Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

MNARA WA MLINZI Na. 2 2017 | Je, Utaithamini Zawadi Bora Zaidi ya Mungu?

WEWE UNA MAONI GANI?

Ni zawadi gani bora zaidi ambayo Mungu amewapatia wanadamu?

Biblia inasema hivi: “Mungu aliupenda ulimwengu sana hivi kwamba akamtoa Mwana wake mzaliwa-pekee.”Yohana 3:16.

Gazeti hili la Mnara wa Mlinzi linazungumzia ni kwa nini Mungu alimtuma Yesu duniani afe kwa ajili yetu na jinsi tunavyoweza kuonyesha kwamba tunathamini zawadi hiyo.

 

HABARI KUU

Zawadi ya Pekee Sana

Biblia inaeleza kuhusu zawadi yenye thamani kubwa, ambayo inawawezesha wale wanaoikubali kupata uzima wa milele. Je, kuna zawadi nyingine yenye thamani zaidi kuliko hiyo?

HABARI KUU

Zawadi Bora Zaidi ya Mungu—Kwa Nini Ni Yenye Thamani Sana?

Ni mambo gani yanayofanya zawadi iwe yenye thamani kuliko zingine? Kufikiria mambo hayo kunaweza kutusaidia kuthamini zaidi fidia.

HABARI KUU

Jinsi ya Kuithamini Zawadi Bora ya Mungu!

Upendo wa Kristo hutulazimisha kufanya nini?

Je, Useja ni Takwa la Wahudumu Wakristo?

Baadhi ya dini zimeweka sheria kwamba viongozi wa kanisa na makasisi wanapaswa kuwa waseja. Maandiko yanasema nini kuhusu jambo hilo?

Kutoka Utumwani—Nyakati za Kale na Sasa

Nyakati za kale, watu wa Mungu walitoka utumwani. Kwa kusikitisha, bado mamilioni ya watu leo wanaendelea kuteseka wakiwa watumwa.

Furahia Faida za Kuwa Mkarimu

Kuwa mkarimu kuna faida kwako na kwa wengine. Unawezaje kuwa mtoaji mchangamfu?

Biblia Inasema Nini?

Biblia inasema kwamba “siku za mwisho” zingekuwa “nyakati za hatari zilizo ngumu kushughulika nazo.” Je, maneno hayo yanapatana na mambo tunayoona katika siku zetu?

Habari Zaidi Mtandaoni