Kumbukumbu la Torati 1:1-46

  • Kuondoka kwenye Mulima Horebu (1-8)

  • Wakubwa na waamuzi wanawekwa (9-18)

  • Watu wanakosa kutii kule Kadesh-barnea (19-46)

    • Israeli anakataa kuingia katika ile inchi (26-33)

    • Hawaweze kukamata Kanaani (41-46)

1  Haya ndiyo maneno yenye Musa aliambia Israeli wote katika eneo la Yordani katika jangwa, katika maeneo tambarare ya jangwa mbele ya Sufi, katikati ya Parani, Tofeli, Labani, Haseroti, na Dizahabu.  Ni safari ya siku kumi na moja (11) kutoka Horebu mupaka Kadesh-barnea+ kupitia njia ya Mulima Seiri.  Katika mwaka wa makumi ine (40),+ mwezi wa kumi na moja (11), siku ya kwanza ya mwezi huo, Musa akasema na Waisraeli* kulingana na mambo yote yenye Yehova alikuwa amemuagiza awaambie.  Hii ilikuwa kisha yeye kumushinda Sihoni+ mufalme wa Waamori, mwenye alikuwa anakaa Heshboni, na Ogu+ mufalme wa Bashani, mwenye alikuwa anakaa Ashtaroti, kule Edrei.+  Katika eneo la Yordani katika inchi ya Moabu, Musa akaanza kufasiria Sheria hii,+ na kusema:  “Yehova Mungu wetu alituambia kule Horebu, ‘Mumekaa wakati murefu sana katika eneo hili lenye milima.+  Mugeuke na kuenda katika eneo lenye milima la Waamori+ na kuelekea majirani wao wote kule Araba,+ eneo la milima, Shefela, Negebu, na eneo la pembeni ya bahari,+ inchi ya Wakanaani, na Lebanoni,*+ mupaka kwenye ule muto mukubwa, muto Efrati.+  Angalia, nimeweka inchi hii mbele yenu. Muingie na kuriti inchi yenye Yehova aliapa kwamba atapatia baba zenu, Abrahamu, Isaka,+ na Yakobo,+ wao pamoja na uzao wao* kisha wao.’+  “Na niliwaambia ninyi wakati huo, ‘Siwezi kuwabeba peke yangu.+ 10  Yehova Mungu wenu amewafanya muongezeke, na ninyi leo muko wengi kama nyota za mbinguni.+ 11  Yehova Mungu wa mababu zenu awafanye muongezeke+ mara elfu moja (1 000) kuliko namna muko sasa, na awabariki kama vile amewaahidi.+ 12  Namna gani mimi peke yangu ninaweza kubeba uzito wenu na mizigo yenu na ugomvi wenu?+ 13  Muchague wanaume wenye hekima, busara, na wenye uzoefu katika makabila yenu, na mimi nitawaweka kuwa vichwa juu yenu.’+ 14  Mukanijibu, ‘Jambo lenye ulituambia tufanye ni la muzuri.’ 15  Kwa hiyo nikachukua vichwa vya makabila yenu, wanaume wenye hekima na uzoefu, na nikawaweka kuwa vichwa juu yenu, wakubwa wa maelfu, wakubwa wa mamia, wakubwa wa makumi tano, wakubwa wa makumi, na maofisa wa makabila yenu.+ 16  “Wakati huo niliwaagiza waamuzi wenu, ‘Wakati munasikia kesi ya hukumu kati ya ndugu zenu, munapaswa kuhukumu kwa haki+ kati ya mutu na ndugu yake ao mukaaji mugeni.+ 17  Hamupaswe kuhukumu kwa upendeleo.+ Munapaswa kusikia mudogo kama vile munasikia mukubwa.+ Musiogopeshwe na wanadamu,+ kwa sababu hukumu ni ya Mungu;+ na kama kesi ya hukumu iko nguvu sana kwenu, muilete kwangu, na nitaisikia.’+ 18  Wakati huo niliwapatia maagizo juu ya mambo yote yenye munapaswa kufanya. 19  “Kisha tukaondoka Horebu na kupita katika lile jangwa lote kubwa na lenye kuogopesha+ lenye muliona katika njia ya kuenda kwenye eneo lenye milima la Waamori,+ kama vile Yehova Mungu wetu alikuwa ametuamuru, na mwishowe tukafika Kadesh-barnea.+ 20  Halafu nikawaambia, ‘Mumefika kwenye eneo lenye milima la Waamori, lenye Yehova Mungu wetu anatupatia. 21  Angalia, Yehova Mungu wako amekupatia inchi hii. Panda, uiriti, kama vile Yehova, Mungu wa mababu zako amekuambia.+ Usiogope wala usikuwe na hofu.’ 22  “Lakini, ninyi wote mulinikaribia na kusema, ‘Tutume wanaume watutangulie ili kupeleleza inchi kwa ajili yetu na watuletee habari kuhusu njia yenye tunapaswa kufuata na ni miji ya namna gani tutakuta.’+ 23  Pendekezo hilo lilionekana kuwa la muzuri kwangu, kwa hiyo nikachagua wanaume kumi na mbili (12) katikati ya wanaume wenu, mwanaume mumoja kwa ajili ya kila kabila.+ 24  Wakaondoka na kupanda kwenye eneo lenye milima,+ na wakafika kwenye Bonde* la Eshkoli na kupeleleza inchi. 25  Wakakamata matunda fulani ya inchi hiyo na kutuletea, na wakatuletea habari hii, ‘Inchi yenye Yehova Mungu wetu anatupatia ni ya muzuri.’+ 26  Lakini mulikataa kupanda, na mukaasi agizo la Yehova Mungu wenu.+ 27  Muliendelea kunungunika katika mahema yenu na mulikuwa munasema, ‘Yehova alituchukia ndiyo sababu alitutosha katika inchi ya Misri ili atutie katika mikono ya Waamori kusudi watumalize. 28  Tunaenda mahali pa namna gani? Ndugu zetu walituvunja moyo*+ kwa kusema, “Watu hao wako na nguvu na ni warefu kuliko sisi, na miji yao ni mikubwa na yenye ngome mupaka mbinguni,*+ na tuliona wana wa Anaki+ kule.”’ 29  “Kwa hiyo nikawaambia, ‘Musikuwe na hofu wala musiogope kwa sababu yao.+ 30  Yehova Mungu wenu atawatangulia na kuwapigania,+ kama vile alifanya kule Misri mbele ya macho yenu wenyewe.+ 31  Na uliona katika jangwa namna Yehova Mungu wako alikubeba kama vile mutu anabeba mwana wake, kila mahali kwenye mulienda mupaka wakati mulifika mahali hapa.’ 32  Lakini ijapokuwa mambo hayo yote, hamukukuwa na imani katika Yehova Mungu wenu,+ 33  mwenye alikuwa anawatangulia katika njia, ili apeleleze mahali kwenye mutapiga kambi. Alitokea kwa moto wakati wa usiku na kwa wingu wakati wa muchana ili awaonyeshe njia yenye munapaswa kufuata.+ 34  “Wakati huo wote Yehova alisikia mambo yenye mulikuwa munasema, na akakasirika na kuapa kwa uzito,+ 35  ‘Hakuna mutu hata mumoja wa kizazi hiki kiovu mwenye ataona inchi ya muzuri yenye niliapa kwamba nitapatia baba zenu,+ 36  isipokuwa Kalebu mwana wa Yefune. Yeye ataiona, na nitamupatia yeye na wana wake inchi hiyo yenye alitembea juu yake, kwa sababu amemufuata Yehova kwa moyo wote.*+ 37  (Yehova alinikasirikia mimi pia kwa sababu yenu, na alisema, “Wewe pia hautaingia ndani.+ 38  Yoshua mwana wa Nuni, mwenye anasimama mbele yako,+ ndiye ataingia katika inchi hiyo.+ Umutie nguvu,*+ kwa maana atafanya Israeli ariti inchi hiyo.”) 39  Zaidi ya hayo, watoto wenu wenye mulisema watakuwa vitu vyenye vinanyanganywa katika vita+ na wana wenu wenye leo hawajue jambo la muzuri ao la mubaya, hao ndio wataingia, na nitawapatia inchi hiyo ili wairiti.+ 40  Lakini ninyi, mugeuke na kuenda katika jangwa kupitia njia ya Bahari Nyekundu.’+ 41  “Basi muliniambia, ‘Tumemutendea Yehova zambi. Sasa tutapanda na kupigana, kama vile Yehova Mungu wetu ametuamuru!’ Kwa hiyo kila mumoja wenu akavaa silaha zake za vita, na mulifikiri itakuwa mwepesi kupanda katika mulima.+ 42  Lakini Yehova akaniambia, ‘Uwaambie: “Musipande na kupigana, kwa sababu sitakuwa pamoja na ninyi.+ Mukienda, mutashindwa na maadui wenu.”’ 43  Kwa hiyo nikaongea na ninyi, lakini hamukusikiliza. Lakini, muliasi agizo la Yehova na mukajaribu kwa kimbelembele kupanda katika mulima. 44  Kisha Waamori wenye walikuwa wanakaa kwenye mulima huo wakatoka ili kukutana na ninyi na wakawakimbiza ninyi kama vile nyuki wanafanya, na wakawasambaza ninyi kuanzia Seiri mupaka Horma. 45  Kwa hiyo mukarudia na kuanza kulia mbele ya Yehova, lakini Yehova hakuwasikiliza wala kuwakazia uangalifu. 46  Ndiyo sababu muliendelea kukaa Kadeshi wakati wote wenye mulikaa kule.

Maelezo ya Chini

Tnn., “wana wa Israeli.”
Inaonekana ni mustari wa milima ya Lebanoni.
Tnn., “mbegu yao.”
Ao “Bonde la Muto.”
Tnn., “walifanya mioyo yetu iyeyuke.”
Ni kusema, yenye kuta za murefu sana.
Tnn., “kwa ukamilifu; kabisa.”
Ao pengine, “Mungu amemutia nguvu.”