Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

Inavunja Moyo na Kuharibu Imani

Inavunja Moyo na Kuharibu Imani

Inavunja Moyo na Kuharibu Imani

“MIILI ilitapakaa kila mahali nasi hatungeweza kutambua mahali nyumba yetu ilipokuwa,” akasema mwanamume fulani huko Sri Lanka baada ya tsunami kuharibu kijiji chao mnamo Desemba 2004. Katika makala moja kuhusu misiba, mhariri wa mambo ya kidini alisema kwamba nyakati nyingine yeye hujikuta akisali kwa hasira.

Watu wengi huona misiba ya asili kuwa ni adhabu kutoka kwa Mungu. Mwandishi mmoja alifafanua tufani moja kuwa “ngumi ya Mungu.” Nchini Marekani, viongozi fulani wa kidini walifafanua matukio kama ya Tufani Katrina kuwa “hasira ya Mungu” dhidi ya “majiji yaliyojaa dhambi.” Huko Sri Lanka, Wabudha wanaoshikilia sana imani waliwalaumu Wakristo kwa sababu ya tsunami, na hivyo kuongeza mgawanyiko wa kidini. Naye Mhindu mmoja mwenye cheo fulani hekaluni alisema kwamba mungu aitwaye Shiva alikuwa amekasirika kwa sababu watu hawakuwa wakiishi kwa njia inayofaa. Kiongozi wa dini ya Wabudha nchini Marekani alisema hivi kuhusu misiba ya asili: “Hatujui kwa nini mambo hayo hufanyika. Hata hatujui kwa nini tuko hapa.”

Unapoona picha za nyumba zilizoharibiwa, watu waliokufa, na watu walio na huzuni, je, nyakati nyingine wewe hujiuliza, ‘Kwa nini Mungu anaruhusu kuteseka kwingi hivyo?’ Au je, unafikiri ‘Mungu ana sababu nyingi za kuruhusu mambo kama hayo yatendeke lakini hajafunua sababu hizo’? Makala zinazofuata zitachunguza habari hiyo. Pia zitazungumzia hatua fulani ambazo watu wanaweza kuchukua ili kupunguza hatari ya kujeruhiwa na kufa wakati ambapo msiba wa asili unatokea.

[Picha katika ukurasa wa 3]

Viongozi wengi wa kidini hawajui kwa nini Mungu huruhusu misiba ya asili