MAISHA YA MKRISTO
Simama Imara Mwisho Unapozidi Kukaribia
KWA NINI NI MUHIMU?: Hivi karibuni matukio yenye kustaajabisha yatatokea na tutahitaji kuwa jasiri na kumtegemea Yehova kuliko wakati mwingine wowote. Dhiki kuu itaanza kwa kuharibiwa kwa dini ya uwongo. (Mt 24:21; Ufu 17:16, 17) Katika kipindi hicho chenye msukosuko, tutahitaji kuhubiri ujumbe wa hukumu. (Ufu 16:21) Tutakabili shambulizi kutoka kwa Gogu wa Magogu. (Eze 38:10-12, 14-16) Kisha Yehova atawalinda watu wake kwa kuleta “vita vya siku kuu ya Mungu Mweza-Yote.” (Ufu 16:14, 16) Ili tuweze kukabiliana na matukio hayo ya wakati ujao kwa ujasiri, tunahitaji kuendelea kudumisha ushikamanifu wetu imani yetu inapojaribiwa sasa.
JINSI YA KUFANYA HIVYO:
-
Tetea kwa ujasiri viwango vya juu vya maadili vya Yehova.—Isa 5:20
-
Endelea kuabudu pamoja na Wakristo wenzako.—Ebr 10:24, 25
-
Fuata haraka mwongozo kutoka kwa tengenezo la Yehova.—Ebr 13:17
-
Tafakari kuhusu jinsi Yehova alivyowaokoa watu wake nyakati za kale.—2Pe 2:9
-
Sali kwa Yehova, na umtegemee.—Zb 112:7, 8
TAZAMENI VIDEO YENYE KICHWA MATUKIO YA WAKATI UJAO YATAKAYOHITAJI UJASIRI—KISEHEMU, KISHA MJIBU MASWALI YAFUATAYO:
-
Utii wa wahubiri ulijaribiwaje kutaniko lao lilipounganishwa na makutaniko mengine?
-
Kuna uhusiano gani kati ya ujasiri na utii?
-
Kwa nini tutahitaji ujasiri Har–Magedoni itakapokuja?
-
Jitayarishe sasa kukabiliana na matukio ya wakati ujao yatakayojaribu ujasiri wetu
Ni simulizi gani la Biblia linaloweza kutusaidia kuimarisha imani yetu katika nguvu za Yehova za kuokoa?—2Nya 20:1-24

