Barua ya Kwanza kwa Wathesalonike 1:1-10

  • Salamu (1)

  • Shukrani kwa ajili ya imani ya Wathesalonike (2-10)

1  Paulo, Silvano,*+ na Timotheo,+ kwa kutaniko la Wathesalonike walio katika muungano na Mungu Baba na Bwana Yesu Kristo: Na muwe na fadhili zisizostahiliwa na amani.  Sikuzote tunamshukuru Mungu tunapowataja nyote katika sala zetu,+  kwa maana tunaendelea kukumbuka kazi yenu ya uaminifu, kazi yenu ngumu ya upendo, na jinsi ambavyo mmevumilia kwa sababu ya tumaini lenu+ katika Bwana wetu Yesu Kristo mbele za Mungu, Baba yetu.  Akina ndugu, tunajua Mungu anawapenda na amewachagua,  kwa sababu hatukuwahubiria habari njema kwa maneno tu, bali pia kwa nguvu na kwa roho takatifu na kwa usadikisho thabiti, kama mnavyojua jinsi tulivyotenda miongoni mwenu kwa ajili yenu.  Nanyi mlituiga sisi+ na Bwana pia,+ kwa kuwa mlilikubali neno kwa shangwe ya roho takatifu ingawa mlikuwa na dhiki nyingi,+  na hivyo mkawa mfano mzuri kwa waamini wote katika Makedonia na Akaya.  Kwa kweli, mmelitangaza neno la Yehova* katika Makedonia na Akaya, na pia kila mahali watu wamesikia kuhusu imani yenu katika Mungu,+ hivi kwamba hatuhitaji kusema lolote.  Watu hao wanaendelea kusema jinsi tulivyowahubiria ninyi mara ya kwanza na jinsi mlivyomgeukia Mungu na kuacha kuabudu sanamu+ ili kumtumikia Mungu wa kweli aliye hai, 10  na kumsubiri Mwana wake aje kutoka mbinguni,+ ambaye alifufuliwa kutoka kwa wafu, yaani, Yesu, anayetukomboa kutoka kwenye ghadhabu inayokuja.+

Maelezo ya Chini

Pia anaitwa Sila.