Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

Njoo Usikilize Hotuba ya Watu Wote Yenye Kichwa “Ni Nani Tunayemtii?”

Njoo Usikilize Hotuba ya Watu Wote Yenye Kichwa “Ni Nani Tunayemtii?”

Njoo Usikilize Hotuba ya Watu Wote Yenye Kichwa “Ni Nani Tunayemtii?”

Watu wengi huchukizwa na wazo la kumtii mtu fulani. Wengi huwa na maoni ya kwamba wangependa kuwa na uhuru wa kufanya wapendavyo. Hata hivyo, ukweli ni kwamba sote huthamini utii katika maisha yetu ya kila siku. Kila mara unapofuata onyo fulani au kufuata maagizo, unaonyesha utii kwa kadiri fulani. Ni nani anayeweza kupinga kwamba watu wanahitaji kutii sheria za serikali ili kudumisha amani na utengamano katika jamii ya kibinadamu? Ebu wazia ni nini kingetokea iwapo watu wote wangekataa kutii sheria za barabarani?

Lakini wanadamu wanapowatawala wanadamu wenzao, mara nyingi matokeo huwa mabaya. Muda mrefu uliopita, Biblia ilisema kwamba “mwanadamu amemtawala mwanadamu kwa kumuumiza.” (Mhubiri 8:9) Je, kuna mtawala ambaye tunastahili kumtumaini na kumtii? Ikiwa yupo, tunaweza kumtambuaje? Na tunaweza kutarajia nini chini ya utawala wake? Maswali hayo yatajibiwa kwenye hotuba ya watu wote yenye kusisimua yenye kichwa, “Ni Nani Tunayemtii?” Hotuba hiyo itatolewa kwenye makusanyiko ya wilaya ya Mashahidi wa Yehova kuanzia mwezi huu. Mamia ya makusanyiko hayo yatafanywa ulimwenguni pote. Ili kujua kusanyiko litakalofanywa karibu nawe, wasiliana na Mashahidi wa Yehova katika eneo lenu au waandikie wachapishaji wa gazeti hili kwa kutumia anwani zilizoonyeshwa kwenye ukurasa wa 5.