Juu ya nini banamuitaka Yesu asema ni Mutoto wa Mungu?
Jibu ya Bible
Mala ya mingi Bible inamuitaka Yesu asema “Mutoto wa Mungu.” (Yohana 1:49) Iyi terme “Mutoto wa Mungu” inaonesha tu peupe asema Mungu njo Muumbaji, ni kwake njo kunatokaka bujima bote, kuwekamo na bwa Yesu. (Zaburi 36:9; Ufunuo 4:11) Bible aifundishe asema Mungu arizalaka mutoto sa vile tu bantu banazalaka batoto.
Bible inaita tena bamalaika “batoto yake ya Mungu wa bya kweri.” (Yobu 1:6) Tena Bible inasema asema muntu wa kwanza, Adam, arikuyaka “mutoto yake ya Mungu” (Luka 3:38) Lakini, nju Yesu njo malaika wa kwanza ule Mungu ariumbaka, na ule ariumbaka ye moya, Bible inamusemea sa vile Mutoto wa sana wa Mungu.
Eske Yesu ariishi ku mbingu mbele ya ye kuya pa dunia?
Ndiyo, njo vile. Yesu arikuyaka kiumbe wa kiroo (ao esprit) mbele bamuzale sa muntu apa pa dunia. Yesu ye moya arisemaka ivi: “Miritoka ku mbingu.”—Yohana 6:38; 8:23.
Mungu arimuumbaka Yesu mbele aumbe kintu kingine kyokyote. Bible inasema ivi nju ya Yesu:
“Ye ni . . . kiumbe kya kwanza mu biumbe byote.”—Wakolosai 1:15.
Ye njo “mwanzo ya uumbaji ya Mungu.”—Ufunuo 3:14.
Iyi profesi irifanshikaka pa Yesu: “Ule mwanzo yake irianzaka nzamani, kuanzia mu mashiku ya nzamani sana.”—Mika 5:2; Matayo 2:4-6.
Yesu arianzaka kufanya nini ku mbingu mbele ya ye kuya apa pa dunia?
Arikuya mu pozision ya yulu sana kule ku mbingu. Tunayuwa vile nju Yesu arisemaka ivi saa arianzaka kuomba: “Baba, unitukuze . . . na utukufu ile mirikuyaka nayo ku mpembeni yako mbele dunia ikuyeko.”—Yohana 17:5.
Arisaidia Baba yake mu kaji ya kuumba bintu bingine byote. Yesu aritumikia ku mpembeni ya Baba yake sa vile “muntu wa kaji wa akiri.” (Mezali 8:30) Bible inasema ivi nju ya Yesu: “Kupitia yeye njo bariumba bintu bingine byote ku mbingu na pa dunia.”—Wakolosai 1:16.
Mungu arimutumikisha Yesu nju ya kuumba bintu byote. Kuwekamo bamalaika na bintu bingine bile tunaonaka. (Ufunuo 5:11) Mu maana ingine, irikuwa sa vile Mungu njo arikuwa ingenieur architecte, na Yesu njo arikuwa sa vile maçon. Architecte ye anafanyaka dessin ya vile nyumba ao batiman fulani itakuyaka; maçon ye sasa anabebaka ile dessin na kushimamisha sasa nyumba ao batiman.
Arikuwa Sauti ao Neno. Wakati ile Bible inasemea maisha ya Yesu ya ku mbingu, inasemaka asema arikuyaka “Sauti.” (Yohana 1:1) Ni kusema, Mungu arianzaka kutumikisha Mutoto yake nju ya kupelekea miyumbi biumbe bingine bya kiroo na nju ya kubaambia bya kufanya.
Tena, Yesu arianzaka kutumika sa vile porte-parole wa Mungu ku bantu ba pa dunia. Pengine Mungu arimutumikishaka Yesu, Sauti, nju ya kuambia Adam na Eve bile barishapashwa kufanya. (Mwanzo 2:16, 17) Pengine Yesu njo arikuyaka malaika ule arianzaka kuongoza batoto ba Israel mu dezer na ule baripashwa kufuata sauti yake.—Kutoka 23:20-23. a
a Mungu ashikutumikishake paka malaika, ule Bible inaita Sauti, nju ya kusumburia na bantu. Kwa mufano, aritumikishaka na bamalaika bengine nju ya kupeleka Sheria ku batoto ba Israel, apana tu paka Mutoto yake wa kwanza.—Matendo 7:53; Wagalatia 3:19; Waebrania 2:2, 3.

