Yohana 6:1-71
6 Baada ya mambo haya Yesu akaondoka kwenda ng’ambo ya bahari ya Galilaya, au Tiberia.+
2 Lakini umati mkubwa wakamfuata, kwa sababu walikuwa wakiona ishara alizokuwa akifanya juu ya wale waliokuwa wakiugua.+
3 Kwa hiyo Yesu akapanda mlimani,+ na hapo alikuwa ameketi pamoja na wanafunzi wake.
4 Sasa pasaka,+ ile sherehe ya Wayahudi, ilikuwa karibu.
5 Kwa hiyo, Yesu alipoinua macho yake na kuona kwamba umati mkubwa walikuwa wakimjia, akamwambia Filipo: “Tutanunua wapi mikate ili hawa wale?”+
6 Hata hivyo, alikuwa akisema hilo ili amjaribu, kwa maana yeye mwenyewe alijua alilokuwa karibu kufanya.
7 Filipo akamjibu: “Mikate yenye thamani ya dinari mia mbili haiwatoshi, hata kwamba kila mmoja aweze kupata kidogo.”+
8 Mmoja wa wanafunzi wake, Andrea ndugu ya Simoni Petro, akamwambia:
9 “Hapa yupo mvulana mdogo ambaye ana mikate mitano ya shayiri+ na samaki wadogo wawili. Lakini vitu hivi ni nini kwa watu wengi sana hivi?”+
10 Yesu akasema: “Waketisheni watu kama kwenye mlo.”+ Basi kulikuwa na majani mengi hapo. Kwa hiyo wanaume wakaketi, hesabu yao karibu elfu tano.+
11 Basi Yesu akachukua ile mikate na, baada ya kushukuru, akaigawanya kwa wale waliokuwa wameketi, vivyo hivyo pia wale samaki wadogo kadiri walivyotaka.+
12 Lakini walipokuwa wameshiba+ akawaambia wanafunzi wake: “Kusanyeni pamoja vipande ambavyo vimebaki, ili chochote kisipotee bure.”
13 Kwa hiyo wakavikusanya pamoja, nao wakajaza vikapu kumi na viwili kwa vipande vya mikate mitano ya shayiri, ambavyo vilibakizwa na wale waliokuwa wamekula.+
14 Kwa hiyo watu hao walipoona ishara alizofanya, wakaanza kusema: “Kwa hakika huyu ndiye nabii+ aliyepaswa kuja ulimwenguni.”
15 Kwa hiyo Yesu, akijua walikuwa karibu kuja kumkamata wamfanye kuwa mfalme, akaondoka+ tena kwenda mlimani akiwa peke yake.
16 Kulipokuwa jioni, wanafunzi wake wakashuka kwenda baharini,+
17 na, baada ya kupanda mashua, wakaondoka kwenda ng’ambo ya bahari ili waende Kapernaumu. Basi, kufikia sasa, giza lilikuwa limeingia na Yesu alikuwa bado hajaja mahali walipokuwa.
18 Pia, bahari ikaanza kuchafuka kwa sababu upepo wenye nguvu ulikuwa ukivuma.+
19 Hata hivyo, walipokuwa wamevuta makasia karibu kilometa tano au sita, wakamwona Yesu akitembea juu ya bahari akiwa anaikaribia mashua; nao wakaogopa.+
20 Lakini akawaambia: “Ni mimi; msiogope!”+
21 Kwa hiyo walikuwa na nia ya kumchukua ndani ya mashua, na mara hiyo mashua ikawa kwenye nchi kavu walikokuwa wakijaribu kwenda.+
22 Siku iliyofuata umati waliokuwa wamesimama upande ule mwingine wa bahari wakaona kwamba hapakuwa na mashua hapo ila moja ndogo, na kwamba Yesu hakuwa ameingia ndani ya mashua pamoja na wanafunzi wake bali wanafunzi wake tu ndio waliokuwa wameondoka;
23 lakini mashua kutoka Tiberia zilifika karibu na mahali ambapo walikula mkate baada ya Bwana kushukuru.
24 Kwa hiyo umati walipoona kwamba Yesu hakuwa hapo wala wanafunzi wake, wakapanda mashua zao ndogo wakaja mpaka Kapernaumu kumtafuta+ Yesu.
25 Kwa hiyo walipompata ng’ambo ya bahari wakamwambia: “Rabi,+ ulifika hapa wakati gani?”
26 Yesu akawajibu na kusema: “Kwa kweli kabisa ninawaambia ninyi, Mnanitafuta, si kwa sababu mliona ishara, bali kwa sababu mlikula mikate mkashiba.+
27 Fanyeni kazi, si kwa ajili ya chakula ambacho huharibika,+ bali kwa ajili ya chakula ambacho hudumu kufikia uzima wa milele,+ ambacho Mwana wa binadamu atawapa ninyi; kwa maana juu yake huyo, Baba, naam Mungu, ametia muhuri wake wa kibali.”+
28 Kwa hiyo wakamwambia: “Tutafanya nini ili tutende kazi za Mungu?”
29 Yesu akajibu, akawaambia: “Hii ndiyo kazi ya Mungu, kwamba mmwamini+ yule ambaye Huyo alimtuma.”+
30 Kwa hiyo wakamwambia: “Basi, wewe unafanya ishara+ gani, ili tuione, tukuamini? Ni kazi gani ambayo unafanya?
31 Mababu zetu walikula mana+ nyikani, kama vile ambavyo imeandikwa, ‘Aliwapa mkate kutoka mbinguni ili wale.’ ”+
32 Kwa sababu hiyo Yesu akawaambia: “Kwa kweli kabisa ninawaambia ninyi, Musa hakuwapa ninyi mkate kutoka mbinguni, lakini Baba yangu anawapa ninyi mkate wa kweli kutoka mbinguni.+
33 Kwa maana mkate wa Mungu ni yule ambaye hushuka kutoka mbinguni na kuupa ulimwengu uzima.”
34 Kwa hiyo wakamwambia: “Bwana, utupe sikuzote mkate huo.”+
35 Yesu akawaambia: “Mimi ndio mkate wa uzima. Yule ambaye huja kwangu hataona njaa hata kidogo, naye anayeniamini hatapata kiu kamwe.+
36 Lakini nimewaambia ninyi, hata mmeniona na bado hamwamini.+
37 Kila kitu anachonipa Baba kitakuja kwangu, naye anayekuja kwangu sitamfukuza kamwe;+
38 kwa sababu nimeshuka kutoka mbinguni+ kufanya, si mapenzi yangu, bali mapenzi yake aliyenituma.+
39 Haya ndiyo mapenzi yake aliyenituma, kwamba nisipoteze kitu chochote kati ya vyote ambavyo amenipa bali kwamba nikifufue+ katika siku ya mwisho.
40 Kwa maana haya ndiyo mapenzi ya Baba yangu, kwamba kila mtu ambaye humtazama Mwana na kumwamini awe na uzima wa milele,+ nami nitamfufua katika siku ya mwisho.”+
41 Kwa hiyo Wayahudi wakaanza kumnung’unikia kwa sababu alisema: “Mimi ndio mkate ambao ulishuka kutoka mbinguni”;+
42 nao wakaanza kusema:+ “Je, huyu si Yesu mwana wa Yosefu,+ ambaye baba na mama yake sisi tunawajua? Anawezaje sasa kusema, ‘Mimi nimeshuka kutoka mbinguni’?”
43 Yesu akajibu, akawaambia: “Acheni kunung’unika kati yenu wenyewe.
44 Hakuna mtu anayeweza kuja kwangu isipokuwa Baba, aliyenituma, amvute;+ nami nitamfufua siku ya mwisho.+
45 Imeandikwa katika Manabii, ‘Na wote watafundishwa na Yehova.’+ Kila mtu ambaye amesikia kutoka kwa Baba na ambaye amejifunza huja kwangu.+
46 Si kwamba mwanadamu yeyote amemwona Baba,+ ila yule aliyetoka kwa Mungu; huyo amemwona Baba.+
47 Kwa kweli kabisa ninawaambia, Yule ambaye huamini ana uzima wa milele.+
48 “Mimi ndio mkate+ wa uzima.
49 Mababu zenu walikula mana+ nyikani na bado wakafa.
50 Huu ndio mkate ambao hushuka kutoka mbinguni, ili yeyote apate kuula na asife.
51 Mimi ndio mkate ulio hai ulioshuka kutoka mbinguni; yeyote akila mkate huu ataishi milele; na, kwa kweli, mkate ambao nitatoa ni mwili+ wangu kwa ajili ya uzima wa ulimwengu.”+
52 Kwa hiyo Wayahudi wakaanza kushindana, wakisema: “Mtu huyu anawezaje kutupa mwili wake tule?”
53 Basi Yesu akawaambia: “Kwa kweli kabisa ninawaambia, Ninyi msipoula mwili+ wa Mwana wa binadamu na kunywa damu+ yake, hamna uzima+ ndani yenu wenyewe.
54 Yule ambaye hula mwili wangu na kunywa damu yangu ana uzima wa milele, nami nitamfufua+ katika siku ya mwisho;
55 kwa maana mwili wangu ni chakula cha kweli, na damu yangu ni kinywaji cha kweli.
56 Yule ambaye hula mwili wangu na kunywa damu yangu hukaa katika muungano nami, na mimi katika muungano naye.+
57 Kama vile Baba aliye hai+ alivyonituma, nami ninaishi kwa sababu ya Baba, yule ambaye pia hunila mimi, hata huyo ataishi kwa sababu yangu.+
58 Huu ndio mkate ulioshuka kutoka mbinguni. Si kama wakati mababu zenu walipokula na bado wakafa. Yule ambaye hula mkate huu ataishi milele.”+
59 Mambo haya aliyasema alipokuwa akifundisha katika kusanyiko la watu wote katika Kapernaumu.
60 Kwa hiyo wengi kati ya wanafunzi wake, waliposikia hilo, wakasema: “Maneno hayo yanashtua; ni nani ambaye anaweza kuyasikiliza?”+
61 Lakini Yesu, akijua ndani yake mwenyewe kwamba wanafunzi wake walikuwa wakinung’unika juu ya hili, akawaambia: “Je, jambo hili linawakwaza+ ninyi?
62 Kwa hiyo, namna gani ikiwa mtamwona Mwana wa binadamu akipanda kwenda alikokuwa mapema?+
63 Roho ndiyo inayotokeza uzima;+ mwili hauna faida hata kidogo. Maneno ambayo nimewaambia ni roho+ na ni uzima.+
64 Lakini kuna wengine kati yenu ambao hawaamini.” Kwa maana tangu mwanzo Yesu alijua ni nani wale waliokuwa hawaamini na ni nani angemsaliti.+
65 Kwa hiyo akaendelea kusema: “Hii ndiyo sababu nimewaambia ninyi, Hakuna anayeweza kuja kwangu isipokuwa aruhusiwe na Baba.”+
66 Kwa sababu ya hili wengi kati ya wanafunzi wake wakaenda zao kwenye mambo yaliyo nyuma+ wakawa hawatembei tena pamoja naye.+
67 Kwa hiyo Yesu akawaambia wale kumi na wawili: “Je, ninyi pia mnataka kwenda?”
68 Simoni Petro+ akamjibu: “Bwana, tutaenda kwa nani?+ Wewe una maneno ya uzima wa milele;+
69 na sisi tumeamini na tumejua kwamba wewe ndiye Mtakatifu wa Mungu.”+
70 Yesu akawajibu: “Niliwachagua ninyi kumi na wawili,+ sivyo? Lakini mmoja wenu ni mchongezi.”+
71 Kwa kweli, alikuwa akisema juu ya Yuda mwana wa Simoni Iskariote; kwa maana huyu alikuwa karibu kumsaliti,+ ajapokuwa mmoja wa wale kumi na wawili.