Yohana 2:1-25

2  Basi siku ya tatu kulikuwa na karamu ya ndoa katika Kana+ ya Galilaya, na mama+ ya Yesu alikuwa huko.  Yesu na wanafunzi wake walialikwa pia kwenye karamu hiyo ya ndoa.  Divai ilipopungua mama+ ya Yesu akamwambia: “Hawana divai.”  Lakini Yesu akamwambia: “Nina nini nawe, mwanamke?+ Saa yangu haijafika bado.”+  Mama yake akawaambia wale wenye kuhudumia: “Lolote atakalowaambia, fanyeni.”+  Kama ilivyokuwa, kulikuwako mitungi sita ya maji ikiwa imekaa hapo kulingana na kanuni za utakaso+ za Wayahudi, kila mmoja ukiwa unaweza kuchukua vipimo viwili au vitatu vya maji.  Yesu akawaambia: “Ijazeni maji mitungi ya maji.” Nao wakaijaza pomoni.  Akawaambia: “Choteni kiasi fulani sasa na kumpelekea msimamizi wa karamu.” Kwa hiyo wakayapeleka.  Basi, msimamizi wa karamu alipoyaonja maji yaliyokuwa yamegeuzwa kuwa divai,+ lakini hakujua chanzo chake, ijapokuwa wale wenye kuhudumia waliokuwa wamechota hayo maji walijua, msimamizi wa karamu akamwita bwana-arusi 10  na kumwambia: “Wengine wote hutoa divai nzuri kwanza,+ na ile hafifu wakati ambapo watu wameingiwa na kileo. Wewe umehifadhi divai nzuri mpaka sasa.” 11  Yesu alifanya jambo hilo katika Kana ya Galilaya likiwa mwanzo wa ishara zake, naye akaufunua utukufu+ wake; na wanafunzi wake wakamwamini. 12  Baada ya hayo, yeye na mama yake na ndugu zake+ na wanafunzi wake wakashuka kwenda Kapernaumu,+ lakini hawakukaa huko siku nyingi. 13  Basi pasaka+ ya Wayahudi ilikuwa karibu, na Yesu akapanda kwenda Yerusalemu.+ 14  Naye akakuta hekaluni wale waliokuwa wakiuza ng’ombe na kondoo na njiwa+ na waliokuwa wakivunja pesa wakiwa wameketi. 15  Kwa hiyo, baada ya kufanya mjeledi wa kamba, akawafukuza hekaluni wale wote wenye kondoo na ng’ombe, akamwaga sarafu za waliokuwa wakibadili pesa na kupindua meza zao.+ 16  Akawaambia wale waliokuwa wakiuza njiwa: “Ondoeni vitu hivi kutoka hapa! Acheni kuifanya nyumba+ ya Baba yangu kuwa nyumba ya biashara!”+ 17  Wanafunzi wake wakakumbuka kwamba imeandikwa: “Bidii kwa ajili ya nyumba yako itanila.”+ 18  Kwa hiyo, Wayahudi wakajibu, wakamwambia: “Una ishara+ gani ya kutuonyesha, kwa kuwa unafanya mambo haya?” 19  Yesu akajibu, akawaambia: “Libomoeni hekalu+ hili, na katika siku tatu nitalisimamisha.” 20  Kwa hiyo Wayahudi wakasema: “Hekalu hili lilijengwa kwa miaka 46, nawe je, utalisimamisha katika siku tatu?” 21  Lakini alikuwa akiongea juu ya hekalu+ la mwili wake. 22  Ingawa hivyo, wakati alipofufuliwa kutoka kwa wafu, wanafunzi wake wakakumbuka+ kwamba alikuwa akisema hilo; nao wakaamini Andiko na maneno ambayo Yesu alisema. 23  Hata hivyo, wakati alipokuwa Yerusalemu kwenye pasaka, kwenye sherehe+ yake, watu wengi wakawa na imani katika jina lake,+ wakitazama ishara zake alizokuwa akifanya.+ 24  Lakini Yesu mwenyewe hakuwa akiwatumaini+ kwa sababu aliwajua wote 25  na kwa sababu hakuwa na uhitaji wa mtu yeyote kutoa ushahidi juu ya mwanadamu, kwa maana yeye mwenyewe alijua kile kilichokuwa ndani ya mwanadamu.+

Maelezo ya Chini