Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

Tosheleza Uhitaji Wako wa Kiroho

Tosheleza Uhitaji Wako wa Kiroho

Njia ya 5

Tosheleza Uhitaji Wako wa Kiroho

BIBLIA INAFUNDISHA NINI? “Wenye furaha ni wale wanaotambua uhitaji wao wa kiroho.”—Mathayo 5:3.

KWA NINI INAWEZA KUWA VIGUMU? Kuna maelfu ya dini tofauti-tofauti, na nyingi ya dini hizo zinafundisha njia zinazopingana za kutosheleza uhitaji wako wa kiroho. Unaweza kujua jinsi gani dini inayofundisha ukweli na inayompendeza Mungu kikweli? Baadhi ya waandishi maarufu wa vitabu wanadai kuwa kumwamini Mungu na kujitoa kwake ni jambo lisilopatana na akili na lina madhara. Gazeti Maclean’s linaeleza kifupi maoni ya mtu mmoja maarufu asiyeamini kuwa kuna Mungu, likisema hivi: “Fundisho la Wakristo kwamba kuna jambo fulani tusiloweza kuthibitisha kisayansi wala kulitambua kupitia hisi zetu . . . linafanya maisha haya yaonekane kuwa yasiyo na thamani na kutufanya tuwe na mwelekeo wa kusababisha vurugu.”

UNAWEZA KUFANYA NINI? Chunguza mambo yanayothibitisha kwamba kuna Mungu. (Waroma 1:20; Waebrania 3:4) Usimruhusu yeyote akuvunje moyo ili usitafute majibu ya maswali muhimu, kama vile, Kwa nini tupo hapa? Je, kuna uhai baada ya kifo? Kwa nini tunateseka sana? Mungu anataka nifanye nini? Kupata majibu yenye kuridhisha kwa maswali hayo ni muhimu ili upate uradhi wa kudumu.

Hata hivyo, usikubali tu kila kitu unachoambiwa bila kufikiri. Neno la Mungu linakutia moyo utumie ‘nguvu zako za kufikiri’ ili ujihakikishie lile linalokubalika kwake. (Waroma 12:1, 2) Ukifanya hivyo utabarikiwa sana. Ikiwa unatenga wakati ili kujifunza Biblia na kutumia mashauri yake, utaepuka matatizo, kupunguza mahangaiko, na kuongeza furaha yako maishani. Hiyo ni ahadi ya kweli. Mamilioni ya watu wa malezi mbalimbali wamefaidika kwa kujifunza kweli kumhusu Mungu na makusudi yake. Kwa mfano, soma masimulizi halisi ya maisha katika ukurasa wa 18 mpaka 21 wa gazeti hili.

Unapoendelea kunufaika kwa kutumia mashauri ya Biblia yenye hekima, ujitoaji wako kwa Mungu unaimarika zaidi. Tunakutia moyo ukubali mwaliko wa kujifunza Biblia pamoja na Mashahidi wa Yehova. Ukifanya hivyo, yaelekea utakubaliana na mtume Paulo, aliyeandika: “Huo ni njia ya kupata faida kubwa, huu ujitoaji-kimungu pamoja na ujitoshelevu [au, uradhi].”—1 Timotheo 6:6.

[Picha katika ukurasa wa 8]

Jihakikishie lile linalokubalika kwa Mungu