DAFTARI LA MKUTANO WA HUDUMA NA MAISHA

Ratiba ya Mkutano wa Huduma na Maisha ya Mei 18-24, 2026

Kiswahili
Ratiba ya Mkutano wa Huduma na Maisha ya Mei 18-24, 2026
https://cms-imgp.jw-cdn.org/img/p/202026163/univ/art/202026163_univ_sqr_xl.jpg
mwb26 Mei kur. 5-16

Mei 18-24

ISAYA 62-64

Mei 18-24

Wimbo 44 na Sala | Utangulizi (Dak. 1)

HAZINA ZA NENO LA MUNGU

1. Mfinyanzi Mwenye Upendo na Huruma

(Dak. 10)

Yehova hushughulika nasi kwa huruma, hata tunapoteseka kwa sababu ya makosa yetu wenyewe (Isa 63:9; cl 253-254 ¶7-9)

Ingawa hatulindi kutokana na matokeo ya makosa yetu, yeye hutusaidia (w23.08 28-29 ¶8-9)

Tukimruhusu, ataendelea kutufinyanga ili tuwe kitu chenye thamani machoni pake (Isa 64:8; w13 9/15 20 ¶15-17)

2. Hazina za Kiroho

(Dak. 10)

  • Isa 63:10—Mstari huu unatufundisha nini kuhusu subira ya Yehova? (it “Rehema” ¶11)

  • Ungependa kushiriki nasi hazina gani kutoka kwenye usomaji wa Biblia wa juma hili?

3. Usomaji wa Biblia

BORESHA HUDUMA YAKO

4. Kuanzisha Mazungumzo

(Dak. 3) MAHUBIRI YA UMMA. Tafuta jambo linalomvutia mtu huyo, na ufanye mipango ya kuwasiliana naye tena. (lmd somo la 1 jambo kuu la 5)

5. Kufuatia Upendezi

(Dak. 4) NYUMBA KWA NYUMBA. Tumia video kutoka kwenye Sanduku la Vifaa vya Kufundishia. (lmd somo la 9 jambo kuu la 4)

6. Kufanya Wanafunzi

(Dak. 5) lff 254 sanduku “Je, Niko Tayari Kuhubiri Pamoja na Kutaniko?” Zungumza na mwanafunzi wako wa Biblia kuhusu lengo la kuwa mhubiri ambaye hajabatizwa. (lmd somo la 12 jambo kuu la 3)

MAISHA YA MKRISTO

Wimbo 115

7. Kuwa Tayari kwa Ajili ya Majanga—Tarajia Mambo Yasiyotazamiwa

(Dak. 15) Mazungumzo. Yaongozwe na mzee. Tia ndani vikumbusho kutoka kwa ofisi ya tawi na kutoka kwa baraza la wazee, ikiwa vipo.

Majanga, kutia ndani mashambulizi, yanaweza kutukia mahali popote bila kutarajiwa. (Mhu 9:11) Hata ikiwa unaishi katika eneo ambalo majanga ya asili hayatukii kwa ukawaida, ni jambo la hekima kutarajia mambo yasiyotazamiwa. (Met 22:3) Unawezaje kujitayarisha?

  • Unapokuwa kwenye maeneo ya umma, kazia uangalifu mazingira yanayokuzunguka, na uhakikishe kwamba unajua mahali ilipo milango ya dharura, hasa ikiwa upo katika eneo lenye watu wengi

  • Ili kujitayarisha kwa ajili ya janga la asili, andaa begi la dharura a na mahitaji ya dharura ya nyumbani. Panga jambo utakalofanya janga likitokea na uwe na habari za mawasiliano za watu wa familia na marafiki.—g17.5 4

Onyesha VIDEO Kuwa Tayari kwa Ajili ya Majanga: Tarajia Mambo Yasiyotazamiwa. Kisha waulize wasikilizaji:

  • Mwanzoni ndugu na dada walihisije kuhusu kujitayarisha kwa ajili ya majanga?

  • Ni hatua gani hususa walizochukua ili kujitayarisha?

  • Yehova alibariki jinsi gani jitihada zao za kujitayarisha kwa ajili ya janga?

  • Walijifunza nini kutokana na mambo waliyokabili?

JIULIZE, ‘Mtazamo wangu kuhusu kuwa tayari kwa ajili ya majanga unaonyeshaje kwamba ninamheshimu Yehova?’

LENGO: Unapokuwa katika maeneo ya umma juma hili, jiulize hivi: ‘Mlango wa dharura ulio karibu zaidi uko wapi?’

8. Funzo la Biblia la Kutaniko

Umalizio (Dak. 3) | Wimbo 151 na Sala

a Ona sanduku lenye kichwa “Je, Una Kile Kinachohitajika Wakati wa Dharura?” kwenye Amkeni! Na. 5 2017, uk. 6.