Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

Mei 5-11

METHALI 12

Mei 5-11

Wimbo 101 na Sala | Utangulizi (Dak. 1)

HAZINA ZA NENO LA MUNGU

1. Kufanya Kazi Kwa Bidii Huridhisha

(Dak. 10)

Usipoteze wakati wako kufuatia vitu visivyo na maana (Met 12:11)

Fanya kazi kwa bidii (Met 12:24; w16.06 30 ¶6)

Utathawabishwa kwa kufanya kazi kwa bidii (Met 12:14)

DOKEZO: Kufanya kazi kwa bidii kunaweza kutunufaisha ikiwa tutakazia fikira jinsi kazi hiyo itakavyowanufaisha wengine.—Mdo 20:35; w15 2/1 5 ¶4-6.

2. Hazina za Kiroho

(Dak. 10)

  • Met 12:16—Kanuni inayopatikana katika mstari huu inaweza kumsaidiaje mtu kuwa jasiri anapokabili hali ngumu? (ijwyp makala ya 95 ¶10-11)

  • Ungependa kushiriki nasi hazina gani kutoka kwenye usomaji wa Biblia wa juma hili?

3. Usomaji wa Biblia

BORESHA HUDUMA YAKO

4. Kuanzisha Mazungumzo

(Dak. 2) NYUMBA KWA NYUMBA. (lmd somo la 1 jambo kuu la 4)

5. Kuanzisha Mazungumzo

(Dak. 3) NYUMBA KWA NYUMBA. Anzisha funzo la Biblia. (lmd somo la 5 jambo kuu la 4)

6. Kufuatia Upendezi

(Dak. 3) MAHUBIRI YASIYO RASMI. Mwonyeshe mtu mwenye watoto tovuti yetu. (lmd somo la 9 jambo kuu la 3)

7. Kufafanua Imani Yako

(Dak. 3) Onyesho. ijwfq makala ya 3—Kichwa: Je, Unaamini Kwamba Dini Yako Tu Ndiyo ya Kweli? (lmd somo la 4 jambo kuu la 3)

MAISHA YA MKRISTO

Wimbo 21

8. Kukabiliana na Matatizo ya Kiuchumi kwa Msaada wa Yehova

(Dak. 15) Mazungumzo.

Je, una wasiwasi kuhusu kupata kazi, kupoteza kazi, au kushindwa kujitegemeza sasa au utakapozeeka? Mfumo wa kiuchumi wa ulimwengu huu unaweza kubadilika ghafla. Hata hivyo, Yehova anatuhakikishia kwamba ikiwa tutamtanguliza, sikuzote atatutimizia mahitaji yetu—hata ikiwa tunakabiliana na badiliko kubwa la kiuchumi lililotokea ghafla.—Zb 46:​1-3; 127:2; Mt 6:​31-33.

Onyesha VIDEO Yehova Hajatuacha Kamwe. Kisha waulize wasikilizaji:

  • Unajifunza nini kutokana na mambo ambayo Ndugu Alvarado alikabili?

Soma 1 Timotheo 5:8. Kisha waulize wasikilizaji:

  • Mstari huu unaimarishaje imani yako kwamba sikuzote Yehova atawaandalia waabudu wake mahitaji yao?

Fikiria baadhi ya kanuni za Biblia ambazo zinaweza kukusaidia unapokabili matatizo ya kiuchumi:

  • Rahisisha maisha yako. Punguza madeni na matumizi yasiyo ya lazima.—Mt 6:22

  • Fanya maamuzi kuhusu kazi na elimu yatakayokusaidia kutanguliza kwanza mambo ya kiroho.—Flp 1:​9-11

  • Uwe mnyenyekevu na ubadilikane kulingana na hali. Ikiwa hujaajiriwa, uwe tayari kufanya kazi yoyote—hata ikiwa ni kazi ya hali ya chini—ambayo itakusaidia kuiandalia familia yako.—Met 14:23

  • Uwe tayari kushiriki na wengine vitu ulivyo navyo, hata ikiwa una vitu vichache.—Ebr 13:16

9. Funzo la Biblia la Kutaniko

Umalizio (Dak. 3) | Wimbo 57 na Sala