Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

Hekima Ni Ulinzi

Hekima Ni Ulinzi

“Fidia ya nafsi ya mtu ni utajiri wake, lakini maskini hajasikia kemeo.” —METHALI 13:8.

HATA ingawa utajiri unaweza kumletea mtu faida nyingi, unaweza pia kumletea mtu matatizo hasa katika nyakati hizi za hatari. (2 Timotheo 3:1-5) Katika sehemu fulani za ulimwengu, watu matajiri, kutia ndani watalii wameporwa na wezi au kutekwa nyara.

Katika nchi moja maskini, taarifa moja ya habari ilisema hivi: “Ujambazi, ulaghai, na utekaji-nyara ni matendo yanayosababisha uadui kati ya matajiri na maskini. Mikahawa hulindwa na walinzi wenye silaha; nyumba za matajiri huwa na kuta zenye nyaya zinazokata kama wembe, taa zenye mwanga mkali, kamera, na walinzi.” Hali hiyo iko katika nchi nyingi ulimwenguni.

Hata hivyo, Biblia inasema “maskini hajasikia kemeo.” Unawezaje kufaidika na ushauri huo wenye hekima? Ikiwa unaishi katika eneo lenye uhalifu na jeuri au ikiwa unahitaji kutembelea eneo kama hilo, usivae au kubeba vitu vitakavyofanya uonekane tajiri. Fikiria kwa makini nguo unazovaa na vitu unavyobeba hadharani, hasa ikiwa vitu hivyo vitaonekana waziwazi. Andiko la Methali 22:3, linasema hivi: “Mtu mwerevu ni yule ambaye ameona msiba na kujificha, lakini wasio na uzoefu wameendelea mbele nao lazima waumie.”

Hekima inayopatikana katika Biblia inaonyesha jinsi Muumba wetu anavyotujali, na kwamba anataka tuwe salama. Andiko la Mhubiri 7:12, husema hivi: “Hekima ni ulinzi . . . huwahifadhi hai waliyo nayo.”