Dini Zote Ni Zimoya? Zote Zinapelekaka kwa Mungu?

Dini Zote Ni Zimoya? Zote Zinapelekaka kwa Mungu?

Jibu ya Biblia

 Hapana, dini zote haiko zimoya. Mu Biblia muko mifano mingi ya dini zenye zinachukiza Mungu. Zile dini zinaweza kuwekwa mu bikundi mbili.

Kikundi kya 1: Benye banaabudu miungu ya bongo

 Biblia inasema kama kuabudu miungu ya bongo ni “udanganyifu,” “mambo ya bure,” na “bitu byenye habina mafaa.” (Yeremia 10:3-5; 16:19, 20) Yehova a Mungu aliambia taifa yake ya Israeli hivi: “Haupaswe kuwa na miungu ingine isipokuwa miye.” (Kutoka 20:3, 23; 23:24) Wakati Baisraeli baliabudu ingine miungu, ‘Yehova alikasirika.’​​—Hesabu 25:3; Walawi 20:2; Waamuzi 2:13, 14.

 Mungu angali najisikia vile wakati batu banaabudu “bale benye banaitwa miungu.” (1 Wakorinto 8:5, 6; Wagalatia 4:8) Mungu anaambia bale benye banataka kumuabudu baache kushirikiana na benye biko mu dini za bongo. Anasema hivi: “Mutoke katikati yabo na mujitenge.” (2 Wakorinto 6:14-​17) Sasa, kama dini zote ni zimoya na kama zote zinapelekaka batu kwa Mungu, juu ya nini Mungu anatoaka ile amri?

Kikundi kya 2: Benye banaabudu Mungu wa kweli, lakini mu njia yenye hapendi

 Wakati fulani, Baisraeli baliabudu Mungu mu kutumia imani na desturi yenye balitosha mu ibada za miungu ya bongo, lakini Yehova alikatala kabisa ile tendo ya kuchanga dini ya kweli na ya bongo. (Kutoka 32:8; Kumbukumbu la Torati 12:2-4) Yesu alihukumu biongozi ya dini ba wakati yake juu ya njia yenye balikuwa natumia kumuabudu Mungu; kwa inje balikuwa naonekana sawa vile ni batakatifu, lakini kwa unafiki balikuwa “napuuza mambo mazito zaidi ya Sheria, ni kusema, haki, rehema, na uaminifu.”​​—Matayo 23:23.

 Vile vile leo, dini yenye inategemea kweli njo yenye inapeleka batu kwa Mungu. Ile kweli inapatikana mu Biblia. (Yohana 4:24; 17:17; 2 Timoteo 3:16, 17) Dini zenye mafundisho yake inapingana na Biblia ziko napeleka batu mbali na Mungu. Batu banawazaka kama mafundisho ya mingi ya zile dini​​—sawa vile fundisho ya Utatu, kutokufa kwa nafsi, na moto wa mateso​​—zinatoka mu Biblia. Lakini haiko vile. Ile mafundisho inatoka mu ibada ya bale benye balikuwa naabudu miungu ya bongo. Ibada yenye inachochea ile mafundisho ni ya “bure,” ao haina maana, juu inafanyaka desturi za dini zikamate nafasi ya sheria ya Mungu.​​—Marko 7:7, 8.

 Mungu anachukia bunafiki ya madini ya bongo. (Tito 1:16) Dini ya kweli inapaswa kusaidia batu bamukaribie Mungu, kuliko tu kubafundisha bafwate desturi fulani. Kwa mufano, Biblia inasema: “Kama mutu yeyote anawaza yeye ni mutu wa dini lakini hazuie kabisa ulimi yake, anadanganya moyo wake mwenyewe, na ibada yake ni ya bure. Dini yenye kuwa safi na yenye haina buchafu kwa maoni ya Mungu wetu na Baba ni hii: kuhangaikia mayatima na bajane katika taabu yabo, na kuendelea kubakia bila doa kutokana na ulimwengu.” (Yakobo 1:26, 27; maelezo ya chini).

a Biblia inasema kama jina ya Mungu wa kweli ni Yehova.