Kusamehe Ni Nini?
Jibu ya Biblia
Neno ya Kigiriki yenye kutafsiriwa “kusamehe” inamaanisha “kuacha.” Iko sa vile mutu mwenye halipishe deni. Yesu alitumikisha hii maneno wakati alikuwa nafundisha bafuasi yake vile bangesali: “Utusamehe zambi zetu, kwa maana sisi pia tunasamehe kila mutu mwenye kuwa na deni letu.” (Luka 11:4) Vilevile, mu mufano wa mutumwa mwenye hana huruma, Yesu alilinganisha kusamehe na kuvuta kosa.—Matayo 18:23-35.
Tunaweza kusema kama tunasamehe mutu ni kama tunaacha kujisikia mubaya ku roho juu ya mambo yenye alitufanyia, na hatumuombe afanye jambo fulani juu tumuhurumie. Biblia inafundisha kama upendo yenye haijipendelee njo jambo yenye inasukumaka mutu asamehe bya kweli, juu ‘upendo hauwekake hesabu ya ubaya.’—1 Wakorinto 13:4, 5.
Mambo yenye kusamehe haimaanishe
Haimaanishe kuachilia tu kosa. Biblia inahukumu bote benye banasema kama matendo ya mubaya haina shida ao kama inaitikiwa.—Isaya 5:20.
Haimaanishe kufanya sa vile hakuna kosa yenye ilifanyika. Mungu alisameheaka zambi nzito ya Mufalme Daudi, lakini hakumulindaka juu asipate matokeo ya matendo yake. Kama Mungu aliacha zile zambi za Daudi ziandikiwe ni juu tuzikumbuke leo.—2 Samweli 12:9-13.
Haimaanishe kuacha bengine bakuonee. Kwa mufano unakopesha mutu makuta, lakini anaitumikisha mubaya na anashindwa kukulipa vile mulisikilizana. Anahuzunika sana na anakuomba musamaha. Unaweza kuchagula kumusamehe. Na kama ni vile, hautaweka tena ile mambo ku roho, hautaendelea kumukumbusha ayo, na kama inawezekana pengine utavuta tu ile deni. Hata vile, unaweza kusema kama hautamukopeshaka tena makuta.—Zaburi 37:21; Mezali 14:15; 22:3; Wagalatia 6:7.
Haimaanishe kusamehe bila musingi yoyote. Mungu hasamehe batu benye banafanyaka mambo ya mubaya kwa kupenda na banakatala kutubu na kuomba musamaha ku bale benye balikosea. (Mezali 28:13; Matendo 26:20; Waebrania 10:26) Bale benye habatubu banakuwa maadui ya Mungu, na yeye hatuombe tusamehe benye hayasamehe.—Zaburi 139:21, 22.
Sasa, utafanya nini kama mutu anakutendea mubaya sana na anakatala kuomba musamaha ao kuitika byenye alifanya? Shauri ya Biblia inasema hivi: “Acha hasira na uache kasirani kali.” (Zaburi 37:8) Hata kama haufurahie mambo yenye balikufanyia, ile haimaanishe kama unapaswa kubakia na kasirani. Ukuwe hakika kama Mungu atamalizana na ule mutu. (Waebrania 10:30, 31) Kujua kama wakati yenye kuya Mungu atamaliza mambo yote yenye kutuletea maumivu na yenye kutuhangaisha inaweza pia kukusaidia utulie.—Isaya 65:17; Ufunuo 21:4.
Haimaanishe “kusamehe” kila kosa ya kidogo yenye tunawaza kama balitukosea. Wakati fulani, kuliko kusema kama tunasamehe mutu mwenye shiye tu njo tunawaza kama alitukosea, ni muzuri kuitika kama hatuna sababu ya kusirika. Biblia inasema hivi: “Usikuwe haraka kukasirika, kwa maana kukasirika ni tabia ya mupumbavu.”—Muhubiri 7:9, maelezo ya chini.
Gisi ya kusamehe mutu
Kumbuka maana ya kusamehe. Wakati unasamehe mutu haimaanishe kama unaona mambo yenye alikufanyia iko tu sawa, ao kufanya sa vile hakuna kosa yenye ilifanyika. Wakati unasamehe mutu unachagula tu kuachilia makosa yenye alikufanyia.
Ukumbuke faida ya kusamehe. Kuacha kasirani na mambo yenye unaweka mu roho, inaweza kukusaidia utulie, ukuwe na afya ya muzuri, ukuwe na furaha sana. (Mezali 14:30; Matayo 5:9) Zaidi ya ile, kama unakuwaka nasamehe bengine njo Mungu atakusamehe na weye.—Matayo 6:14, 15.
Ujitie pa nafasi ya bengine. Siye bote hatukamilike. (Yakobo 3:2) Vile tu tunapendaka batusamehe, njo vile tupaswa kusamehe makosa ya bengine.—Matayo 7:12.
Ukuwe mwenye usawaziko. Wakati mutu anatufanyia kosa yenye haiko kubwa, tunapaswa kufuata hii shauri ya Biblia: “Muendelee kuvumiliana.”—Wakolosai 3:13.
Fanya mbio. Ujikaze kusamehe mbiombio kuliko kuacha kasirani iongezeke.—Waefeso 4:26, 27.

