Wimbo wa Sulemani 6:1-13
6 “Mpenzi wako ameenda wapi,Ewe mwanamke mrembo kuliko wote?
Mpenzi wako amegeuka na kufuata njia gani?
Acha tukamtafute pamoja nawe.”
2 “Mpenzi wangu ameshuka kwenda kwenye bustani yake,Kwenye kitalu cha mimea ya viungo,Kuchunga kondoo kwenye bustaniNa kuchuma mayungiyungi.+
3 Mimi ni wa mpenzi wangu,Na mpenzi wangu ni wangu mimi.+
Anachunga kondoo kati ya mayungiyungi.”+
4 “Wewe ni mrembo, kama Tirsa,*+ mpenzi wangu,+Unapendeza kama Yerusalemu,+Unavutia sana kama majeshi yaliyokusanyika kuzunguka bendera zao.+
5 Usinitazame,+Ukinitazama nahangaika.
Nywele zako ni kama kundi la mbuziLinaloshuka kwenye miteremko ya Gileadi.+
6 Meno yako ni kama kundi la kondooAmbao wametoka kuoshwa,Wote wamezaa mapacha,Na hakuna yeyote aliyepoteza watoto wake.
7 Kama kipande cha komamangaNdivyo yalivyo mashavu yako nyuma ya shela yako.
8 Hata kukiwa na malkia 60
Na masuria 80
Na wasichana wasiohesabika.+
9 Lakini kuna mmoja tu ambaye ni njiwa wangu,+ mpenzi wangu asiye na kasoro.
Binti pekee kwa mama yake.
Yeye ni kipenzi cha mama yake.*
Mabinti wanapomwona, humtangaza kuwa mwenye furaha;Malkia na masuria humsifu.
10 ‘Ni mwanamke gani anayeng’aa* kama mapambazuko,Mrembo kama mwezi mpevu,Aliye mwangavu kama nuru ya jua,Mwenye kuvutia sana kama majeshi yaliyokusanyika kuzunguka bendera zao?’”+
11 “Nilishuka kwenye bustani ya miti yenye kokwa+Ili nione machipukizi bondeni,Nione ikiwa mzabibu umechipuaIkiwa mikomamanga imechanua.
12 Bila kutarajia,Tamaa yangu ilinifikishaKwenye magari ya watu wangu waungwana.”*
13 “Rudi, rudi, ewe Mshulami!
Rudi, rudi,Ili tukutazame!”
“Kwa nini mnamkodolea macho Mshulami?”+
“Yeye ni kama dansi ya kambi mbili!”*
Maelezo ya Chini
^ Au “Jiji Linalopendeza.”
^ Tnn., “ndiye aliye safi sana kwa yule aliyemzaa.”
^ Tnn., “anayetazama chini.”
^ Au “watu wangu walio tayari kusaidia.”
^ Au “dansi ya Mahanaimu.”