Barua ya Pili kwa Wathesalonike 3:1-18
3 Mwishowe, akina ndugu, endeleeni kusali kwa ajili yetu,+ ili neno la Yehova* lizidi kuenea upesi+ na kutukuzwa, kama ilivyo kwenu,
2 na kwamba tukombolewe kutoka kwa watu hatari na waovu,+ kwa maana imani si mali ya watu wote.+
3 Lakini Bwana ni mwaminifu, naye atawaimarisha na kuwalinda dhidi ya yule mwovu.
4 Zaidi ya hayo, tuna uhakika katika Bwana kuwahusu ninyi, kwamba mnafanya na mtaendelea kufanya mambo tunayowaagiza.
5 Bwana na aendelee kuongoza mioyo yenu ili mfanikiwe kumpenda Mungu+ na kuvumilia+ kwa ajili ya Kristo.
6 Sasa akina ndugu, tunawaagiza katika jina la Bwana Yesu Kristo, mjiepushe na kila ndugu asiyefuata utaratibu+ na desturi* mlizopokea* kutoka kwetu.+
7 Kwa maana ninyi wenyewe mnajua jinsi mnavyopaswa kutuiga,+ kwa sababu hatukukosa kufuata utaratibu tulipokuwa nanyi,
8 wala hatukula chakula cha yeyote bure.*+ Badala yake, tulifanya kazi ngumu na yenye kutaabisha usiku na mchana ili tusimpe yeyote kati yenu mzigo wenye gharama.+
9 Si kwamba hatuna mamlaka,+ bali tulitaka kuwawekea mfano ili mtuige.+
10 Kwa kweli, tulipokuwa nanyi tulikuwa tukiwaagiza hivi: “Mtu yeyote asiyetaka kufanya kazi, asile chakula.”+
11 Kwa maana tunasikia watu fulani miongoni mwenu hawafuati utaratibu,+ hawafanyi kazi yoyote, bali wanajiingiza katika mambo yasiyowahusu.+
12 Tunawaagiza watu hao na kuwahimiza katika Bwana Yesu Kristo wafanye kazi kwa utulivu na kula chakula ambacho wao wenyewe wamekifanyia kazi.+
13 Nanyi akina ndugu, msichoke kutenda mema.
14 Lakini ikiwa yeyote hatii maneno yetu kupitia barua hii, mtieni alama na mwache kushirikiana naye,+ ili aone aibu.
15 Lakini msimwone mtu huyo kama adui, bali endeleeni kumwonya+ kama ndugu.
16 Basi, Bwana wa amani na aendelee kuwapa amani kwa kila njia.+ Bwana awe nanyi nyote.
17 Hii ni salamu yangu, mimi Paulo, kwa mkono wangu mwenyewe,+ ambayo ni ishara katika kila barua; hivi ndivyo ninavyoandika.
18 Fadhili zisizostahiliwa za Bwana wetu Yesu Kristo na ziwe pamoja nanyi nyote.
Maelezo ya Chini
^ Angalia Nyongeza A5.
^ Au “maagizo.”
^ Au labda, “walizopokea.”
^ Au “bila kulipa.”