Barua ya Kwanza kwa Wakoritho 3:1-23

  • Bado Wakorintho ni wa kimwili (1-4)

  • Mungu hufanya ikue (5-9)

    • Wafanyakazi wenzi wa Mungu (9)

  • Jengeni kwa vifaa visivyoshika moto (10-15)

  • Ninyi ni hekalu la Mungu (16, 17)

  • Hekima ya ulimwengu ni upumbavu kwa Mungu (18-23)

3  Basi akina ndugu, mimi sikuweza kuzungumza nanyi kama watu wa kiroho,+ bali kama watu wa kimwili, kama watoto+ katika Kristo.  Niliwalisha maziwa, si chakula kigumu, kwa maana mlikuwa bado hamna nguvu za kutosha. Kwa kweli, hata sasa hamna nguvu za kutosha,+  kwa maana bado ninyi ni wa kimwili.+ Kwa kuwa kuna wivu na mizozo kati yenu, je, ninyi si wa kimwili+ na je, hamtembei kama wanadamu wanavyotembea?  Kwa maana mtu mmoja anaposema, “Mimi ni wa Paulo,” naye mwingine anasema, “Mimi ni wa Apolo,”+ je, hamfanyi kama wanadamu tu?  Basi, Apolo ni nani? Ndiyo, Paulo ni nani? Wahudumu+ ambao kupitia wao mlikuja kuwa waamini, kama vile Bwana alivyomwezesha kila mmoja.  Mimi nilipanda,+ Apolo akatia maji,+ lakini Mungu akaendelea kuikuza,  hivi kwamba anayepanda si kitu wala anayetia maji, bali Mungu anayeikuza.+  Basi anayepanda na anayetia maji ni kitu kimoja,* lakini kila mtu atapokea thawabu yake kulingana na kazi yake mwenyewe.+  Kwa maana sisi ni wafanyakazi wenzi wa Mungu. Ninyi ni shamba la Mungu linalolimwa, jengo la Mungu.+ 10  Kulingana na fadhili zisizostahiliwa za Mungu nilizopewa, niliweka msingi,+ nikiwa mjenzi mkuu mwenye ustadi,* hata hivyo, mtu mwingine anajenga juu yake. Lakini kila mmoja na aendelee kuangalia jinsi anavyojenga juu yake. 11  Kwa maana hakuna mtu yeyote anayeweza kuweka msingi mwingine wowote zaidi ya ule uliowekwa, ambao ni Yesu Kristo.+ 12  Basi yeyote akijenga juu ya msingi huo dhahabu, fedha, mawe ya thamani, mbao, nyasi kavu, au majani makavu, 13  kazi ya kila mmoja itaonekana jinsi ilivyo,* kwa maana ile siku itaifichua, kwa sababu itafunuliwa kupitia moto,+ na moto wenyewe utaonyesha jinsi kila mmoja alivyojenga. 14  Ikiwa kazi ya yeyote aliyejenga juu yake itabaki, atapokea thawabu; 15  ikiwa kazi ya yeyote itateketea, atapata hasara, lakini yeye mwenyewe ataokolewa; hata hivyo, itakuwa ni kama kupitia moto. 16  Je, hamjui kwamba ninyi ni hekalu la Mungu,+ na kwamba roho ya Mungu inakaa ndani yenu?+ 17  Yeyote akiliangamiza hekalu la Mungu, Mungu atamwangamiza; kwa maana hekalu la Mungu ni takatifu, nanyi ni hekalu hilo.+ 18  Mtu yeyote asijidanganye: Ikiwa yeyote miongoni mwenu anafikiri ana hekima katika mfumo huu wa mambo,* acheni awe mpumbavu ili awe na hekima. 19  Kwa maana hekima ya ulimwengu huu ni upumbavu kwa Mungu, kwa kuwa imeandikwa: “Yeye huwanasa wenye hekima katika ujanja wao wenyewe.”+ 20  Na tena: “Yehova* anajua kwamba kufikiri kwa watu wenye hekima ni ubatili.”+ 21  Basi yeyote asijisifu katika watu; kwa maana vitu vyote ni vyenu, 22  iwe ni Paulo au Apolo au Kefa*+ au ulimwengu au uzima au kifo au mambo yaliyopo sasa au mambo yatakayokuja, vitu vyote ni vyenu; 23  nanyi ni wa Kristo;+ naye Kristo ni wa Mungu.

Maelezo ya Chini

Au “ wana kusudi moja.”
Au “msimamizi wa kazi mwenye hekima.”
Tnn., “itafunuliwa.”
Angalia Kamusi, “Mfumo wa mambo.”
Pia anaitwa Petro.