Kitabu cha Pili cha Mambo ya Nyakati 16:1-14

  • Asa afanya mkataba na Siria (1-6)

  • Hanani amkemea Asa (7-10)

  • Kifo cha Asa (11-14)

16  Katika mwaka wa 36 wa utawala wa Asa, Mfalme Baasha+ wa Israeli alikuja kushambulia Yuda, akaanza kujenga* Rama+ ili kumzuia mtu yeyote asitoke wala kuingia kwa* Mfalme Asa wa Yuda.+  Ndipo Asa akatoa fedha na dhahabu kutoka katika hazina za nyumba ya Yehova+ na nyumba ya* mfalme na kumpelekea Mfalme Ben-hadadi wa Siria,+ aliyekuwa akiishi Damasko, akamwambia:  “Kuna mkataba* kati yangu na wewe na kati ya baba yangu na baba yako. Ninakutumia fedha na dhahabu. Njoo, vunja mkataba wako* na Mfalme Baasha wa Israeli, ili aondoke kwangu.”  Ben-hadadi akamsikiliza Mfalme Asa, akawatuma wakuu wa majeshi yake kushambulia majiji ya Israeli, wakashinda Iyoni,+ Dani,+ Abel-maimu, na maghala yote ya majiji ya Naftali.+  Baasha aliposikia habari hizo, mara moja akaacha kujenga* Rama, akasimamisha kazi hiyo.  Kisha Mfalme Asa akawachukua watu wote wa Yuda, nao wakabeba mawe na mbao zilizokuwa zikitumiwa na Baasha kujenga Rama,+ akazitumia kujenga* Geba+ na Mispa.+  Wakati huo mwonaji Hanani+ akaja kwa Mfalme Asa wa Yuda na kumwambia: “Kwa sababu ulimtegemea* mfalme wa Siria nawe hukumtegemea* Yehova Mungu wako, jeshi la mfalme wa Siria limeponyoka kutoka mikononi mwako.+  Je, Waethiopia na Walibya hawakuwa jeshi kubwa sana lenye magari mengi ya vita na wapanda farasi? Lakini kwa sababu ulimtegemea Yehova, aliwatia mikononi mwako.+  Kwa maana macho ya Yehova yanaenda huku na huku duniani kote+ ili adhihirishe nguvu zake* kwa niaba ya wale ambao moyo wao ni kamili* kumwelekea yeye.+ Umetenda kwa upumbavu katika jambo hili; kuanzia sasa na kuendelea kutakuwa na vita dhidi yako.”+ 10  Hata hivyo, Asa akamkasirikia mwonaji huyo na kumtia gerezani,* alikasirishwa sana naye kwa sababu ya jambo hilo. Wakati huohuo, Asa akaanza kuwatesa watu wengine. 11  Sasa historia ya Asa, kuanzia mwanzo mpaka mwisho, imeandikwa katika Kitabu cha Wafalme wa Yuda na wa Israeli.+ 12  Katika mwaka wa 39 wa utawala wake, Asa alishikwa na ugonjwa miguuni, akawa mgonjwa sana; na hata alipokuwa mgonjwa, hakumwomba Yehova msaada, bali waponyaji. 13  Kisha Asa akafa na kuzikwa pamoja na mababu zake;+ alikufa katika mwaka wa 41 wa utawala wake. 14  Kwa hiyo walimzika katika kaburi lake la kifahari alilokuwa amejichimbia katika Jiji la Daudi;+ walimlaza kwenye machela ya kubebea maiti iliyojazwa mafuta ya zeri na mafuta* yaliyotengenezwa kwa njia ya pekee kwa mchanganyiko wa vikolezo mbalimbali.+ Isitoshe, waliwasha moto mkubwa isivyo kawaida kwa ajili yake.*

Maelezo ya Chini

Au “kuimarisha; kujenga upya.”
Au “asiondoke wala kuingia katika eneo la.”
Au “jumba la.”
Au “agano.”
Au “agano lako.”
Au “kuimarisha; kujenga upya.”
Au “kuimarisha; kujenga upya.”
Tnn., “ulimwegemea.”
Tnn., “hukumwegemea.”
Au “una ujitoaji kamili.”
Au “utegemezo wake.”
Tnn., “katika nyumba ya mikatale.”
Au “marhamu.”
Inaonekana kwamba hawakuichoma maiti ya Asa, bali walichoma vikolezo vyenye manukato.