Biblia Inasema Nini Juu ya Kuuawa kwa Mugonjwa Mwenye Kuteseka Sana?
Jibu la Biblia
Biblia haizungumuzie waziwazi kifo cha namna hiyo. * Lakini, mambo yenye inasema juu ya uzima na kifo yanatusaidia tukuwe na mawazo yenye usawaziko. Hakuna mutu mwenye anaruhusiwa kuua mwengine, lakini hakuna sheria hata moja yenye kuonyesha kama tunapaswa kujikaza sana ili kurefusha uzima wa mugonjwa mwenye kukaribia kufa hata wakati hakuna tumaini kuwa atapona.
Biblia inazungumuzia Mungu kuwa Muumbaji wetu, “chemchemi ya uzima.” (Zaburi 36:9; Matendo 17:28) Mungu anaona uzima kuwa wa maana sana. Ndiyo sababu Mungu haruhusu mutu aue mwengine ao ajiue mwenyewe. (Kutoka 20:13; 1 Yohana 3:15) Zaidi ya hilo tunapaswa kukamata mipango yenye usawaziko ili kulinda uzima wetu na uzima wa wengine. (Kumbukumbu la Torati 22:8) Ni wazi kama, Mungu anapenda tuone zawadi ya uzima kuwa ya maana.
Inaomba kufanya nini ikiwa mugonjwa hawezi kupona?
Biblia hairuhusu kuua mutu fulani hata kama mutu huyo anakaribia kufa na hawezi kupona. Mufano wa Mufalme Sauli unaunga mukono jambo hilo. Wakati aliumia sana karibu kufa katika vita, aliomba mutumishi wake amuue. (1 Samweli 31:3, 4) Mutumishi wa Sauli alikataa. Lakini, mwanaume mwengine alifikia kusema kwa uongo kama alitimiza ombi la Sauli. Daudi, mutu mwenye alikuwa na mawazo ya Mungu juu ya jambo hilo, alihukumu mwanaume huyo kifo kwa sababu ya hatia ya damu.—2 Samweli 1:6-16.
Je, tunapaswa kufanya yetu yote ili kurefusha uzima wa mutu?
Wakati inaonekana wazi kama hakuna tumaini la kupona, Biblia haiombe kurefusha uzima wa mutu mwenye kuwa katika hali hiyo. Lakini, Biblia inatusaidia kuwa na mawazo yenye usawaziko. Kifo ni adui wetu mukubwa, matokeo ya hali yetu yenye zambi. (Waroma 5:12; 1 Wakorintho 15:26) Hata kama hatupendi kifo, hatupaswe kukiogopa, kwa sababu Mungu anaahidi kufufua watu wenye wanakufa. (Yohana 6:39, 40) Mutu mwenye anaheshimia uzima atatafuta matunzo ya muzuri zaidi yenye kupatikana. Lakini, kufanya hivyo hakuombe kukamata mipango ya kutunziwa yenye inarefusha uzima wa mutu mwenye hana kabisa tena tumaini la kupona.
Je, kujiua ni zambi yenye haiwezi kusamehewa?
Hapana, Biblia haitie zambi ya kujiua kati ya zambi zenye haziwezi kusamehewa. Hata kama kujiua ni zambi nzito, * Mungu anaelewa muzuri mambo yenye yanaweza kufanya mutu ajiue kama vile magonjwa ya akili, mahangaiko makubwa ya akili, ao hata tabia zenye kutokana na chembe za uriti. (Zaburi 103:13, 14) Kupitia Biblia, Mungu anatoa kitulizo kwa wenye kuwa na mahangaiko. Zaidi ya hilo, Biblia inasema kama kutakuwa “ufufuo wa wenye haki na wenye hawako wenye haki.” (Matendo 24:15) Hilo linaonyesha kama kuko tumaini la ufufuo kwa ajili ya wale wenye walifanya makosa makubwa, kama vile kujiua.
^ Habari hii itazungumuzia kuuawa kwa mutu mwenye kugonjwa sana ao mwenye kuumia sana ili asiendelee kuteseka na maumivu. Katika hali fulani wanganga wanasaidia mugonjwa akufe
^ Mifano kidogo ya watu wenye walijiua yenye kupatikana katika Biblia inahusu wale wenye hawakuwa wanatenda kulingana na mapenzi ya Mungu.—2 Samweli 17:23; 1 Wafalme 16:18; Mathayo 27:3-5.