Ona video zinazopatikana

Biblia Inasema Nini Juu ya Kutosha Mimba?

Biblia Inasema Nini Juu ya Kutosha Mimba?

Jibu ya Biblia

 Mu Biblia hamuna sheria yenye inazungumuzia waziwazi kuhusu “kutosha mimba.” Lakini, mu Biblia muko maandiko yenye inazungumuzia mawazo ya Mungu juu ya uzima wa wanadamu, na hata juu ya mutoto mwenye angali mu tumbo ya mama yake.

 Uzima ni zawadi yenye Mungu ametupatia. (Mwanzo 9:6; Zaburi 36:9) Mungu anaona uzima wote kuwa wa maana, hata uzima wa mutoto mwenye hayazaliwa. Njo maana kama mutu anaua kimakusudi mutoto mwenye hayazaliwa, mbele ya Mungu, ule mutu ni muuaji.

 Sheria yenye Mungu alipatia Waisraeli ilisema hivi: “Kama watu wanapigana na wanamuumiza mwanamuke mwenye mimba naye anazaa mbele ya wakati wake lakini hakutokee kifo, ule mwenye alimuumiza anapaswa kulipa amande yenye bwana ya bibi huyo atamuomba; na anapaswa kulipa amande hiyo kupitia waamuzi. Lakini kama kifo kinatokea, basi unapaswa kutoa uzima kwa uzima.”​—Kutoka 21:22, 23. *

 Uzima wa mwanadamu unaanzaka wakati gani?

 Mungu anaona kama uzima wa mwanadamu unaanza wakati tu mama anabeba mimba. Mu Biblia, anaonyesha mara kwa mara kama mutoto mwenye hayazaliwa, naye ni mutu mwenye iko naishi. Tuone mifano fulani yenye inaonyesha kama Mungu anaona uzima wa mutoto mwenye hayazaliwa na mwenye alishazaliwa kuwa sawasawa.

  •   Kwa muongozo wa roho ya Mungu, Mufalme Daudi aliambia Mungu hivi: “Macho yako hata yaliniona wakati nilikuwa kiini-tete.” (Zaburi 139:16) Hata mbele Daudi azaliwe, Mungu alimuona kuwa mutu mwenye kuishi.

  •   Tena, hata mbele nabii Yeremia azaliwe, Mungu alijua kama atatimiza kazi fulani ya maana. Mungu alimuambia hivi: “Mbele nikuumbe katika tumbo la uzazi nilikujua, na mbele uzaliwe nilikutakasa. Nilikufanya kuwa nabii kwa mataifa.”​—Yeremia 1:5.

  •   Luka, muandikaji fulani wa Biblia mwenye alikuwa munganga, alitumia neno ileile ya Kigiriki ili kuzungumuzia mutoto mwenye hayazaliwa na mwenye alikuwa tayari alishazaliwa.​—Luka 1:41; 2:12, 16.

 Mungu anaweza kusamehe wale wenye walishakatosha mimba?

 Kama sasa wamekubali mawazo ya Mungu juu ya uzima, hawana sababu ya kuendelea kujihukumu. “Yehova ni mwenye rehema na huruma . . . Kama vile mahali jua linatokea kuko mbali sana na mahali jua linashukia, ni vile ametia zambi zetu mbali sana na sisi.” * (Zaburi 103:8-12) Yehova atasamehe wale wenye wanatubu kwa moyo wote zambi zenye walifanyaka zamani, hata zambi ya kutosha mimba.​—Zaburi 86:5.

 Ni mubaya kutosha mimba ikiwa uzima wa mama ao wa mutoto uko mu hatari?

 Kisha kuelewa mambo yenye Biblia inasema juu ya uzima wa mutoto mwenye hayazaliwa, mama hawezi kuwa na sababu ya kutosha mimba juu tu ya hatari fulani ya afya yenye inaweza kumupata yeye ao mutoto.

 Tuseme nini kama wakati wa kuzala kunatokea hali fulani yenye inaomba kuchagua kati ya kuokoa uzima wa mama ao wa mutoto? Mu hali ya vile, bibi na bwana njo wanapaswa kuamua wao wenyewe ikiwa watajaribu kuokoa uzima wa nani.

^ Tafsiri fulani zinafanya ionekane kuwa mu ile sheria, jambo ya maana yenye watu walipaswa kuhangaikia, ni jambo yenye ilipata mama, hapana mutoto mwenye angali mu tumbo. Lakini, maandishi ya Kiebrania inazungumuzia kifo ya mama ao ya mutoto.

^ Biblia inasema kama jina ya Mungu ni Yehova.​—Zaburi 83:18.