Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

Biblia Inasema Nini?

Biblia Inasema Nini?

Je, haki ya kweli itapatikana duniani?

Ungejibuje?

  • Ndiyo

  • Hapana

  • Labda

Biblia inasema hivi

“Najua vema kwamba Yehova atatimiza dai halali la mwenye kuteseka, hukumu ya maskini.” (Zaburi 140:12) Ufalme wa Mungu utaleta haki ya kweli duniani.

Mambo mengine tunayojifunza katika Biblia

  • Mungu anaona ukosefu wa haki unaoendelea sasa, naye ataukomesha.—Mhubiri 5:8.

  • Haki ambayo Mungu ataleta, itaifanya dunia iwe na amani na usalama.—Isaya 32:16-18.

Je, Mungu anapendelea jamii moja ya watu kuliko nyingine?

Baadhi ya watu wanaamini kwamba Mungu amezibariki au kulaani jamii fulani hususa za watu, ilhali wengine wanaamini kwamba Mungu anawatendea watu wote kwa usawa. Wewe una maoni gani?

Biblia inasema

“Mungu hana ubaguzi, bali katika kila taifa mtu ambaye anamwogopa na kutenda uadilifu anakubalika kwake.” (Matendo 10:34, 35) Kwa maoni ya Mungu, watu wote ni sawa.

Ni nini kingine tunachojifunza katika Biblia?

  • Biblia ina “habari njema” kwa “kila taifa na kabila na lugha na watu.”—Ufunuo 14:6.