Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

 HABARI KUU | MAJANGA YANAPOTOKEA

Majanga Yanapotokea

Majanga Yanapotokea

WAKATI fulani, sisi sote hupatwa na janga la aina fulani. Hata matajiri hupatwa pia na matatizo.

BIBLIA INASEMA HIVI:

“Si wenye mbio wanaoshinda katika mbio, wala wenye nguvu wanaoshinda katika pigano, wala pia wenye hekima wanaopata chakula, wala pia wenye uelewaji wanaokuwa na utajiri, wala wenye ujuzi wanaopata kibali; kwa sababu wakati na tukio lisilotazamiwa huwapata wote.”— Mhubiri 9:11.

Kwa hiyo jambo la kuzingatia si ikiwa utapatwa na janga bali jinsi utakavyokabiliana na hali hiyo. Kwa mfano:

  • Utafanyaje ukipoteza mali zako zote katika msiba wa asili?

  • Namna gani ukipatwa na ugonjwa hatari?

  • Na vipi mtu unayempenda akifa?

Mashahidi wa Yehova ambao ni wachapishaji wa gazeti hili, wanaamini kwamba Biblia inaweza kukusaidia kukabiliana na majanga na pia kupata tumaini la kweli. (Waroma 15:4) Chunguza mifano mitatu ifuatayo.