‘MWIMBIENI YEHOVA KWA SHANGWE’

Sala ya Shukrani (Wimbo

Na. 43)

Kiswahili
Sala ya Shukrani (WimboNa. 43)
/assets/ct/28ada02fb0/images/syn_placeholder_sqr.png
sjj wimbo na. 43

WIMBO NA. 43

Sala ya Shukrani

Sala ya Shukrani

(Zaburi 95:2)

  1. 1. Yehova Mungu tunakushukuru,

    Twaja kwako kupitia sala,

    Nasi tunainama mbele zako,

    Twajiweka mikononi mwako.

    Sisi ni watenda dhambi, wanyonge;

    Tunakuomba utusamehe.

    Kwa damu ya Mwanao tusafishe,

    Wajua umbo letu vizuri.

  2. 2. Twakushukuru kwa fadhili zako,

    Asante kwa kutuvuta kwako.

    Utufundishe kukujua wewe,

    Twataka tuwe waaminifu.

    Una nguvu zisizo na kifani,

    Asante kwa kutujasirisha.

    Tusonge mbele kwa unyenyekevu;

    Ee Yehova wastahili sifa!