Mei 19-25
METHALI 14
Wimbo 89 na Sala | Utangulizi (Dak. 1)
1. Tafakari kwa Makini Kuhusu Kile Utakachofanya Janga Linapotokea
(Dak. 10)
Uwe mwangalifu usiamini “kila neno” unalosikia (Met 14:15; w23.02 22-23 ¶10-12)
Usitegemee tu hisia zako, au uzoefu wako wa wakati uliopita (Met 14:12)
Usiwasikilize wale wanaokataa mwongozo kutoka kwa tengenezo la Yehova (Met 14:7)
JAMBO LA KUTAFAKARI: Je, wazee mmejitayarisha kufuata mwongozo na kumtegemea Yehova janga linapotokea?—w24.07 5 ¶11.
2. Hazina za Kiroho
(Dak. 10)
-
Met 14:17—Ni katika njia zipi “mtu anayechanganua mambo” anaweza kuchukiwa? (it-2 1094)
-
Ungependa kushiriki nasi hazina gani kutoka kwenye usomaji wa Biblia wa juma hili?
3. Usomaji wa Biblia
(Dak. 4) Met 14:1-21 (th somo la 11)
4. Kuanzisha Mazungumzo
(Dak. 3) MAHUBIRI YA UMMA. Shiriki jambo fulani kutoka kwenye Biblia na mtu anayekueleza kwamba anahangaishwa na hali ya kiuchumi. (lmd somo la 3 jambo kuu la 3)
5. Kufuatia Upendezi
(Dak. 4) NYUMBA KWA NYUMBA. Toa gazeti kuhusu habari ambayo mwenye nyumba alipendezwa nayo mlipozungumza wakati uliopita. (lmd somo la 9 jambo kuu la 4)
6. Kufanya Wanafunzi
(Dak. 5) Mtie moyo mwanafunzi wako asome Biblia kila siku, na umwonyeshe jinsi anavyoweza kufikia lengo lake. (th somo la 19)
Wimbo 126
7. Jitayarishe kwa Ajili ya Majanga
(Dak. 15) Mazungumzo.
Yaongozwe na mzee. Tia ndani vikumbusho kutoka kwa ofisi ya tawi na kutoka kwa baraza la wazee, ikiwa vipo.
Kadiri tunavyovumilia hali ngumu katika “siku za mwisho,” tunatarajia kwamba matatizo yataongezeka. (2Ti 3:1; nwtsty habari za utafiti Mt 24:8) Janga la asili linapotokea, mara nyingi watu wa Yehova hupokea mwongozo kwa wakati na unaookoa uhai. Hivyo, tunahitaji kutii na kujitayarisha sasa kiroho na kimwili ili tuokoke wakati huo.—Met 14:6, 8.
-
Jitayarishe Kiroho: Dumisha ratiba nzuri. Jifunze njia mbalimbali za kushiriki katika huduma. Usiwe na hofu hata ikiwa utatenganishwa kwa muda mfupi na wengine kutanikoni. (Met 14:30) Hujatenganishwa na Yehova Mungu na Kristo Yesu.—od 176 ¶15-17
-
Jitayarishe Kimwili: Mbali na mikoba ya dharura, kila familia inapaswa kuwa na chakula cha ziada, maji, dawa, na mahitaji mengine ikiwa itakuwa lazima kukaa ndani kwa muda mrefu.—Met 22:3; g17.5 4
Onyesha VIDEO Je, Umejitayarisha Kukabiliana na Majanga? Kisha waulize wasikilizaji:
-
Yehova anaweza kutusaidiaje wakati wa janga?
-
Tunaweza kuchukua hatua gani hususa ili kujitayarisha?
-
Tunawezaje kuwasaidia wengine ambao wameathiriwa na majanga?
8. Funzo la Biblia la Kutaniko
(Dak. 30) bt sura ya 26 ¶18-22, sanduku uk. 209