Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

Je, Ni Lazima Uamini Utatu ili Uwe Mkristo?

Je, Ni Lazima Uamini Utatu ili Uwe Mkristo?

Wasomaji Wetu Wanauliza . . .

Je, Ni Lazima Uamini Utatu ili Uwe Mkristo?

▪ Kitabu kimoja cha shule za sekondari (World Religions in Denmark), kilichochapishwa mwaka wa 2007, kilisema kwamba Mashahidi wa Yehova ni dini ndogo ya Kikristo inayofuata Biblia kwa makini. Kwa kweli, Mashahidi wa Yehova ndiyo dini ya tatu kwa ukubwa kati ya dini zote za Kikristo nchini Denmark.

Hata hivyo, askofu wa Kanisa la Kitaifa la Denmark alimshutumu vikali mwandishi wa kitabu hicho kwa kuwataja Mashahidi katika kitabu hicho. Kwa nini? Askofu huyo alisema hivi: “Bado sijawahi kukutana na mwanatheolojia yeyote ambaye anawaona [Mashahidi wa Yehova] kuwa Wakristo. Wanakataa Utatu, ambao ndio msingi wa dini ya Kikristo.”

Annika Hvithamar, mwandishi wa kitabu hicho, ambaye ni mwanasosholojia wa dini, alisema kwamba watu wanapoulizwa kwa nini wanajiona kuwa Wakristo, hawasemi kamwe kwamba ni kwa sababu wanaamini Mungu ni Utatu. Zaidi ya hilo, sehemu ya kitabu hicho yenye kichwa “Je, Wewe Ni Mkristo?” inasema: “Fundisho la Utatu ni moja kati ya matatizo makubwa zaidi katika mafundisho ya dini ya Kikristo.” Inaongezea hivi: “Sikuzote, imekuwa vigumu kuwaeleza Wakristo wasio na elimu kwa nini Mungu wa Wakristo ni mungu mmoja bali si miungu watatu.”

Biblia ina mafundisho rahisi na yaliyo wazi kumhusu Mungu na Yesu. Yanaeleweka kwa urahisi. Neno “Utatu” halipatikani katika Neno la Mungu wala wazo hilo. Biblia inasema waziwazi kwamba Yesu Kristo ni Mwana mzaliwa wa kwanza wa Mungu. (Wakolosai 1:15) Pia, inasema kwamba Yesu ni ‘mpatanishi kati ya Mungu na wanadamu.’ (1 Timotheo 2:5) Biblia inasema hivi kumhusu Baba: “Wewe, ambaye jina lako ni Yehova, wewe peke yako ndiye Uliye Juu Zaidi, juu ya dunia yote.”—Zaburi 83:18.

Mashahidi wa Yehova wanaamini kwamba ni jambo la maana sana kumwamini Yesu. (Yohana 3:16) Kwa hiyo, wanachukua kwa uzito amri hii ya Yesu: “Imeandikwa, ‘Yehova Mungu wako ndiye unayepaswa kumwabudu, na yeye peke yake ndiye unayepaswa kumtolea utumishi mtakatifu.’” (Mathayo 4:10) Bila shaka, mtu anayejitahidi kutii amri za Yesu anaweza kuitwa Mkristo.

[Blabu katika ukurasa wa 22]

“Fundisho la Utatu ni moja kati ya matatizo makubwa zaidi katika mafundisho ya dini ya Kikristo”