Mungu Anakuwaka?
Jibu ya Biblia
Ndiyo, mu Biblia muko ushuhuda wenye kuonyesha kabisa kama Mungu anakuwaka. Biblia inatutia moyo tumuamini Mungu. Ile haimaanishe kama tunapaswa tu kuitika-itika mambo yenye makanisa inafundishaka. Lakini tunapaswa kutumia ‘nguvu zetu za kufikiri’ na “uwezo [wetu] wa kufikiri.” (Waroma 12:1; 1 Yohana 5:20, maelezo ya chini) Ona ushuhuda fulani wenye Biblia inatoa:
Ulimwengu wenye kupangwa muzuri na pia bitu yenye iko ndani binaonyesha kama kuko Muumbaji. Biblia inasema hivi: “Kwa kweli, kila nyumba inajengwa na mutu fulani, lakini ule mwenye alijenga bitu yote ni Mungu.” (Waebrania 3:4) Hata kama mawazo ya ile andiko ni ya mwepesi, batu mingi benye elimu banaona kama ni mawazo yenye mutu hawezi kupinga. a
Siye banadamu tunazaliwaka na tamaa ya kutafuta kujua juu ya nini tuko ku dunia. Tunaendeleaka kuwa na ile tamaa hata kisha kutimiza mahitaji yetu ya kimwili. Biblia inaita ile tamaa kuwa ‘uhitaji wa kiroho.’ Ule uhitaji unatia ndani pia kupenda sana kumujua Mungu na kumuabudu. (Matayo 5:3; Ufunuo 4:11) Vile tuko na ile nia, ile inaonyesha kama Mungu iko, na kama iko Muumbaji mwenye upendo na anapenda tutimize ile uhitaji.—Matayo 4:4.
Mu Biblia muko maunabii yenye iliandikiwaka zamani sana na ilifikia kutimia kabisa sawa vile tu Biblia ilikuwaka ilishasema. Juu ile maunabii ilitimia kabisa, ile inaonyesha kama mwenye aliisemaka iko na uwezo sana kupita banadamu.—2 Petro 1:21.
Benye baliandikaka Biblia balijua mambo ya sianse yenye batu benye balikuwa naishi ile wakati habakukuwa najua. Kwa mufano, zamani batu mingi balikuwaka naamini kama dunia inakuwaka njo yulu ya nyama moya hivi, sawa vile tembo, nguruwe ya pori, ao ngombe dume. Lakini, Biblia inasema kama Mungu “ananinginiza dunia mahali kwenye hakuna kitu.” (Yobu 26:7) Vilevile, Biblia inafasiria muzuri umbo ya dunia. Inasema kama dunia iko “muviringo.” (Isaya 40:22) Batu mingi banaona kama inapaswa tu kuwa Mungu njo alisaidia bale benye baliandikaka Biblia baelewe zile habari.
Biblia inajibia maulizo mingi ya nguvu sana, yenye kama haijibiwe muzuri inaweza kufanya mutu asiamini kama Mungu anakuwaka. Kwa mufano: Kama Mungu iko na upendo na iko na nguvu sana, juu ya nini anaacha mateso na mambo ya mubaya iendelee mu dunia? Juu ya nini mara mingi makanisa inachocheaka batu bafanye mambo ya mubaya, kuliko kubachochea bafanye mambo ya muzuri?—Tito 1:16.
a Kwa mufano, Allan Sandage, mwenye alikuwaka najifunza mambo ya astronomia, alisemaka hivi juu ya ulimwengu: “Siamini kabisa kama ulimwengu wenye kupangwa muzuri sana hivi ulijitokeza wenyewe. Kuko tu mutu mwenye aliupanga vile. Miye sijue kama Mungu anakuwaka. Lakini bitu yenye kuwa mu ulimwengu inaonyesha kama kunapaswa kuwa muumbaji.”

