Yohana 20:1-31

20  Siku ya kwanza+ ya juma Maria Magdalene akaja mapema kwenye kaburi, kulipokuwa na giza bado, naye akaona jiwe likiwa tayari limeondolewa kutoka kwenye kaburi.+  Kwa hiyo akakimbia na kuja kwa Simoni Petro na kwa yule mwanafunzi+ mwingine, ambaye Yesu alikuwa anampenda, naye akawaambia: “Wamemwondoa Bwana kutoka katika kaburi,+ nasi hatujui wamemlaza wapi.”  Ndipo Petro+ na yule mwanafunzi mwingine wakatoka kwenda kaburini.  Ndiyo, hao wawili pamoja wakaanza kukimbia; lakini yule mwanafunzi mwingine akakimbia mbele ya Petro mbio zaidi naye akafika kaburini kwanza.  Naye akainama, akaona vitambaa vikiwa chini humo,+ lakini hakuingia.  Ndipo Simoni Petro pia akaja akimfuata, naye akaingia ndani ya kaburi. Naye akaona vitambaa vikiwa chini humo,+  pia nguo iliyokuwa juu ya kichwa chake haikuwapo pamoja na vitambaa bali ilikuwa imekunjwa ikiwa peke yake.  Kwa hiyo, wakati huo mwanafunzi yule mwingine aliyekuwa amefika kwanza kwenye kaburi akaingia pia, naye akaona na kuamini.  Kwa maana bado hawakufahamu andiko kwamba lazima afufuliwe kutoka kwa wafu.+ 10  Na kwa hiyo wanafunzi wakarudi nyumbani kwao. 11  Hata hivyo, Maria akaendelea kusimama nje karibu na kaburi, akilia. Ndipo, alipokuwa akilia, akainama kutazama ndani ya kaburi 12  naye akaona malaika+ wawili waliokuwa wamevaa mavazi meupe wakiwa wameketi mmoja kichwani na mwingine miguuni ambapo mwili wa Yesu ulikuwa umelazwa. 13  Nao wakamwambia: “Mwanamke, kwa nini unalia?” Akawaambia: “Wamemwondoa Bwana wangu, nami sijui wamemlaza wapi.” 14  Baada ya kusema hayo, akageuka na kumwona Yesu akiwa amesimama, lakini hakufahamu ni Yesu.+ 15  Yesu akamwambia: “Mwanamke, kwa nini unalia? Unamtafuta nani?”+ Yeye, akiwaza ni mtunza-bustani, akamwambia: “Bwana, ikiwa umemchukua, niambie umemlaza wapi, nami nitamwondoa.” 16  Yesu akamwambia: “Maria!”+ Alipogeuka, Maria akamwambia, katika Kiebrania: “Raboni!”+ (ambalo linamaanisha “Mwalimu!”) 17  Yesu akamwambia: “Acha kuning’ang’ania. Kwa maana bado sijapanda kwenda kwa Baba. Lakini nenda kwa ndugu+ zangu, nawe uwaambie, ‘Mimi ninapanda kwenda kwa Baba+ yangu na Baba yenu na kwa Mungu wangu+ na Mungu wenu.’ ”+ 18  Maria Magdalene akaja na kuleta habari hizo kwa wanafunzi: “Nimemwona Bwana!” na kwamba alimwambia mambo hayo.+ 19  Kwa hiyo, ilipokuwa jioni-jioni siku hiyo, siku ya kwanza ya juma,+ na, ijapokuwa milango ilikuwa imefungwa mahali ambamo wanafunzi walikuwa kwa sababu ya kuwaogopa+ Wayahudi, Yesu alikuja+ na kusimama katikati yao na kuwaambia: “Na muwe na amani.”+ 20  Na baada ya kusema hayo, akawaonyesha mikono yake miwili na ubavu wake.+ Basi wanafunzi hao wakashangilia+ kwa kumwona Bwana. 21  Kwa hiyo, Yesu akawaambia tena: “Na muwe na amani. Kama vile ambavyo Baba amenituma,+ mimi pia ninawatuma ninyi.”+ 22  Na baada ya kusema jambo hilo akapuliza juu yao na kuwaambia: “Pokeeni roho takatifu.+ 23  Mkisamehe dhambi za watu wowote,+ watakuwa wamesamehewa; msiposamehe zile za watu wowote, watakuwa hawajasamehewa.”+ 24  Lakini Tomasi,+ mmoja wa wale kumi na wawili, aliyeitwa Pacha, hakuwa pamoja nao Yesu alipokuja. 25  Kwa hiyo wanafunzi wengine wakawa wanamwambia: “Tumemwona Bwana!” Lakini yeye akawaambia: “Nisipoona katika mikono yake alama ya misumari na nitie kidole changu katika alama ya misumari na kuutia mkono wangu ndani ya ubavu wake,+ hakika mimi sitaamini.”+ 26  Basi, siku nane baadaye wanafunzi wake walikuwa tena ndani ya nyumba, naye Tomasi alikuwa pamoja nao. Yesu akaja, ijapokuwa milango ilikuwa imefungwa, naye akasimama katikati yao, akasema: “Na muwe na amani.”+ 27  Halafu akamwambia Tomasi: “Weka kidole chako hapa, uone mikono yangu, na chukua mkono+ wako utie ndani ya ubavu wangu, na uache kuwa asiyeamini bali uwe mwenye kuamini.” 28  Tomasi akajibu akamwambia: “Bwana wangu na Mungu wangu!”+ 29  Yesu akamwambia: “Kwa sababu umeniona je, umeamini? Wenye furaha ni wale ambao hawaoni na bado wanaamini.”+ 30  Kwa hakika, Yesu alifanya pia ishara nyingine nyingi mbele ya wanafunzi hao, ambazo hazikuandikwa katika kitabu hiki cha kukunjwa.+ 31  Lakini haya yameandikwa+ ili mpate kuamini kwamba Yesu ndiye Kristo Mwana wa Mungu, na kwamba, kwa sababu ya kuamini,+ mpate kuwa na uzima kupitia jina lake.

Maelezo ya Chini