Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

Je, Unakumbuka?

Je, Unakumbuka?

Je, Unakumbuka?

Je, umefurahia kusoma matoleo ya hivi karibuni ya Mnara wa Mlinzi? Ona kama unaweza kujibu maswali yafuatayo:

Ni kwa sababu gani Desemba 25 ilichaguliwa kuwa tarehe ya kuzaliwa kwa Yesu?

Neno la Mungu halionyeshi tarehe ya kuzaliwa kwa Yesu. Kichapo Enciclopedia Hispánica kinasema hivi: “Tarehe 25 Desemba haikuchaguliwa kuwa siku ya kuadhimisha Krismasi kwa sababu ilikuwa tarehe sahihi ya siku aliyozaliwa Yesu, bali ilichaguliwa ili kufanya sherehe zilizoadhimishwa huko Roma wakati wa majira ya baridi ziwe za Kikristo.” Waroma wa kale waliadhimisha kuchomoza kwa jua wakati wa majira ya baridi kali kwa kula na kunywa, kufanya karamu za kupindukia, na kupeana zawadi.—12/15, ukurasa wa 4-5.

• Je, andiko la Matendo 7:59 linamaanisha kwamba Stefano alisali kwa Yesu?

La. Biblia inaonyesha kwamba sala inapaswa kuelekezwa kwa Yehova Mungu peke yake. Lakini Stefano alipomwona Yesu aliyefufuliwa katika maono, yaelekea alijihisi huru kumsihi moja kwa moja, akisema: “Bwana Yesu, pokea roho yangu.” Stefano alijua kwamba Yesu alikuwa amepewa mamlaka ya kuwafufua wafu. (Yohana 5:27-29) Hivyo, Stefano akamwomba Yesu ahifadhi roho yake hadi siku ya ufufuo.—1/1, ukurasa wa 31.

• Tunajuaje kwamba mtu hapangiwi mapema mambo yatakayompata?

Mungu amempa mwanadamu uhuru wa kuchagua ambao hupingana na wazo la kwamba watu hupangiwa mambo mapema. Ingekuwa kukosa upendo na haki iwapo kabla hatujazaliwa Yehova angepanga mapema jinsi maisha yetu yatakavyokuwa kisha atutoze hesabu kwa matendo yetu. (Kumbukumbu la Torati 32:4; 1 Yohana 4:8)—1/15, ukurasa wa 4-5.

• Kwa nini ingekuwa kukosa kiasi kusema kwamba miujiza haiwezi kutukia kamwe?

Kwa kuwa wanatambua kwamba hawana ujuzi kamili wa mambo ya kisayansi yenye kustaajabisha yanayoonekana katika uumbaji wa Mungu, wanasayansi fulani wanakiri kuwa hawawezi kusema kwa uhakika kwamba jambo fulani haliwezi kutukia kamwe. Wanaweza tu kusema kwamba huenda lisitukie.—2/15, ukurasa wa 5-6.

• Kwa nini Mwamuzi Samsoni aliwaambia wazazi wake kwamba alitaka kuoa mwanamke Mfilisti? (Waamuzi 14:2)

Ilikuwa kinyume cha sheria ya Mungu kufunga ndoa na mwabudu wa uwongo. (Kutoka 34:11-16) Hata hivyo, mwanamke huyo Mfilisti ‘alistahili kabisa’ machoni pa Samsoni. Samsoni “alikuwa akitafuta nafasi ya kuwapiga Wafilisti,” na mwanamke huyo ndiye aliyestahili kwa lengo hilo. Mungu alimtegemeza Samsoni kupitia roho Yake. (Waamuzi 13:25; 14:3, 4, 6)—3/15, ukurasa wa 26.

• Je, Mkristo anaweza kumpa mfanyakazi wa serikali bakshishi au zawadi fulani kwa huduma yake?

Ni kosa kutoa rushwa kwa mfanyakazi wa serikali, kumpa kitu fulani chenye thamani ili afanye jambo linalokiuka sheria, kupotosha haki, au kukufanyia hisani. Lakini kumpa mtumishi wa umma zawadi au bakshishi kwa kazi yake au ili akuhudumie kwa njia halali au ili uepuke kuhangaishwa, si kutoa rushwa.—4/1, ukurasa wa 29.