Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

Jinsi Paradiso Ilivyopotea

Jinsi Paradiso Ilivyopotea

Kwa Ajili ya Vijana Wetu

Jinsi Paradiso Ilivyopotea

Maagizo: Fanya zoezi hili katika mazingira matulivu. Unaposoma maandiko, jiwazie ukiwa katika tukio linalozungumziwa. Wazia kikao. Sikia sauti. Hisi kama watu wanaozungumziwa katika tukio hilo. Wazia kwamba masimulizi haya ni halisi kabisa.

CHUNGUZA TUKIO HILI.— SOMA MWANZO 3:1-24.

Unafikiri Hawa alitenda jinsi gani mwanzoni wakati nyoka alipoanza kuzungumza naye?

․․․․․

Ukikumbuka kwamba Adamu na Hawa walitenda dhambi kimakusudi, unafikiri walihisi namna gani kama inavyoripotiwa katika mstari wa 7-10?

․․․․․

Unawazia Adamu na Hawa walifukuzwa jinsi gani kutoka katika bustani ya Edeni, kama inavyoelezwa katika mstari wa 22-24?

․․․․․

CHIMBA ZAIDI.

Macho ya Hawa yalimwongoza jinsi gani kuanguka katika dhambi? (Soma tena mstari wa 6.)

․․․․․

Kwa nini Hawa aliona lile tunda kuwa “kitu cha kutamanika”? (Soma tena mstari wa 4 na wa 5.)

․․․․․

Huenda ni nini kilichomsukuma Adamu kujiunga na Hawa katika dhambi yake? (Soma tena mstari wa 6.)

․․․․․

Dhambi ingekuwa na matokeo gani mabaya kwa uhusiano kati ya wanaume na wanawake katika vizazi ambavyo vingefuata? (Soma tena mstari wa 16.)

․․․․․

Ni nini kinachoonyesha kwamba uhusiano kati ya Adamu na Hawa ulikuwa umeharibika kwa sababu ya dhambi? (Soma tena mstari wa 12.)

․․․․․

Yehova alishughulikia haraka jinsi gani tatizo hilo ili kusudi lake lifanikiwe? (Soma tena mstari wa 15.)

․․․․․

TUMIA MAMBO ULIYOJIFUNZA. ANDIKA MAMBO ULIYOJIFUNZA KUHUSU . . .

Hatari za roho ya kujitegemea.

․․․․․

Jinsi macho yanavyoweza kuchochea tamaa mbaya.

․․․․․

Kwa nini si vizuri kuwalaumu wengine kwa sababu ya makosa yetu.

․․․․․

NI MAMBO GANI KATIKA SIMULIZI HILI AMBAYO YAMEKUGUSA MOYO SANA, NA KWA NINI?

․․․․․