Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

Mungu ambaye ni “Msikiaji wa sala,” anapenda kutusikiliza tunaposali kwake.​—ZABURI 65:2

Endelea Kusali Ili Upate Kibali cha Mungu

Endelea Kusali Ili Upate Kibali cha Mungu

Mungu amewapa wanadamu zawadi ya pekee, yaani, uwezo wa kuwasiliana naye na kueleza hisia zao kupitia sala. Nabii Daudi alisali hivi: “Ee Msikiaji wa sala, watu wa kila aina watakujia.” (Zaburi 65:2) Lakini tunapaswa kusali kwa njia gani ili Mungu atusikilize na kutubariki?

SALI KUTOKA MOYONI NA KWA UNYENYEKEVU

Sala zako za kibinafsi zitakuwezesha kumwaga moyo wako mbele za Mungu, na kumweleza hisia zako za ndani. (Zaburi 62:8) Mwenyezi Mungu anapenda tusali kwa unyofu kutoka moyoni.

TUMIA JINA LA MUNGU UNAPOSALI

Ingawa Mungu ana majina mengi ya cheo kama vile Bwana au Mwenyezi Mungu, lakini ana jina moja tu la kibinafsi. “Mimi ni Yehova. Hilo ndilo jina langu.” (Isaya 42:8) Jina Yehova linapatikana mara 7,000 hivi katika Maandiko Matakatifu. Manabii wengi walitumia jina la Mungu walipokuwa wakisali. Abrahamu alisema hivi: “Tafadhali Yehova, . . . niruhusu niendelee kuongea [nawe].” (Mwanzo 18:30) Sisi pia tunapaswa kutumia jina la Mungu, Yehova, tunaposali.

SALI KWA LUGHA YAKO

Mungu anaelewa mawazo na hisia zetu tunapozungumza kwa lugha yoyote ile. Neno Lake linatuhakikishia hivi: “Mungu hana ubaguzi, lakini katika kila taifa mtu anayemwogopa na kutenda uadilifu anakubaliwa naye.”​—Matendo 10:34, 35.

Hata hivyo, ili tupate baraka za Mungu, tunahitaji kufanya mambo mengine zaidi ya kusali. Katika makala zinazofuata tutachunguza mambo tunayopaswa kufanya.