HABARI KUU | MAJANGA YANAPOTOKEA
Majanga Yanapotokea
WAKATI fulani, sisi sote hupatwa na janga la aina fulani. Hata matajiri hupatwa pia na matatizo.
BIBLIA INASEMA HIVI:
“Si wenye mbio wanaoshinda katika mbio, wala wenye nguvu wanaoshinda katika pigano, wala pia wenye hekima wanaopata chakula, wala pia wenye uelewaji wanaokuwa na utajiri, wala wenye ujuzi wanaopata kibali; kwa sababu wakati na tukio lisilotazamiwa huwapata wote.”— Mhubiri 9:11.
Kwa hiyo jambo la kuzingatia si ikiwa utapatwa na janga bali jinsi utakavyokabiliana na hali hiyo. Kwa mfano:
Utafanyaje ukipoteza mali zako zote katika msiba wa asili?
Namna gani ukipatwa na ugonjwa hatari?
Na vipi mtu unayempenda akifa?
Mashahidi wa Yehova ambao ni wachapishaji wa gazeti hili, wanaamini kwamba Biblia inaweza kukusaidia kukabiliana na majanga na pia kupata tumaini la kweli. (Waroma 15:4) Chunguza mifano mitatu ifuatayo.