga muzeituni ili kuangusha zeituni, haupaswe kufanya vile tena kwenye matawi yake. Zeituni zenye kubakia zitakuwa za mukaaji mugeni, mutoto mwenye hana baba, na mujane.+ 21  “Wakati unakusanya zabibu katika shamba lako la mizabibu, haupaswe kurudia kukusanya masalio. Yataachwa kwa ajili ya mukaaji mugeni, mutoto mwenye hana baba, na mujane. 22  Kumbuka kwamba ulikuwa mutumwa katika inchi ya Misri. Ndiyo sababu ninakuamuru ufanye vile.

Maelezo ya Chini

Ao “anamukataa.”
Ao “kukamata uzima wa; kukamata nafsi ya.”
Neno la Kiebrania lenye kutafsiriwa “ukoma” liko na maana nyingi na linaweza kutia ndani magonjwa mbalimbali yenye kuambukizwa ya ngozi. Linaweza pia kutia ndani magonjwa fulani yenye kuambukizwa yenye yanapatikana kwenye nguo na ndani ya nyumba.
Ao “eko.”
Ao “eko.”
Tnn., “milango yako mikubwa.”
Ao “eko.”
Ao “nafsi yake inategemea.”
Ao “yatima.”