Yohana 3:1-36
3 Basi kulikuwa na mtu mmoja kati ya Mafarisayo, aliyeitwa Nikodemo,+ mtawala wa Wayahudi.
2 Huyo alimjia wakati wa usiku+ na kumwambia: “Rabi,+ tunajua kwamba wewe ukiwa mwalimu+ umekuja kutoka kwa Mungu;+ kwa maana hakuna anayeweza kufanya ishara+ hizi ambazo unafanya isipokuwa Mungu awe pamoja naye.”+
3 Yesu akajibu akamwambia:+ “Kwa kweli kabisa ninakuambia, Mtu asipozaliwa tena,+ hawezi kuuona ufalme wa Mungu.”+
4 Nikodemo akamwambia: “Mtu anawezaje kuzaliwa akiwa mzee? Je, anaweza kuingia katika tumbo la uzazi la mama yake mara ya pili na kuzaliwa?”
5 Yesu akajibu: “Kwa kweli kabisa ninakuambia, Mtu asipozaliwa kwa maji+ na roho,+ hawezi kuingia katika ufalme wa Mungu.
6 Kile ambacho kimezaliwa kwa mwili ni mwili, na kile ambacho kimezaliwa kwa roho ni roho.+
7 Usistaajabu kwa sababu nimekuambia, Ninyi lazima mzaliwe tena.+
8 Upepo+ huvuma mahali ambapo unataka, nawe unasikia mvumo wake, lakini hujui mahali ambapo huo unatoka wala mahali unapoenda. Ndivyo alivyo kila mtu ambaye amezaliwa kwa roho.”+
9 Nikodemo akajibu, akamwambia: “Mambo haya yanaweza kutukia jinsi gani?”
10 Yesu akajibu, akamwambia: “Je, wewe ni mwalimu wa Israeli na bado hujui mambo haya?+
11 Kwa kweli kabisa ninakuambia, Yale tunayoyajua tunayasema na yale ambayo tumeyaona tunatoa ushahidi+ juu yake, lakini ninyi hampokei ushahidi ambao tunatoa.+
12 Ikiwa nimewaambia ninyi mambo ya duniani na bado hamwamini, mtaamini jinsi gani nikiwaambia mambo ya mbinguni?+
13 Zaidi ya hayo, hakuna mtu ambaye amepanda kuingia mbinguni+ ila yule aliyeshuka kutoka mbinguni,+ Mwana wa binadamu.+
14 Na kama vile Musa alivyoinua nyoka+ nyikani, ndivyo Mwana wa binadamu atakavyoinuliwa,+
15 ili kila mtu anayemwamini apate kuwa na uzima wa milele.+
16 “Kwa maana Mungu aliupenda+ ulimwengu sana hivi kwamba akamtoa Mwana wake mzaliwa-pekee,+ ili kila mtu anayemwamini+ asiangamizwe+ bali awe na uzima wa milele.+
17 Kwa maana Mungu alimtuma Mwana wake ulimwenguni, si ili auhukumu+ ulimwengu, bali ili ulimwengu uokolewe+ kupitia kwake.
18 Yule anayemwamini hatahukumiwa.+ Yule ambaye hamwamini amehukumiwa tayari, kwa sababu hana imani katika jina la Mwana mzaliwa-pekee wa Mungu.+
19 Basi huu ndio msingi wa hukumu, kwamba nuru+ imekuja ulimwenguni+ lakini watu wamelipenda giza kuliko nuru,+ kwa maana matendo yao yalikuwa maovu.
20 Kwa maana yule ambaye huzoea kufanya mambo maovu+ huchukia nuru na haji kwenye nuru, ili matendo yake yasipate kukaripiwa.+
21 Lakini yule ambaye hufanya yaliyo ya kweli huja kwenye nuru,+ ili matendo yake yapate kufunuliwa kuwa tayari yamefanywa kupatana na Mungu.”
22 Baada ya mambo haya Yesu na wanafunzi wake wakaenda katika nchi ya Yudea, na huko akatumia wakati fulani pamoja nao naye alikuwa akibatiza.+
23 Lakini Yohana+ pia alikuwa akibatiza katika Ainoni karibu na Salimu, kwa sababu kulikuwa na kiasi kikubwa cha maji+ huko, na watu wakawa wakija na kubatizwa;+
24 kwa maana Yohana alikuwa hajatupwa gerezani bado.+
25 Kwa hiyo bishano likatokea kati ya wanafunzi wa Yohana na Myahudi mmoja kuhusu utakaso.+
26 Kwa hiyo wakaja kwa Yohana na kumwambia: “Rabi, mtu aliyekuwa pamoja nawe ng’ambo ya Yordani, ambaye umetoa ushahidi+ juu yake, ona, huyu anabatiza na wote wanamwendea.”+
27 Yohana akajibu, akasema: “Mtu hawezi kupokea hata kitu kimoja isipokuwa awe amepewa kutoka mbinguni.+
28 Ninyi wenyewe mnanitolea ushahidi kwamba nilisema, Mimi siye Kristo,+ bali, nimetumwa kumtangulia huyo.+
29 Yeye aliye na bibi-arusi ndiye bwana-arusi.+ Hata hivyo, rafiki ya bwana-arusi, anaposimama na kumsikia, ana shangwe nyingi sana kwa sababu ya sauti ya bwana-arusi. Kwa hiyo shangwe yangu hii imejazwa.+
30 Lazima huyo aendelee kuongezeka, lakini mimi lazima niendelee kupungua.”
31 Yule anayekuja kutoka juu yuko juu ya wengine wote.+ Yule anayetoka duniani ni wa kutoka duniani na husema kuhusu mambo ya duniani.+ Yule anayekuja kutoka mbinguni yuko juu ya wengine wote.+
32 Kile ambacho ameona na kusikia, yeye hutoa ushahidi juu yake,+ lakini hakuna mtu anayekubali ushahidi wake.+
33 Yule ambaye ameukubali ushahidi wake ametia muhuri wake juu ya huo kwamba Mungu ni wa kweli.+
34 Kwa maana yule ambaye Mungu amemtuma husema maneno ya Mungu,+ kwa maana hatoi roho kwa kipimio.+
35 Baba humpenda Mwana+ naye ametia vitu vyote mkononi mwake.+
36 Yule anayemwamini+ Mwana ana uzima wa milele;+ yule asiyemtii Mwana hataona uzima,+ bali ghadhabu ya Mungu hukaa juu yake.+