Hamia kwenye habari

Kwa Nini Mashahidi wa Yehova Wanawatembelea Watu Nyumba kwa Nyumba?

Kwa Nini Mashahidi wa Yehova Wanawatembelea Watu Nyumba kwa Nyumba?

 Yesu aliwaambia wafuasi wake ‘wafanye wanafunzi kutoka kwa watu wa mataifa yote.’ (Mathayo 28:19, 20) Alipowatuma wanafunzi wake wa karne ya kwanza, Yesu aliwaagiza waende nyumbani kwa watu. (Mathayo 10:7, 11-13) Baada ya kifo cha Yesu, Wakristo wa karne ya kwanza waliendelea kueneza ujumbe wao “hadharani na nyumba kwa nyumba.” (Matendo 5:42; 20:20) Tunafuata mfano wa Wakristo hao wa karne ya kwanza na tumeona kwamba kuhubiri nyumba kwa nyumba ni njia nzuri ya kuwafikia watu.