Yohana 20:1-31
20 Siku ya kwanza+ ya juma Maria Magdalene akaja mapema kwenye kaburi, kulipokuwa na giza bado, naye akaona jiwe likiwa tayari limeondolewa kutoka kwenye kaburi.+
2 Kwa hiyo akakimbia na kuja kwa Simoni Petro na kwa yule mwanafunzi+ mwingine, ambaye Yesu alikuwa anampenda, naye akawaambia: “Wamemwondoa Bwana kutoka katika kaburi,+ nasi hatujui wamemlaza wapi.”
3 Ndipo Petro+ na yule mwanafunzi mwingine wakatoka kwenda kaburini.
4 Ndiyo, hao wawili pamoja wakaanza kukimbia; lakini yule mwanafunzi mwingine akakimbia mbele ya Petro mbio zaidi naye akafika kaburini kwanza.
5 Naye akainama, akaona vitambaa vikiwa chini humo,+ lakini hakuingia.
6 Ndipo Simoni Petro pia akaja akimfuata, naye akaingia ndani ya kaburi. Naye akaona vitambaa vikiwa chini humo,+
7 pia nguo iliyokuwa juu ya kichwa chake haikuwapo pamoja na vitambaa bali ilikuwa imekunjwa ikiwa peke yake.
8 Kwa hiyo, wakati huo mwanafunzi yule mwingine aliyekuwa amefika kwanza kwenye kaburi akaingia pia, naye akaona na kuamini.
9 Kwa maana bado hawakufahamu andiko kwamba lazima afufuliwe kutoka kwa wafu.+
10 Na kwa hiyo wanafunzi wakarudi nyumbani kwao.
11 Hata hivyo, Maria akaendelea kusimama nje karibu na kaburi, akilia. Ndipo, alipokuwa akilia, akainama kutazama ndani ya kaburi
12 naye akaona malaika+ wawili waliokuwa wamevaa mavazi meupe wakiwa wameketi mmoja kichwani na mwingine miguuni ambapo mwili wa Yesu ulikuwa umelazwa.
13 Nao wakamwambia: “Mwanamke, kwa nini unalia?” Akawaambia: “Wamemwondoa Bwana wangu, nami sijui wamemlaza wapi.”
14 Baada ya kusema hayo, akageuka na kumwona Yesu akiwa amesimama, lakini hakufahamu ni Yesu.+
15 Yesu akamwambia: “Mwanamke, kwa nini unalia? Unamtafuta nani?”+ Yeye, akiwaza ni mtunza-bustani, akamwambia: “Bwana, ikiwa umemchukua, niambie umemlaza wapi, nami nitamwondoa.”
16 Yesu akamwambia: “Maria!”+ Alipogeuka, Maria akamwambia, katika Kiebrania: “Raboni!”+ (ambalo linamaanisha “Mwalimu!”)
17 Yesu akamwambia: “Acha kuning’ang’ania. Kwa maana bado sijapanda kwenda kwa Baba. Lakini nenda kwa ndugu+ zangu, nawe uwaambie, ‘Mimi ninapanda kwenda kwa Baba+ yangu na Baba yenu na kwa Mungu wangu+ na Mungu wenu.’ ”+
18 Maria Magdalene akaja na kuleta habari hizo kwa wanafunzi: “Nimemwona Bwana!” na kwamba alimwambia mambo hayo.+
19 Kwa hiyo, ilipokuwa jioni-jioni siku hiyo, siku ya kwanza ya juma,+ na, ijapokuwa milango ilikuwa imefungwa mahali ambamo wanafunzi walikuwa kwa sababu ya kuwaogopa+ Wayahudi, Yesu alikuja+ na kusimama katikati yao na kuwaambia: “Na muwe na amani.”+
20 Na baada ya kusema hayo, akawaonyesha mikono yake miwili na ubavu wake.+ Basi wanafunzi hao wakashangilia+ kwa kumwona Bwana.
21 Kwa hiyo, Yesu akawaambia tena: “Na muwe na amani. Kama vile ambavyo Baba amenituma,+ mimi pia ninawatuma ninyi.”+
22 Na baada ya kusema jambo hilo akapuliza juu yao na kuwaambia: “Pokeeni roho takatifu.+
23 Mkisamehe dhambi za watu wowote,+ watakuwa wamesamehewa; msiposamehe zile za watu wowote, watakuwa hawajasamehewa.”+
24 Lakini Tomasi,+ mmoja wa wale kumi na wawili, aliyeitwa Pacha, hakuwa pamoja nao Yesu alipokuja.
25 Kwa hiyo wanafunzi wengine wakawa wanamwambia: “Tumemwona Bwana!” Lakini yeye akawaambia: “Nisipoona katika mikono yake alama ya misumari na nitie kidole changu katika alama ya misumari na kuutia mkono wangu ndani ya ubavu wake,+ hakika mimi sitaamini.”+
26 Basi, siku nane baadaye wanafunzi wake walikuwa tena ndani ya nyumba, naye Tomasi alikuwa pamoja nao. Yesu akaja, ijapokuwa milango ilikuwa imefungwa, naye akasimama katikati yao, akasema: “Na muwe na amani.”+
27 Halafu akamwambia Tomasi: “Weka kidole chako hapa, uone mikono yangu, na chukua mkono+ wako utie ndani ya ubavu wangu, na uache kuwa asiyeamini bali uwe mwenye kuamini.”
28 Tomasi akajibu akamwambia: “Bwana wangu na Mungu wangu!”+
29 Yesu akamwambia: “Kwa sababu umeniona je, umeamini? Wenye furaha ni wale ambao hawaoni na bado wanaamini.”+
30 Kwa hakika, Yesu alifanya pia ishara nyingine nyingi mbele ya wanafunzi hao, ambazo hazikuandikwa katika kitabu hiki cha kukunjwa.+
31 Lakini haya yameandikwa+ ili mpate kuamini kwamba Yesu ndiye Kristo Mwana wa Mungu, na kwamba, kwa sababu ya kuamini,+ mpate kuwa na uzima kupitia jina lake.