Ezekieli 19:1-14
-
Wimbo wa huzuni kwa ajili ya wakuu wa Israeli (1-14)
19 “Nawe lazima uimbe wimbo wa huzuni* kuhusu wakuu wa Israeli,
2 useme,
‘Mama yako alikuwa nani? Simba jike kati ya simba.
Alilala kati ya wanasimba wenye nguvu* naye akawalea watoto wake.
3 Alimlea mmoja wa watoto wake, akawa mwanasimba mwenye nguvu.+
Naye akajifunza jinsi ya kurarua mawindo,
Akamnyafua hata mwanadamu.
4 Mataifa yalisikia kumhusu na wakamkamata katika shimo lao,
Nao wakamleta kwa kulabu nchini Misri.+
5 Mama huyo alisubiri na hatimaye akaona hakuna tumaini kwamba atarudi.
Basi akamchukua mwingine kati ya watoto wake na kumtuma akiwa mwanasimba mwenye nguvu.
6 Yeye pia alitembea huku na huku kati ya simba, naye akawa mwanasimba mwenye nguvu.
Akajifunza jinsi ya kurarua mawindo, na hata akawanyafua wanadamu.+
7 Akazungukazunguka katika minara yao yenye ngome na kuyaharibu majiji yao,
Hivi kwamba nchi iliyo ukiwa ikajaa sauti ya mngurumo wake.+
8 Mataifa ya wilaya jirani yalikuja dhidi yake ili kuutandaza wavu wao juu yake,
Naye akanaswa katika shimo lao.
9 Wakamweka katika kizimba kwa kulabu na kumpeleka kwa mfalme wa Babiloni.
Wakamfunga huko ili sauti yake isisikike tena kwenye milima ya Israeli.
10 Mama yako alikuwa kama mzabibu+ katika damu yako,* uliopandwa kando ya maji.
Ukazaa matunda na kujaa matawi kwa sababu ya maji mengi.
11 Nao ukatokeza matawi yenye nguvu,* yanayofaa kuwa fimbo za ufalme za watawala.
Ukakua, ukawa mrefu kuliko miti mingine,
Nao ukaonekana kwa sababu ya urefu wake na wingi wa majani yake.
12 Lakini aling’olewa kwa ghadhabu+ na kutupwa chini ardhini,
Na upepo wa mashariki ukayakausha matunda yake.
Matawi yake yenye nguvu yalikatwa yakakauka,+ na moto ukayateketeza.+
13 Sasa amepandwa nyikani,
Katika nchi isiyo na maji na yenye kiu.+
14 Moto ukaenea kutoka kwenye matawi yake* na kuteketeza machipukizi yake na matunda yake,
Na hakuna tawi lenye nguvu lililobaki, hakuna fimbo ya mfalme ya kutawala.+
“‘Huo ni wimbo wa huzuni, nao utatumiwa kama wimbo wa huzuni.’”
Maelezo ya Chini
^ Au “wimbo wa maombolezo.”
^ Au “wanasimba wenye manyoya marefu shingoni.”
^ Au labda, “kama mzabibu katika shamba lako la mizabibu.”
^ Au “fimbo zenye nguvu.”
^ Au “fimbo zake.”