Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

Maswali Kutoka kwa Wasomaji

Maswali Kutoka kwa Wasomaji

Maswali Kutoka kwa Wasomaji

Andiko la Kumbukumbu la Torati 14:21 linasema: “Msile mwili wowote uliokufa tayari.” Je, maneno hayo yanapingana na andiko la Mambo ya Walawi 11:40, linalosema: “Anayekula sehemu yoyote ya mzoga wake atayafua mavazi yake, naye atakuwa asiye safi mpaka jioni”?

Mistari hiyo miwili haipingani. Andiko la Kumbukumbu la Torati 14:21 linarudia sheria iliyokataza kula mnyama aliyepatikana akiwa amekufa, labda baada ya kuuawa na wanyama-mwitu. (Kutoka 22:31; Mambo ya Walawi 22:8) Andiko la Mambo ya Walawi 11:40 linaeleza yale ambayo Mwisraeli angeweza kufanya alipovunja sheria hiyo, labda bila kukusudia.

Sheria ilipokataza jambo fulani, hilo halikumaanisha kwamba haingevunjwa wakati fulani. Kwa mfano, kulikuwa na sheria zilizokataza wizi, uuaji, kutoa ushahidi wa uwongo, na kadhalika. Wakati huohuo, kulikuwa na adhabu fulani zilizotolewa kwa kuvunja sheria hizo zilizotoka kwa Mungu. Adhabu hizo zilionyesha uzito wa sheria hizo.

Mtu aliyevunja sheria iliyokataza kula mwili wa mnyama aliyepatikana akiwa amekufa angekuwa asiye safi mbele za Yehova na ingembidi afuate utaratibu unaofaa ili awe safi. Iwapo hangejisafisha kwa njia inayofaa, ‘angejibu kwa kosa lake.’—Mambo ya Walawi 17:15, 16.