Cha Pili cha Wafalme 2:1-25
2 Wakati Yehova alikuwa karibu kumuchukua Eliya+ kuelekea mbinguni* katika zoruba yenye upepo mukali,+ Eliya na Elisha+ wakaondoka Gilgali.+
2 Eliya akamuambia Elisha: “Bakia hapa, tafazali, kwa sababu Yehova amenituma Beteli.” Lakini Elisha akasema: “Kama vile hakika Yehova anaishi na kama vile unaishi,* sitakuacha.” Basi wakashuka kuenda Beteli.+
3 Kisha wana wa manabii* katika Beteli wakakuja kwa Elisha na kumuambia: “Je, unajua kwamba leo Yehova anamuchukua bwana wako asikuwe kiongozi juu yako?”+ Halafu akajibu: “Tayari ninajua. Munyamaze.”
4 Sasa Eliya akamuambia: “Elisha, bakia hapa, tafazali, kwa sababu Yehova amenituma Yeriko.”+ Lakini akasema: “Kama vile hakika Yehova anaishi na kama vile unaishi,* sitakuacha.” Basi wakaenda Yeriko.
5 Kisha wana wa manabii wenye walikuwa Yeriko wakamukaribia Elisha na kumuambia: “Je, unajua kwamba leo Yehova anamuchukua bwana wako asikuwe kiongozi juu yako?” Halafu akasema: “Tayari ninajua. Munyamaze.”
6 Sasa Eliya akamuambia: “Bakia hapa, tafazali, kwa sababu Yehova amenituma Yordani.” Lakini akasema: “Kama vile hakika Yehova anaishi na kama vile unaishi,* sitakuacha.” Basi wote wawili wakaendelea.
7 Na watu makumi tano (50) kati ya wana wa manabii wakaenda pia na wakasimama wakiangalia kwa mbali wakati wote wawili walikuwa wanasimama pembeni ya Yordani.
8 Kisha Eliya akakamata nguo yake ya pekee+ na akaiviringa na kupiga maji, na yakagawanyika kushoto na kuume, na hivyo wote wawili wakavuka upande mwingine kupitia inchi kavu.+
9 Wakati tu walikuwa wamevuka, Eliya akamuambia Elisha: “Omba jambo lenye unataka nikufanyie mbele nichukuliwe kutoka kwako.” Basi Elisha akasema: “Tafazali, ninaweza kupata sehemu mbili za*+ roho yako?”+
10 Akajibu: “Umeomba jambo ngumu. Kama unaniona wakati nitachukuliwa kutoka kwako, itatendeka kwako kwa njia hiyo; lakini kama haunione, jambo hilo halitatendeka.”
11 Wakati walikuwa wanatembea, wakizungumuza wakiwa wanatembea, kwa kushitukia gari la moto na farasi wa moto+ vikawatenganisha hao wawili, na Eliya akapanda kuelekea mbinguni* katika ile zoruba yenye upepo mukali.+
12 Wakati Elisha alikuwa anaangalia, alikuwa anasema kwa sauti kubwa: “Baba yangu, baba yangu! Gari la Israeli na wapanda-farasi wake!”+ Wakati hangeweza tena kumuona, akashika nguo zake mwenyewe na akazipasua vipande mbili.+
13 Kisha akaokota nguo ya pekee+ ya Eliya yenye ilikuwa imemuanguka na akarudia na kusimama pembeni ya Yordani.
14 Kisha akakamata nguo ya pekee ya Eliya yenye ilikuwa imemuanguka na akapiga maji na kusema: “Iko* wapi Yehova, Mungu wa Eliya?” Wakati alipiga maji, yaligawanyika kushoto na kuume, na hivyo Elisha akavuka.+
15 Wakati wana wa manabii wenye walikuwa Yeriko walimuona kwa mbali, wakasema: “Roho ya Eliya imetua juu ya Elisha.”+ Basi wakaenda kukutana naye na wakainama mupaka chini mbele yake.
16 Wakamuambia: “Hapa kuko wanaume makumi tano (50) wenye uwezo pamoja na watumishi wako. Tafazali, uwaache waende kumutafuta bwana wako. Pengine roho ya Yehova imemuinua* na kumutupa juu ya mulima mumoja ao katika bonde moja.”+ Lakini akasema: “Musiwatume.”
17 Hata hivyo, waliendelea kumuomba mupaka akasikia haya, kwa hiyo akasema: “Muwatume.” Wakatuma wale wanaume makumi tano (50), wenye waliendelea kutafuta kwa siku tatu (3) lakini hawakumupata.
18 Wakati walirudia kwake, alikuwa anakaa katika Yeriko.+ Kisha akawaambia: “Je, sikuwaambia musiende?”
19 Kisha wakati fulani watu wa muji huo wakamuambia Elisha: “Bwana wangu anaona namna muji huu uko mahali pazuri;+ lakini maji ni mabaya, na inchi ni tasa.”*
20 Halafu akasema: “Muniletee bakuli la kidogo la mupya na mutie chumvi ndani.” Basi wakamuletea.
21 Kisha akatoka na kuenda kwenye chemchemi ya maji hayo na akatupa chumvi ndani+ na kusema: “Yehova anasema hivi: ‘Nimeponyesha maji haya. Hayatatokeza tena kifo ao utasa.’”*
22 Na maji hayo yameponyeshwa mupaka leo, kulingana na neno lenye Elisha alisema.
23 Akapanda kutoka kule na kuenda Beteli. Wakati alikuwa anatembea katika njia, vijana fulani wadogo walitoka katika muji na wakaanza kumuchekelea,+ na waliendelea kumuambia: “Panda juu, wewe mwenye upara! Panda juu, wewe mwenye upara!”
24 Mwishowe akageuka na kuwaangalia na akawalaani katika jina la Yehova. Kisha dubu-dike wawili+ wakatoka katika pori na kupasua vipande-vipande watoto makumi ine na mbili (42) kati yao.+
25 Kutoka kule akaendelea mupaka Mulima Karmeli,+ na kutoka kule akarudia Samaria.
Maelezo ya Chini
^ Ao “kuelekea katika anga.”
^ Ao “nafsi yako inaishi.”
^ Inaonekana “wana wa manabii” ilikuwa masomo ya kufundisha manabii ao chama fulani cha manabii.
^ Ao “nafsi yako inaishi.”
^ Ao “nafsi yako inaishi.”
^ Ao “mafungu mbili ya.”
^ Ao “kuelekea katika anga.”
^ Ao “Eko.”
^ Ao “upepo wa Yehova umemuinua.”
^ Ao pengine, “inafanya mimba zitoke.”
^ Ao pengine, “kufanya mimba zitoke.”