Juni 30–Julai 6
METHALI 20
Wimbo 131 na Sala | Utangulizi (Dak. 1)
1. Jinsi ya Kuwa na Uchumba Wenye Mafanikio
(Dak. 10)
Uwe na maoni kama ya Yehova kuhusu uchumba (Met 20:24, 25; w24.05 26-27 ¶3-4)
Mchunguze mtu huyo kabla ya kuanzisha urafiki wa kimapenzi (Met 20:18; w24.05 22 ¶8)
Jitahidini kufahamiana vizuri wakati wa uchumba (Met 20:5; w24.05 28 ¶7-8)
KUMBUKA: Uchumba mzuri hauongozi tu kwenye ndoa, lakini unawasaidia watu wanaochumbiana kufanya uamuzi mzuri.
2. Hazina za Kiroho
(Dak. 10)
-
Met 20:27—Ni katika njia gani “pumzi ya mtu ni taa ya Yehova”? (it-2 196 ¶7)
-
Ungependa kushiriki nasi hazina gani kutoka kwenye usomaji wa Biblia wa juma hili?
3. Usomaji wa Biblia
(Dak. 4) Met 20:1-15 (th somo la 5)
4. Kuanzisha Mazungumzo
(Dak. 4) NYUMBA KWA NYUMBA. Mwenye nyumba anakueleza kwamba amehamia kutoka nchi nyingine hivi karibuni. (lmd somo la 3 jambo kuu la 3)
5. Kufuatia Upendezi
(Dak. 4) MAHUBIRI YA UMMA. Mweleze mtu huyo kuhusu programu ya JW Library®, na umsaidie kupakua programu hiyo kwenye kifaa chake cha kielektroni. (lmd somo la 9 jambo kuu la 5)
6. Kufafanua Imani Yako
(Dak. 4) Onyesho. ijwbq makala ya 159—Kichwa: Je, Wanyama Wanaenda Mbinguni? (lmd somo la 3 jambo kuu la 4)
Wimbo 78
7. Watie Moyo Wengine Wajaribu Programu Yetu ya Kujifunza Biblia
(Dak. 5.) Mazungumzo.
Kuanzisha mafunzo ya Biblia ni sehemu muhimu ya huduma yetu. Hatuwezi kuwasaidia watu kuwa wanafunzi ikiwa hatujifunzi nao Biblia. (Ro 10:13-15) Kwa nini usijiwekee lengo la kuanzisha funzo la Biblia moja kwa moja kwa ukawaida, unapohubiri nyumba kwa nyumba? Kwanza, jaribu kufikiria habari ambayo itamvutia mwenye nyumba. Kisha, mwonyeshe jinsi Biblia inavyoweza kujibu maswali yake na kumsaidia katika njia hususa.
Kiunganishi “Jaribu Funzo Letu la Biblia” kwenye jw.org kinaweza kukusaidia kuanzisha mafunzo ya Biblia kwa wale unaokutana nao.
-
Unaweza kutumiaje kiunganishi “Jaribu Funzo Letu la Biblia” kuanzisha funzo la Biblia?
-
Umepata njia gani zenye matokeo unazoweza kutumia kuanzisha mafunzo ya Biblia kwenye eneo unaloishi?
8. Video ya Juni ya Mambo Yaliyotimizwa na Tengenezo
(Dak. 10.) Onyesha VIDEO.
9. Funzo la Biblia la Kutaniko
(Dak. 30) bt sura ya 28 ¶8-15