Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

Juni 16-22

METHALI 18

Juni 16-22

Wimbo 90 na Sala | Utangulizi (Dak. 1)

HAZINA ZA NENO LA MUNGU

1. Watie Moyo Wale Wanaokabili Matatizo ya Kiafya

(Dak. 10)

Tumia hekima inayotoka kwa Mungu unapozungumza (Met 18:4; w22.10 22 ¶17)

Jitahidi kuelewa hali ambayo mtu anakabili (Met 18:13; mrt makala ya 19 sanduku)

Uwe rafiki anayetegemeka na mwenye subira (Met 18:24; wp23.1 14 ¶3–15 ¶1)

JIULIZE, ‘Ninaweza kufanya nini ili kumtegemeza mwenzi wangu wa ndoa, ikiwa anakabili matatizo ya afya ya kimwili au ya kiakili?’

2. Hazina za Kiroho

(Dak. 10)

  • Met 18:18—Kwa nini kura zilitumiwa katika nyakati za Biblia? (it-2 271-272)

  • Ungependa kushiriki nasi hazina gani kutoka kwenye usomaji wa Biblia wa juma hili?

3. Usomaji wa Biblia

BORESHA HUDUMA YAKO

4. Kuanzisha Mazungumzo

(Dak. 1) NYUMBA KWA NYUMBA. Mwenye nyumba anazungumza lugha nyingine. (lmd somo la 2 jambo kuu la 5)

5. Kufuatia Upendezi

(Dak. 3) MAHUBIRI YA UMMA. Mwenye nyumba anakuomba uzungumze kwa ufupi. (lmd somo la 7 jambo kuu la 4)

6. Kufuatia Upendezi

(Dak. 3) MAHUBIRI YASIYO RASMI. Mfundishe mtu huyo kweli muhimu kuhusu Ufalme wa Mungu. (lmd somo la 9 jambo kuu la 5)

7. Kufafanua Imani Yako

(Dak. 4) Onyesho. ijwfq makala ya 29—Kichwa: Je, Unaamini kwamba Dunia Iliumbwa kwa Siku Sita Zenye Urefu wa Saa 24? (lmd somo la 5 jambo kuu la 5)

MAISHA YA MKRISTO

Wimbo 144

8. Wasaidie Wapendwa Wako Wamkaribie Yehova “Bila Neno”

(Dak. 15) Mazungumzo.

Wengi wetu tunamjua mtu fulani ambaye kwa sasa hamtumikii Yehova—huenda ni mwenzi wetu wa ndoa, mtoto wetu, au rafiki mpendwa ambaye ameacha kushirikiana na kutaniko. Je, pindi fulani umewahi kumlazimisha mtu au kuzungumza naye kwa njia isiyo ya fadhili ukiwa na nia ya kumshawishi amtumikie Yehova? Ingawa nia yetu ni nzuri, maneno yetu yanaweza kufanya hali iwe mbaya hata zaidi. (Met 12:18) Je, ni njia gani nzuri ya kumsaidia?

Petro ya kwanza 3:1 inasema kwamba mume asiyeamini ‘anaweza kuvutwa bila neno.’ Hata ikiwa mume wa dada Mkristo anakataa kuzungumzia kweli za Biblia pamoja naye, bado anaweza kumsaidia mume huyo amjue Yehova. Mwenendo wake, ambao umefinyangwa na sifa za Mungu kama vile upendo, fadhili, na hekima, unaweza kulainisha moyo wake. (Met 16:23) Mwenendo wetu na kuwa wenye neema kunaweza kuwa na matokeo mazuri kwa wapendwa wetu ambao kwa sasa hawamtumikii Yehova.—“Neema” habari za utafiti Kol 4:​6, nwtsty.

Onyesha VIDEO Wapiganaji wa Imani Waliofanikiwa—Walio na Wenzi wa Ndoa Wasio Waamini. Kisha waulize wasikilizaji:

  • Unajifunza nini kutokana na mambo ambayo Dada Sasaki alikabili?

  • Unajifunza nini kutokana na mambo ambayo Dada Ito alikabili?

  • Unajifunza nini kutokana na mambo ambayo Dada Okada alikabili?

9. Funzo la Biblia la Kutaniko

Umalizio (Dak. 3) | Wimbo 60 na Sala