Mei 12-18
METHALI 13
Wimbo 34 na Sala | Utangulizi (Dak. 1)
1. Usipumbazwe na “Taa ya Waovu”
(Dak. 10)
Watu waovu hawana tumaini la wakati ujao (Met 13:9; it-2 196 ¶2-3)
Usishirikiane na wale wanaofanya mambo mabaya yaonekane kuwa mazuri (Met 13:20; w12 7/15 12 ¶3)
Yehova huwabariki waadilifu (Met 13:25; w04 7/15 31 ¶6)
Mara nyingi, maisha ya wale wanaofuatia tamaa za ulimwengu huu huwa kinyume na matarajio yao. Lakini wale wanaofanya mapenzi ya Yehova wanafurahia maisha yanayoridhisha kikweli
2. Hazina za Kiroho
(Dak. 10)
-
Met 13:24—Watu wana maoni gani yasiyofaa kuhusu upendo na nidhamu? (it-2 276 ¶2)
-
Ungependa kushiriki nasi hazina gani kutoka kwenye usomaji wa Biblia wa juma hili?
3. Usomaji wa Biblia
(Dak. 4) Met 13:1-17 (th somo la 10)
4. Kuanzisha Mazungumzo
(Dak. 3) NYUMBA KWA NYUMBA. Baada ya kuzungumza kuhusu tukio fulani la karibuni, mwonyeshe mwenye nyumba jambo litakalomvutia kutoka katika Biblia. (lmd somo la 2 jambo kuu la 5)
5. Kuanzisha Mazungumzo
(Dak. 4) MAHUBIRI YASIYO RASMI. Mwalike mtu huyo ahudhurie mikutano. (lmd somo la 2 jambo kuu la 3)
6. Hotuba
(Dak. 5) lmd nyongeza A jambo kuu la 9—Kichwa: Watoto Wanaowaheshimu na Kuwatii Wazazi Wao Watafanikiwa. (th somo la 16)
Wimbo 77
7. “Nuru ya Waadilifu Hung’aa kwa Uangavu”
(Dak. 8) Mazungumzo.
Tunapata ujuzi na hekima nyingi kutoka katika Neno la Mungu. Tunapotumia maishani mwetu mambo tuliyojifunza, tunapata mafanikio na furaha ya kudumu. Hilo ni jambo ambalo ulimwengu huu hauwezi kutupatia.
Onyesha VIDEO Ulimwengu Hauwezi Kukupa Kitu Ambacho Hauna. Kisha waulize wasikilizaji:
-
Hali ambayo Dada Gainanshina alikabili inaonyeshaje ubora wa “nuru ya waadilifu” inapolinganishwa na “taa ya waovu”?—Met 13:9
Usipoteze muda wako kamwe ukiwazia kuhusu mambo ya ulimwengu huu, au kujutia maamuzi uliyofanya yanayokuruhusu umtumikie Yehova. (1Yo 2:15-17) Badala yake, kazia fikira ‘thamani bora zaidi ya ujuzi’ ambao umepata.—Flp 3:8.
8. Mahitaji ya Kutaniko
(Dak. 7)
9. Funzo la Biblia la Kutaniko
(Dak. 30) bt sura ya 26 ¶9-17