Kitabu cha Kwanza cha Mambo ya Nyakati 27:1-34

  • Maofisa waliomtumikia mfalme (1-34)

27  Hii ndiyo idadi ya Waisraeli, viongozi wa koo,* wakuu wa maelfu na wa mamia,+ na maofisa wao waliomhudumia mfalme+ katika kila jambo lililohusu vikundi ambavyo viliingia ndani na kutoka nje mwezi baada ya mwezi, miezi yote ya mwaka; kila kikundi kilikuwa na watu 24,000.  Msimamizi wa kikundi cha kwanza kwa ajili ya mwezi wa kwanza alikuwa Yashobeamu+ mwana wa Zabdieli, na kikundi chake kilikuwa na watu 24,000.  Kati ya wana wa Perezi,+ yeye ndiye aliyekuwa kiongozi wa wakuu wote wa vikundi vilivyopewa zamu ya kutumikia katika mwezi wa kwanza.  Msimamizi wa kikundi cha mwezi wa pili alikuwa Dodai+ Mwahohi,+ na Miklothi ndiye aliyekuwa kiongozi, na kikundi chake kilikuwa na watu 24,000.  Msimamizi wa kikundi cha tatu kilichopewa zamu ya kutumikia katika mwezi wa tatu alikuwa Benaya+ mwana wa Yehoyada+ mkuu wa makuhani, na kikundi chake kilikuwa na watu 24,000.  Huyo Benaya alikuwa shujaa hodari miongoni mwa wale 30 na ndiye aliyekuwa msimamizi wao, na kiongozi wa kikundi chake alikuwa Amizabadi mwanawe.  Msimamizi wa nne kwa ajili ya mwezi wa nne alikuwa Asaheli,+ ndugu ya Yoabu,+ na baada yake Zebadia mwanawe, na kikundi chake kilikuwa na watu 24,000.  Msimamizi wa tano kwa ajili ya mwezi wa tano alikuwa Shamhuthi Mwizrahia, na kikundi chake kilikuwa na watu 24,000.  Msimamizi wa sita kwa ajili ya mwezi wa sita alikuwa Ira+ mwana wa Ikeshi Mtekoa,+ na kikundi chake kilikuwa na watu 24,000. 10  Msimamizi wa saba kwa ajili ya mwezi wa saba alikuwa Helezi+ Mpeloni kutoka kwa Waefraimu, na kikundi chake kilikuwa na watu 24,000. 11  Msimamizi wa nane kwa ajili ya mwezi wa nane alikuwa Sibekai+ Mhusha kutoka kwa Wazera,+ na kikundi chake kilikuwa na watu 24,000. 12  Msimamizi wa tisa kwa ajili ya mwezi wa tisa alikuwa Abiezeri+ Mwanathothi+ kutoka kwa Wabenjamini, na kikundi chake kilikuwa na watu 24,000. 13  Msimamizi wa kumi kwa ajili ya mwezi wa kumi alikuwa Maharai+ Mnetofa kutoka kwa Wazera,+ na kikundi chake kilikuwa na watu 24,000. 14  Msimamizi wa 11 kwa ajili ya mwezi wa 11 alikuwa Benaya+ Mpirathoni kutoka kwa wana wa Efraimu, na kikundi chake kilikuwa na watu 24,000. 15  Msimamizi wa 12 kwa ajili ya mwezi wa 12 alikuwa Heldai Mnetofa, wa Othnieli, na kikundi chake kilikuwa na watu 24,000. 16  Hawa ndio waliokuwa viongozi wa makabila ya Israeli: Wa kabila la Rubeni, Eliezeri mwana wa Zikri; wa kabila la Simeoni, Shefatia mwana wa Maaka; 17  wa kabila la Lawi, Hashabia mwana wa Kemueli; wa wazao wa Haruni, Sadoki; 18  wa kabila la Yuda, Elihu,+ mmoja wa ndugu za Daudi; wa kabila la Isakari, Omri mwana wa Mikaeli; 19  wa kabila la Zabuloni, Ishmaya mwana wa Obadia; wa kabila la Naftali, Yerimothi mwana wa Azrieli; 20  wa kabila la Efraimu, Hoshea mwana wa Azazia; wa nusu ya kabila la Manase, Yoeli mwana wa Pedaya; 21  wa nusu ya kabila la Manase kule Gileadi, Ido mwana wa Zekaria; wa kabila la Benjamini, Yaasieli mwana wa Abneri;+ 22  wa kabila la Dani, Azareli mwana wa Yerohamu. Hao ndio waliokuwa wakuu wa makabila ya Israeli. 23  Daudi hakuwahesabu wale waliokuwa na umri wa miaka 20 kurudi chini, kwa sababu Yehova alikuwa ameahidi kwamba angewafanya Waisraeli wawe wengi kama nyota za mbinguni.+ 24  Yoabu mwana wa Seruya alikuwa ameanza kuwahesabu, lakini hakumaliza; hasira ya Mungu iliwaka dhidi ya Waisraeli kwa sababu ya jambo hilo,+ na idadi hiyo haikuandikwa katika masimulizi ya historia ya nyakati za Mfalme Daudi. 25  Azmavethi mwana wa Adieli ndiye aliyesimamia hazina za mfalme.+ Yonathani mwana wa Uzia alisimamia maghala yaliyokuwa* mashambani, katika majiji, vijijini, na katika minara. 26  Ezri mwana wa Kelubu aliwasimamia wafanyakazi waliolima mashamba. 27  Shimei Mrama alisimamia mashamba ya mizabibu; Zabdi Mshifi alisimamia maghala ya divai iliyotengenezwa kwa zabibu zilizozalishwa katika mashamba ya mizabibu. 28  Baal-hanani Mgederi alisimamia mashamba ya mizeituni na mikuyu+ katika Shefela;+ Yoashi alisimamia maghala ya mafuta. 29  Shitrai Msharoni alisimamia makundi ya ng’ombe yaliyolisha kule Sharoni,+ na Shafati mwana wa Adlai alisimamia makundi ya ng’ombe katika mabonde tambarare.* 30  Obili Mwishmaeli alisimamia ngamia; Yehdeya Mmeronothi alisimamia punda. 31  Yazizi Mhagri alisimamia makundi ya kondoo na mbuzi. Hao wote ndio waliokuwa wasimamizi wa mali za Mfalme Daudi. 32  Yonathani,+ mpwa wa Daudi, alikuwa mshauri, mwanamume mwenye uelewaji na pia mwandishi, na Yehieli mwana wa Hakmoni aliwatunza wana wa mfalme.+ 33  Ahithofeli+ alikuwa mshauri wa mfalme, na Hushai+ Mwarki alikuwa rafiki ya* mfalme. 34  Baada ya Ahithofeli kulikuwa na Yehoyada mwana wa Benaya+ na Abiathari;+ na Yoabu+ alikuwa mkuu wa jeshi la mfalme.

Maelezo ya Chini

Yaani, ukoo wa upande wa baba.
Tnn., “hazina zilizokuwa.”
Tnn., “nchi tambarare za chini.”
Au “msiri wa.”