Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

Habari Kuu | UNAWEZA KUIELEWA BIBLIA

Kwa Nini Uielewe Biblia?

Kwa Nini Uielewe Biblia?

“Biblia ni kitabu cha dini kinachojulikana sana. Hata hivyo, ni kitabu cha kigeni na hakiwafai Wachina.”—LIN, CHINA.

“Hata vitabu vitakatifu vya dini yangu ya Kihindu sivielewi. Nitawezaje kuielewa Biblia Takatifu?” —AMIT, INDIA.

“Ninaiheshimu Biblia kwa kuwa ni kitabu cha zamani na nimesikia kwamba kimeuzwa zaidi kuliko vitabu vingine. Lakini, sijawahi kuiona.”—YUMIKO, JAPANI.

Watu wengi ulimwenguni wanaiheshimu sana Biblia. Hata hivyo, wengi wao hawajui yaliyomo katika Biblia. Hali iko hivyo kwa mamilioni ya watu wanaoishi barani Asia na hata katika nchi nyingi ambazo watu wengi wana Biblia.

Huenda ukajiuliza hivi, ‘Kwa nini ninahitaji kuielewa Biblia?’ Kujifunza kuhusu kitabu hicho kitakatifu kunaweza kukusaidia:

  • Uridhike na uwe na furaha

  • Ushughulikie matatizo ya familia

  • Ukabiliane na mahangaiko

  • Uwe na uhusiano mzuri na watu

  • Utumie pesa kwa hekima

Mfikirie Yoshiko, anayeishi Japani. Alitaka sana kujua Biblia ina ujumbe gani, hivyo akaanza kuisoma. Matokeo yalikuwa nini? Anasema hivi: “Biblia imenisaidia kupata kusudi maishani na tumaini la wakati ujao. Sasa nimeridhika.” Amit aliyetajwa mwanzoni aliamua pia kuichunguza Biblia. Anasema: “Nilishangaa. Biblia ina habari zinazomfaa kila mtu.”

Biblia imeboresha sana maisha ya watu wengi. Kwa nini usiichunguze uone jinsi inavyoweza kukunufaisha?