Yohana 4:1-54

4  Basi, Bwana alipojua kwamba Mafarisayo walikuwa wamesikia kwamba Yesu alikuwa akifanya na kubatiza+ wanafunzi wengi kuliko Yohana​—  ijapokuwa, kwa kweli, Yesu mwenyewe hakuwa akibatiza ila wanafunzi wake ndio waliokuwa wakibatiza⁠—  aliondoka Yudea na kuelekea tena Galilaya.  Lakini ilikuwa lazima apitie Samaria.+  Basi akaja mpaka jiji moja la Samaria linaloitwa Sikari karibu na shamba ambalo Yakobo alimpa Yosefu mwana wake.+  Kwa kweli, chemchemi+ ya Yakobo ilikuwa hapo. Basi Yesu, kwa kuwa alikuwa amechoka kwa sababu ya safari hiyo, alikuwa ameketi kando ya chemchemi kama vile alivyokuwa. Ilikuwa karibu saa sita.  Mwanamke mmoja wa Samaria akaja kuteka maji. Yesu akamwambia: “Nipe maji ninywe.”  (Kwa maana wanafunzi wake walikuwa wameenda katika jiji kununua chakula.)  Kwa hiyo mwanamke huyo Msamaria akamwambia: “Wewe, ujapokuwa Myahudi, unawezaje kuniomba maji ya kunywa, na mimi ni mwanamke Msamaria?” (Kwa maana Wayahudi hawana shughuli na Wasamaria.)+ 10  Yesu akajibu, akamwambia: “Kama ungalijua zawadi+ ya bure inayotoka kwa Mungu, na ni nani+ ambaye anakuambia, ‘Nipe maji ninywe,’ ungalimwomba, naye angalikupa maji yaliyo hai.”+ 11  Akamwambia: “Bwana, huna hata ndoo ya kutekea maji, na kisima ni kirefu. Kwa hiyo, umeyatoa wapi maji hayo yaliyo hai? 12  Je, wewe ni mkuu+ kuliko babu yetu Yakobo, ambaye alitupa kisima hiki na ambaye yeye mwenyewe pamoja na wanawe na mifugo yake walikunywa maji yake?” 13  Yesu akajibu, akamwambia: “Kila mtu anayekunywa maji haya atapatwa na kiu tena. 14  Yule atakayekunywa maji ambayo nitampa hatapatwa na kiu hata kidogo,+ lakini maji ambayo nitampa yatakuwa chemchemi ya maji+ ndani yake, inayobubujika ili kutokeza uzima wa milele.”+ 15  Huyo mwanamke akamwambia: “Bwana, nipe maji hayo, ili nisiwe na kiu wala nisiendelee kuja hapa kuteka maji.” 16  Akamwambia: “Nenda, ukamwite mume wako mje hapa.” 17  Mwanamke huyo akajibu akasema: “Sina mume.” Yesu akamwambia: “Umesema vema, ‘Sina mume.’ 18  Kwa maana umekuwa na waume watano, na mwanamume uliye naye sasa si mume wako. Hapo umesema kweli.” 19  Huyo mwanamke akamwambia: “Bwana, ninaona kwamba wewe ni nabii.+ 20  Mababu zetu waliabudu katika mlima huu;+ lakini ninyi husema kwamba Yerusalemu ndipo mahali ambapo watu wanapaswa kuabudia.”+ 21  Yesu akamwambia: “Niamini mimi, mwanamke, Saa inakuja wakati ambapo mtamwabudu+ Baba si katika mlima huu wala kule Yerusalemu.+ 22  Ninyi mnaabudu msichokijua; sisi tunaabudu tunachokijua,+ kwa sababu wokovu hutokana na Wayahudi.+ 23  Hata hivyo, saa inakuja, nayo ipo sasa, wakati ambapo waabudu wa kweli watamwabudu Baba kwa roho+ na kweli,+ kwa maana, kwa kweli, Baba anawatafuta watu wa namna hiyo wamwabudu.+ 24  Mungu ni Roho,+ na wale wanaomwabudu lazima wamwabudu kwa roho na kweli.”+ 25  Huyo mwanamke akamwambia: “Ninajua kwamba Masihi+ anakuja, anayeitwa Kristo.+ Atakapofika, atatujulisha mambo yote waziwazi.” 26  Yesu akamwambia: “Mimi ninayesema nawe ndiye.”+ 27  Ndipo wanafunzi wake wakafika, nao wakaanza kustaajabu kwa sababu alikuwa akisema na mwanamke. Bila shaka, hakuna yeyote aliyesema: “Unatafuta nini?” au, “Kwa nini unaongea naye?” 28  Kwa hiyo, mwanamke huyo akauacha mtungi wake wa maji akaenda zake jijini na kuwaambia watu: 29  “Njooni hapa, mwone mtu aliyeniambia mambo yote niliyofanya. Je, huyu labda ndiye Kristo?”+ 30  Wakatoka jijini na kumwendea. 31  Wakati huohuo wanafunzi walikuwa wakimhimiza, wakisema: “Rabi,+ kula.” 32  Lakini akawaambia: “Mimi nina chakula ambacho hamkijui.” 33  Kwa hiyo wanafunzi wakaanza kusemezana: “Je, kuna mtu ambaye amemletea chakula chochote?” 34  Yesu akawaambia: “Chakula+ changu ni mimi kufanya mapenzi+ yake aliyenituma na kuimaliza kazi yake.+ 35  Je, ninyi hamsemi kwamba bado kuna miezi minne kabla ya mavuno kuja? Tazama! Ninawaambia ninyi: Inueni macho yenu myatazame mashamba, kwamba ni meupe kwa ajili ya kuvunwa.+ Tayari 36  mvunaji anapokea mshahara na kukusanya matunda kwa ajili ya uzima wa milele,+ ili mpandaji+ na mvunaji wapate kushangilia pamoja.+ 37  Katika habari hii, kwa kweli, maneno haya ni kweli, Mpandaji ni mmoja na mvunaji ni mwingine. 38  Niliwatuma ninyi mkavune kile ambacho hamkufanyia kazi. Wengine wamefanya kazi,+ nanyi mmeingia katika faida ya kazi yao.” 39  Sasa wengi wa Wasamaria kutoka jiji hilo walimwamini+ kwa sababu ya neno la yule mwanamke aliyesema hivi kwa ushahidi: “Aliniambia mambo yote niliyofanya.”+ 40  Kwa hiyo Wasamaria walipomjia, wakaanza kumwomba akae pamoja nao; naye akakaa huko siku mbili.+ 41  Kwa hiyo wengi zaidi wakaamini kwa ajili ya aliyoyasema,+ 42  nao wakaanza kumwambia yule mwanamke: “Hatuamini tena kwa sababu ya maneno yako; kwa maana sisi wenyewe+ tumesikia nasi tunajua kwamba mtu huyu kwa hakika ndiye mwokozi+ wa ulimwengu.” 43  Baada ya hizo siku mbili akaondoka huko kwenda Galilaya.+ 44  Hata hivyo, Yesu alitoa ushahidi kwamba nabii hapati heshima katika nchi yake mwenyewe.+ 45  Kwa hiyo, alipofika Galilaya, Wagalilaya wakampokea, kwa sababu walikuwa wameona mambo yote aliyofanya Yerusalemu kwenye sherehe,+ kwa maana wao pia walikuwa wameenda kwenye sherehe.+ 46  Basi akaja tena mpaka Kana+ ya Galilaya, ambako alikuwa amegeuza maji yakawa divai.+ Basi kulikuwako mtumishi fulani wa mfalme ambaye mwana wake alikuwa mgonjwa katika Kapernaumu.+ 47  Mtu huyu aliposikia kwamba Yesu alikuwa amekuja kutoka Yudea kuingia Galilaya, akamwendea na kuanza kumwomba ashuke ili amponye mwana wake, kwa maana alikuwa karibu kufa. 48  Hata hivyo, Yesu akamwambia: “Msipoona ishara+ na maajabu,+ hamtaamini kamwe.” 49  Mtumishi wa mfalme akamwambia: “Bwana, shuka uje kabla mtoto wangu mchanga hajafa.” 50  Yesu akamwambia: “Shika njia uende zako;+ mwana wako yuko hai.”+ Yule mtu akaliamini neno ambalo Yesu alikuwa amemwambia, akashika njia na kwenda zake. 51  Lakini tayari alipokuwa akishuka kwenda zake watumwa wake wakakutana naye ili kusema kwamba mvulana wake alikuwa hai.+ 52  Kwa hiyo akaanza kuwauliza saa ambayo alipata nafuu. Basi wakamwambia: “Jana saa saba homa+ ilimwacha.” 53  Kwa hiyo yule baba akajua ilikuwa saa+ ileile ambayo Yesu alimwambia: “Mwana wako yuko hai.” Kisha yeye na watu wote wa nyumbani mwake wakaamini.+ 54  Tena hiyo ilikuwa ndiyo ishara+ ya pili aliyoifanya Yesu alipokuja kutoka Yudea na kuingia Galilaya.

Maelezo ya Chini