Kumbukumbu la Torati 23:1-25

  • Wenye hawaruhusiwe katika kutaniko la Mungu (1-8)

  • Usafi wa kambi (9-14)

  • Watumwa wenye walikimbia (15, 16)

  • Ukahaba unakatazwa (17, 18)

  • Kulipisha faida na naziri (19-23)

  • Vitu vyenye wapita-njia wanaruhusiwa kula (24, 25)

23  “Mwanaume yeyote mwenye amefanywa kuwa towashi kwa sababu mapumbu yake yamepondwa ao mwenye amekatwa kiungo chake cha kiume hapaswe kuingia katika kutaniko la Yehova.+  “Mwana-haramu yeyote hapaswe kuingia katika kutaniko la Yehova.+ Hata kufikia kizazi cha kumi (10), muzao wake yeyote hapaswe kuingia katika kutaniko la Yehova.  “Mwamoni ao Mumoabu yeyote hapaswe kuingia katika kutaniko la Yehova.+ Hata kufikia kizazi cha kumi (10), muzao wao yeyote hapaswe kuingia hata siku moja katika kutaniko la Yehova,  kwa sababu hawakuwasaidia na chakula na maji wakati mulikuwa katika njia kutoka Misri,+ na kwa sababu walimulipa Balaamu mwana wa Beori kutoka Petori kule Mesopotamia ili awalaani* ninyi.+  Lakini Yehova Mungu wako alikataa kumusikiliza Balaamu.+ Kuliko kufanya vile, Yehova Mungu wako alibadilisha laana hiyo kuwa baraka kwa ajili yako,+ kwa sababu Yehova Mungu wako alikupenda.+  Haupaswe hata kidogo kuhangaikia hali njema yao wala mafanikio yao siku zako zote.+  “Haupaswe kumuchukia Mwedomu, kwa sababu yeye ni ndugu yako.+ “Haupaswe kumuchukia Mumisri, kwa sababu ulikuwa mukaaji mugeni katika inchi yake.+  Kizazi cha tatu (3) cha watoto wao wenye watazaa kinaweza kuingia katika kutaniko la Yehova.  “Wakati unapiga kambi ili kupigana na maadui wako, unapaswa kuepuka kitu chochote kibaya.*+ 10  Kama mwanaume anakuwa muchafu kwa sababu ametokwa na mbegu za uzazi* usiku,+ anapaswa kuenda inje ya kambi na asirudie katika kambi. 11  Wakati inafika mangaribi, anapaswa kunawa maji, na kisha anaweza kurudia katika kambi wakati jua linashuka.+ 12  Mahali pa faraga* panapaswa kuwekwa ili patumiwe inje ya kambi, na ni pale unapaswa kuenda. 13  Kipande kidogo cha muti kinapaswa kuwa katika vitu vyako. Wakati unashutama inje, unapaswa kukitumia ili kuchimba shimo na kisha ufunike mavi yako. 14  Kwa maana Yehova Mungu wako anatembea katika kambi yako+ ili kukukomboa na kutia maadui wako katika mukono wako, na kambi yako inapaswa kuwa takatifu,+ ili asione kitu chochote chenye hakifae katikati yako na ageuke na kuacha kutembea pamoja na wewe. 15  “Haupaswe kumutia mutumwa katika mukono wa bwana wake wakati anamukimbia bwana wake na kuja kwako. 16  Anaweza kukaa kati yako mahali popote penye atachagua katika muji mumoja kati ya miji yako, popote penye anapenda. Haupaswe kumutendea mubaya.+ 17  “Binti yeyote kati ya mabinti wa Israeli hapaswe kuwa kahaba wa hekalu,+ wala mwana yeyote kati ya wana wa Israeli hapaswe kuwa kahaba wa hekalu.+ 18  Haupaswe kuleta malipo ya kahaba mwanamuke ao malipo ya* kahaba mwanaume* katika nyumba ya Yehova Mungu wako ili kutimiza naziri, kwa sababu vyote viwili ni chukizo kwa Yehova Mungu wako. 19  “Haupaswe kumulipisha ndugu yako faida,+ ikuwe faida juu ya feza, juu ya chakula, ao juu ya kitu chochote chenye faida inaweza kuombwa juu yake. 20  Unaweza kumulipisha mugeni faida,+ lakini haupaswe kumulipisha ndugu yako faida,+ ili Yehova Mungu wako akubariki katika kazi zako zote katika inchi yenye unaenda kuriti.+ 21  “Kama unafanya naziri kwa Yehova Mungu wako,+ usikawie kuitimiza.+ Kwa maana Yehova Mungu wako hakika atakudai naziri hiyo; kama sivyo, utakuwa umetenda zambi.+ 22  Lakini kama unajizuia kufanya naziri, hautakuwa na hatia ya zambi.+ 23  Unapaswa kutimiza neno la midomo yako,+ na unapaswa kutimiza naziri yenye ulifanya kwa kinywa chako mwenyewe ili kuwa toleo la kujipendea kwa Yehova Mungu wako.+ 24  “Kama unaingia katika shamba la mizabibu la jirani yako, unaweza kula zabibu za kutosha ili kutosheleza hamu yako ya kula,* lakini haupaswe kutia zabibu zozote katika chombo chako.+ 25  “Kama unaingia katika shamba la nafaka yenye kusimama ya jirani yako, unaweza kuchuma kwa mukono wako masuke yenye kukomaa, lakini haupaswe kutia mundu* kwenye nafaka ya jirani yako.+

Maelezo ya Chini

Ao “aite ubaya juu yenu.”
Ao “chenye kuchafua.”
Ao “shahawa.”
Ni kusema, musalani, choo, W.C.
Ao “mapato ya.”
Tnn., “imbwa.”
Ao “kutosheleza nafsi yako.”
Mundu ni kisu chenye kujikunja chenye kinatumiwa ili kuvuna.