Februari 16-22

ISAYA 36-37

Februari 16-22

Wimbo 150 na Sala | Utangulizi (Dak. 1)

HAZINA ZA NENO LA MUNGU

1. “Usiogope kwa Sababu ya Maneno Uliyosikia”

(Dak. 10)

Rabshake alienda Yerusalemu ili kuwatisha watu wa Mungu (Isa 36:​1, 2; it “Hezekia” Na. 1 ¶14)

Alijaribu kuwafanya wajihisi kwamba wao ni dhaifu na hawana tumaini (Isa 36:8; ip-1 387 ¶10)

Aliwadhihaki kwa sababu walimwamini Yehova na wale walioongoza (Isa 36:​7, 18-20; ip-1 388 ¶13-14)

Watu wa Yehova hawahitaji kuwaogopa wale wanaojaribu kuwatisha.—Isa 37:​6, 7

PENDEKEZO KWA AJILI YA IBADA YA FAMILIA: Tazama VIDEO ”‏Ee Yehova, . . . Nimekutegemea Wewe,”‏ na mzungumzie masomo mliyojifunza.

2. Hazina za Kiroho

(Dak. 10)

  • Isa 37:29—Ni katika njia gani Yehova aliweka lijamu katikati ya midomo ya Mfalme Senakeribu? (it “Lijamu” ¶4)

  • Ungependa kushiriki nasi hazina gani kutoka kwenye usomaji wa Biblia wa juma hili?

3. Usomaji wa Biblia

BORESHA HUDUMA YAKO

4. Kuanzisha Mazungumzo

(Dak. 3) NYUMBA KWA NYUMBA. Shiriki kweli kutoka kwenye nyongeza A ya broshua Wapende Watu. (lmd somo la 1 jambo kuu la 4)

5. Kuanzisha Mazungumzo

(Dak. 4) MAHUBIRI YASIYO RASMI. (lmd somo la 3 jambo kuu la 5)

6. Kufafanua Imani Yako

(Dak. 5) Onyesho. ijwbq makala ya 110 ¶1-4—Kichwa: Ubatizo Ni Nini? (th somo la 17)

MAISHA YA MKRISTO

Wimbo 118

7. “Ujasiri Wako Unategemea Msingi Gani?”

(Dak. 15) Mazungumzo.

Je, mtu amewahi kutilia shaka au kukudhihaki kwa sababu unamwamini Mungu, unaiamini Biblia, au kwa sababu ya uamuzi wako wa kuwa mmoja wa Mashahidi wa Yehova? Ikiwa ndivyo, huenda ulihisi wasiwasi au woga. Mambo ambayo wengine wanasema yanaweza kukufanya uwe na shaka. Unawezaje kuzuia hilo lisitukie?

Soma Isaya 36:4. Kisha waulize wasikilizaji:

  • Kwa nini ni muhimu tuimarishe uhakika kuelekea kile tunachoamini?

Onyesha VIDEO Maisha Yangu ya Utineja—Je, Inapatana na Akili Kuamini Kwamba Kuna Mungu? Kisha waulize wasikilizaji:

  • Elibaldo na Crystal walifanya nini ili kuimarisha imani yao?

  • Ni nini kinachokuthibitishia kwamba Mungu yupo?

  • Ni mistari gani ya Biblia inayoimarisha imani yako kwamba . . .

    Yehova anakupenda?

    Sikuzote Yehova atakusaidia?

    Umewapata watu wa Mungu?

8. Funzo la Biblia la Kutaniko

(Dak. 30) lfb somo la 62-63

Umalizio (Dak. 3) | Wimbo 9 na Sala