DAFTARI LA MKUTANO WA HUDUMA NA MAISHA

Simama Imara Mwisho Unapozidi Kukaribia

Kiswahili
Simama Imara Mwisho Unapozidi Kukaribia
https://cms-imgp.jw-cdn.org/img/p/202020284/univ/art/202020284_univ_sqr_xl.jpg
mwb20 Agosti uku. 3

MAISHA YA MKRISTO

Simama Imara Mwisho Unapozidi Kukaribia

Simama Imara Mwisho Unapozidi Kukaribia

KWA NINI NI MUHIMU?: Hivi karibuni matukio yenye kustaajabisha yatatokea na tutahitaji kuwa jasiri na kumtegemea Yehova kuliko wakati mwingine wowote. Dhiki kuu itaanza kwa kuharibiwa kwa dini ya uwongo. (Mt 24:21; Ufu 17:16, 17) Katika kipindi hicho chenye msukosuko, tutahitaji kuhubiri ujumbe wa hukumu. (Ufu 16:21) Tutakabili shambulizi kutoka kwa Gogu wa Magogu. (Eze 38:10-12, 14-16) Kisha Yehova atawalinda watu wake kwa kuleta “vita vya siku kuu ya Mungu Mweza-Yote.” (Ufu 16:14, 16) Ili tuweze kukabiliana na matukio hayo ya wakati ujao kwa ujasiri, tunahitaji kuendelea kudumisha ushikamanifu wetu imani yetu inapojaribiwa sasa.

JINSI YA KUFANYA HIVYO:

  • Tetea kwa ujasiri viwango vya juu vya maadili vya Yehova.​—Isa 5:20

  • Endelea kuabudu pamoja na Wakristo wenzako.​—Ebr 10:24, 25

  • Fuata haraka mwongozo kutoka kwa tengenezo la Yehova.​—Ebr 13:17

  • Tafakari kuhusu jinsi Yehova alivyowaokoa watu wake nyakati za kale.​—2Pe 2:9

  • Sali kwa Yehova, na umtegemee.​—Zb 112:7, 8

TAZAMENI VIDEO YENYE KICHWA MATUKIO YA WAKATI UJAO YATAKAYOHITAJI UJASIRIKISEHEMU, KISHA MJIBU MASWALI YAFUATAYO:

  • Utii wa wahubiri ulijaribiwaje kutaniko lao lilipounganishwa na makutaniko mengine?

  • Kuna uhusiano gani kati ya ujasiri na utii?

  • Kwa nini tutahitaji ujasiri Har–Magedoni itakapokuja?

  • Jitayarishe sasa kukabiliana na matukio ya wakati ujao yatakayojaribu ujasiri wetu

    Ni simulizi gani la Biblia linaloweza kutusaidia kuimarisha imani yetu katika nguvu za Yehova za kuokoa?​—2Nya 20:1-24