Barua ya Kwanza kwa Wathesalonike 1:1-10
1 Paulo, Silvano,*+ na Timotheo,+ kwa kutaniko la Wathesalonike walio katika muungano na Mungu Baba na Bwana Yesu Kristo:
Na muwe na fadhili zisizostahiliwa na amani.
2 Sikuzote tunamshukuru Mungu tunapowataja nyote katika sala zetu,+
3 kwa maana tunaendelea kukumbuka kazi yenu ya uaminifu, kazi yenu ngumu ya upendo, na jinsi ambavyo mmevumilia kwa sababu ya tumaini lenu+ katika Bwana wetu Yesu Kristo mbele za Mungu, Baba yetu.
4 Akina ndugu, tunajua Mungu anawapenda na amewachagua,
5 kwa sababu hatukuwahubiria habari njema kwa maneno tu, bali pia kwa nguvu na kwa roho takatifu na kwa usadikisho thabiti, kama mnavyojua jinsi tulivyotenda miongoni mwenu kwa ajili yenu.
6 Nanyi mlituiga sisi+ na Bwana pia,+ kwa kuwa mlilikubali neno kwa shangwe ya roho takatifu ingawa mlikuwa na dhiki nyingi,+
7 na hivyo mkawa mfano mzuri kwa waamini wote katika Makedonia na Akaya.
8 Kwa kweli, mmelitangaza neno la Yehova* katika Makedonia na Akaya, na pia kila mahali watu wamesikia kuhusu imani yenu katika Mungu,+ hivi kwamba hatuhitaji kusema lolote.
9 Watu hao wanaendelea kusema jinsi tulivyowahubiria ninyi mara ya kwanza na jinsi mlivyomgeukia Mungu na kuacha kuabudu sanamu+ ili kumtumikia Mungu wa kweli aliye hai,
10 na kumsubiri Mwana wake aje kutoka mbinguni,+ ambaye alifufuliwa kutoka kwa wafu, yaani, Yesu, anayetukomboa kutoka kwenye ghadhabu inayokuja.+